Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja

Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu.

Hekima ya Ukewenza

Kuna sababu nyingi za kibinafsi, kimaadili, kiuchumi na kijamii zinazoonesha kuwa wakati mwingine, kuoa mke zaidi ya mmoja ni jambo lisilobudi. Hebu turejee mifano ya hali kadhaa zifuatazo:

 


(a)Kama Mke ni Tasa
Mfikirie mwanamume ambaye amehakikisha kuwa mkewe ni tasa na bado anahamu ya kupata mtoto atakayekuwa mrithi wake. Katika hali hii mwanamume huyu atafanya mojawapo katika haya yafuatayo:
(i)Atakaa na kusononeka kwa kukosa mtoto katika maisha yake yote au
(ii)Atamuacha huyu mke asiye zaa iii aoe mwingine anayezaa au
(iii)Atatembea na wanawake wengine nje ya ndoa iii
wampatie watoto, japo kisheria si watoto wake au
(iv)Ataendelea kukaa na mkewe kwa mapenzi na furaha, kisha aoe mke mwingine atakayemzalia watoto ambao watakuwa wake kisheria.
Utakuta, uchaguzi wa kuoa mke wa pili, ndio ulio bora kabisa. Wengi katika jamii ya Kiislamu, wameoa mke wa pili kwa sababu hii:

 


(b)Kama Mke ana maradhi ya kudumu
Mfikirie tena mwanamume ambaye mkewe ana ugonjwa wa kudumu kwa kiasi kwamba hana uwezo wa kutekeleza majukumu yake kama mke. Bila shaka mwanamume huyu atafanya mojawapo katika haya yafuatayo:
(i)Atajizuia na matamanio yake ya kimwili kwa muda wote wa maisha yake uliobakia.
(ii)Anaweza kumtaliki mkewe mgonjwa wakati ambapo anahitajia uangalizi, huruma na mapenzi ya hali ya juu kutoka kwake, iii aoe mke mwingine atakaye tosheleza mahitaji yake, au.
(iii)Anaweza kubakia na mkewe mgonjwa na kufanya uzinifu kwa sin na wanawake wengi nje ya ndoa, au.
(iv)Ataoa mke wa pili atakayemsaidia kumuhudumia mkewe mgonjwa.

 


Hebu tuzijadili hizi hatua tatu za mwanzo kwa mtazamo wa mafundisho ya Uislamu.
Hatua ya kwanza inakwenda kinyume na umbile Ia mwanaadamu. Mwenyezi Mungu (s.w) analifahamu fika umbile Ia mwanaadamu na haja yake ya kutosheleza matamanio ya jimai na ameweka utaratibu mzuri wa sheria ya ndoa wa kutosheleza mahitajio haya ya kimaumbile.

 


Hatua ya pili ni kinyume kabisa ha ubinaadamu. Kumwacha mke kwa sababu amekuwa mgonjwa, badala ya kumuhudumia kwa upendo na huruma, ni kinyume kabisa na utu.
Hatua ya tatu ni haramu na ni uchafu katika Uislamu.

 


Utaona kuwa hatua ambayo itamuwezesha mume huyu aendelee kumtunza mkewe kwa huruma na wakati huo huo aweze kutosheleza mahitajio yake ya kimaumbile kwa utaratibu mzuri wa heshima na ucha-Mungu ni kuoa mke wa pili.

 


(c)Wanawake Wajane:
Wajane ni wanawake waliofiwa na waume zao au waliotalakiwa. Hakuna jamii isiyo na wajane, na idadi yao huongezeka zaidi nyakati za vita ambapo wanaume wengi huuliwa vitani. Je, wanawake hawa warudishwe kwa wazazi au walezi wao na kukaa hivyo hivyo bila ya kukidhi matashi yao ya kimaumbile mpaka wazeeke? Au waachwe wawe Malaya na kuitokomeza jamii kutokana na matatizo mbali mbali yanayosababishwa na zinaa? Kwa vyovyote vile utaona kuwa njia pekee ya kuwahifadhi wanawake wajane na watoto wao ni hii ruhusa ya kuoa mke zaidi ya mmoja hadi wane - kwa kufuata masharti yaliyowekwa.

