image

Kutokana kwenye kisima mpaka kuwa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME.

Pale kisimani khalidi aliokolewa na majini waliokuwa wakiishi pale kwa muda wa miaka mingi iliyopita. Hata kabla ya kufika chini walimzi,isha na kumbebe na kumtua kidogokidogo na hakupatwa na madhara. Majini hawa walimpenda Khalidi kwa tabia zake njema na ukarimu uliopambwa na uchamungu wake. Hivyo hawakupenda damu ya mtu mkarimu iumwagike mule kisimani walipokuwa wakiishi.

 

Basi alipokuwa kati ya kupoteza fahamu na kurudi fahamu yaani akiwa kwenye mang’amung’amu akawasikia majini wakizungumza. “unajuwa mtoto wa mfalme wa nchi hii anaumwa sana na inapata miezi sita sasa bila ya kupona” wengine wakawa wanajibu “mimi sijapata kusikia hilo kabisa” kukatokea mmoja akasema “mimi nafahamu dawa ya ugonjwa wake” basi pale yule aliye anzisha mada akamuuliza “ni ipi dawa yake?” akamjibu “nyumbani kwa Khalidi kuna paka mwenye rangi nne na adimu sana paka hawa. Magoya saba ya mkia wa paka huyu ukiyachoma na ubani na harufu ikimpata vilivyo huyo mtoto wa mfalme kwa hakika atapona.

 

Wale majini hawakujuwa kama Khalidi amewasikia. Basi baa da ya muda wakamtoa pale ndani ya kisima. Khalidi alipitiwa na usingizi na aliposhituka akajikuta kitandani kwake. Alipoamka asubuhi akachukuwa magoya saba ya mkia wa ule paka akisubii kuona kama aliuwa anaota au ilikuwani kweli. Siku ile ilienda salama sana na hakukuwa na tatizo lolote, na huku Jalidi akaamini amemuuwa Khalidi,

 

Siku ilofata akaona ugeni unaingia kwake ni mfalme na msafra wake wakija kwakwe ili amuombee dua binti yake aliyekuwa anaumwa kwa miezi sita hata bila ya kupoona. Hapo khalidi akajuwa kumbe haikuwa ndoto ila ni ukweli. Pale akamchukuwa mgonjwa yule na akachukuwa udi na kachanganya na mgoya yale na akaomba dua. Hata kabla ya kumaliza alisikia kishindo. Mgonjwa alianguka chini na kupoteza fahamu.

 

Watu wakaanza kumpepea na mflme alijuwa lamda binti yake amepatwa na jambo. Baada ya masaa kadha akazinduka na hakuhisi maumivu yeyote. Hii inamaanisha alipona kabisa ugonjwa wake. Basi mfalme kwa furaha akamwambia “kijana kwa furaha nilizo nazo sina kikubwa cha kukulipa lakini naomba umuoe binti yangu” Khalidi alikubaliana na mawazo hayo na akamuowa binti mfalme. Kwakuwa mfalme hakuwa na mtoto wa kiume basi alopofariki Khalidi akapewa ufalme na akawa anaongoza nchi.

 

Miaka 15 sasa imepita toka aonane na Jalidi. Siku moja aliiona tena sura ya Jalidi ikiwa getini kuja kuomba msaada kwani maisha yamemuwia magumu. Jalidi alishangazwa kumuona Khalidi kuwa ndiye mfalme wao. Bila ya kinyongo Khalidi akamaidia Halidi n kumpati a vyakula na nguo kwa wingi sana na kumpatia na usafiri wa kubebea mizigo kwenda na yayo kijiji ni.

 

Kijana alipomaliza kusimulia hadithi hii akmwambia jini “nii ndio ilivyokuwa kati ya wagomvi wawili hawa, hivyo nakuomba unifanyie huruma kama Khalidi alivyomuhurumia Jalidi pindi alipomtumbukiza shimoni. Lile jini likasema “kwa hakika khabari hii inasikitisha lakini haiewzi kulinganisha hasira nilizo nazo . kwa hakika binti niliyemuuwa nilitoka nae mabli sana. Basi pale pale jini likapiga mguu chini na upepo mkali ukanibeba. Niliachwa kuleleni cha mlima uliopo pembenu ya ufukwe. Jini lile likanambia “nitakuonea huruma, sitakuuwa lakini nitakigeuza nyani” basi akanimwagia maji yamoto na palepale nikaanza kutowa magoya na kuota mkia. Kucha na hatimaye nikawa nyani kamili.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1212


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

HADITHI YA WAZIRI ALIYE ADHIBIWA
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA WAZIRI ALIYEADHIBIWA. Soma Zaidi...

USULUHISHWAJI KWA WALODHULUMIWA
Download kitabu Hiki Bofya hapa USULUHISHAJI WA WALODHULUMIWA. Soma Zaidi...

alif lela u lela
Download kitabu Hiki Bofya hapa Kupata mwendelezo wa hadithi hii Download App yetu. Soma Zaidi...

SAFARI YA SITA YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA SITA YA SINBAD. Soma Zaidi...

Kisiwa cha uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

SAFARI YA TANO YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA TANO YA SINBAD Baada ya watu kukusanyika siku ilofata sinbad akaanza kusimulia stori ya safari yake ya tano. Soma Zaidi...

Safari ya tano ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

BINTI WA NDOTONI
Download kitabu Hiki Bofya hapa BINTI WA NDOTONI. Soma Zaidi...

SAFARI YA KWANZA YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA KWANZA YA SINBAD Tambua kuwa baba yangu alikuwa ni mfanya biashara mkubwa sana katika nchi ya baghdad wakati wa utawala wa sultan harun Rashid. Soma Zaidi...

Hadithi ya mwenye kutabiriwa mtoto wa tajiri
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

MWANZO WA USALITI
Download kitabu Hiki Bofya hapa USALITI UNANZA HAPA Baada ya kukaa pale siku moja nahodha akaamrisha chombo kiondoke pale na kurudi nyumbani. Soma Zaidi...

Usuluhishaji wa walio dhurumiwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...