 


(d)Wanawake wakiwa wengi katika Jamii:
Inatokea katika jamii nyingi wanawake kuwa wengi zaidi kuliko wanaume. Katika jamii hizi, kama tutaweka sheria ya mume mmoja - mke mmoja, kama wanavyodai watetezi wa usawa wa mwanamke, wanawake watakao kosa wanaume wa kuwaoa watakwenda wapi? Watafanyaje ili kukidhi matashi yao ya kimaumbile? Je, kama watajizuilia mpaka wazeeke huoni hii itawaathiri kimwili, na kisaikologia na kuwafanya wasiwe watu wenye manufaa katika jamii? Nani atakayetoa hifadhi kwa wanawake hawa kiuchumi na kimaadili? llivyo katika maumbile ya mwanaadamu, kila mwanamke wa kawaida anahitajia kuwa na mwanamume anayempenda na kumhurumia. Hivyo, wanawake hawa watakapowakosa wanaume wa ndoa, watafanya kila hila ya kuwashawishi wanaume kwa kuwawekea mitego mbali mbali kama vile kujipitisha mbele yao wakiwa wamejipodoa na kujiremba, kutembea mbele yao uchi, kuzurura kwenye majumba ya sinema, n.k., ambayo itawanasa na kuwatumbukiza katika zinaa.

 


Mfikirie mwanamke anayeishi kwa kuvizia wanaume. Je, atakuwa na utulivu na usalama katika maisha yake? Je, jamii yenye wanawake wa namna hii wa kuwavizia na kuwateka kwa tashiwishi waume za watu, inaweza kuwa jamii yenye amani na furaha? Wanawake wa namna hii mara nyingi wamekuwa ndio chanzo cha vurugu katika unyumba wa watu, kuwafitinisha watu na kusababisha vifo. Ikitokea mwanamke wa namna hii kupata mimba, jukumu Ia kumlea mtoto ni lake mwenyewe. Hivyo, watoto wanaozaliwa nje ya ndoa mara nyingi hukosa malezi mazuri na wengi wao huishia kuwa wezi wavuta bangi, na wahuni wa kupindukia katika jamii.

 


Kwa vyovyote vile iko haja kwa kila mwanamke kupata mume wa kukidhi haja zake na kuhifadhi maisha yake na utu wake. Uislamu umetoa ruhusa ya kuoa wake zaidi ya mmoja hadi wanne ili kumfanya kila mwanamke anayetaka kuolewa, aolewe na kupata hifadhi na haki zake zote zinazomstahiki.
Kwa nini mwanamke asiruhusiwe kuolewa na Mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja?

 


Wapinzani wa ukewenza, wanadai kuwa ili pawe na usawa, wanawake waruhusiwe kuolewa na mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja endapo wanaume wataruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja.

 


Kimaumbile na kisaikolojia, mwanamke ni wa mwanamume mmoja. llivyo, takriban katika jamii zote za ulimwenguni, mwanamume ndiye kiongozi wa familia. Fikiria ingalikuwaje kama familia moja ingalikuwa na viongozi wawili au zaidi!

 

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/16/Tuesday - 12:01:12 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 776

Post zifazofanana:-

Taratibu za kuchaguwa mchumba katika uislamu
Hapa utajifunza hatuwa kwa hatuwa za kuchaguwa mchumba kulingana na sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii
Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake? Soma Zaidi...

Taratibu za mahari katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu. Soma Zaidi...

Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu
Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha Soma Zaidi...

Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja. Soma Zaidi...

Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu
Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa. Soma Zaidi...

Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako. Soma Zaidi...

Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja
Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

Kugungisha ndoa ya kiislamu hatuwa kwa hatuwa
Hapa utajifunza jinsi ya kuozesha hatuwa kwa hatuwa. Pia utajifunza masharti ya kuoa na masharti ya kuolewa. Soma Zaidi...

Nini maana ya ndoa katia uislamu na ni upi umuhimu wake
Hapa utajifunza maana ya ndoa kulingana na uislamu na umuhimu wake katika jamiii Soma Zaidi...

Sifa nyingine za kuchaguwa mchumba ambazo watu wengi hawazijui
Hizi ni sifa za ziada za mchumba katika uislamu. Sifa hizi wengi hawazijui ama hawazingatii. Soma Zaidi...

Faida na umuhimu wa nfoa katika jamii
Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi Soma Zaidi...