image

Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja

Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu.

Hekima ya Ukewenza

Kuna sababu nyingi za kibinafsi, kimaadili, kiuchumi na kijamii zinazoonesha kuwa wakati mwingine, kuoa mke zaidi ya mmoja ni jambo lisilobudi. Hebu turejee mifano ya hali kadhaa zifuatazo:

 


(a)Kama Mke ni Tasa
Mfikirie mwanamume ambaye amehakikisha kuwa mkewe ni tasa na bado anahamu ya kupata mtoto atakayekuwa mrithi wake. Katika hali hii mwanamume huyu atafanya mojawapo katika haya yafuatayo:
(i)Atakaa na kusononeka kwa kukosa mtoto katika maisha yake yote au
(ii)Atamuacha huyu mke asiye zaa iii aoe mwingine anayezaa au
(iii)Atatembea na wanawake wengine nje ya ndoa iii
wampatie watoto, japo kisheria si watoto wake au
(iv)Ataendelea kukaa na mkewe kwa mapenzi na furaha, kisha aoe mke mwingine atakayemzalia watoto ambao watakuwa wake kisheria.
Utakuta, uchaguzi wa kuoa mke wa pili, ndio ulio bora kabisa. Wengi katika jamii ya Kiislamu, wameoa mke wa pili kwa sababu hii:

 


(b)Kama Mke ana maradhi ya kudumu
Mfikirie tena mwanamume ambaye mkewe ana ugonjwa wa kudumu kwa kiasi kwamba hana uwezo wa kutekeleza majukumu yake kama mke. Bila shaka mwanamume huyu atafanya mojawapo katika haya yafuatayo:
(i)Atajizuia na matamanio yake ya kimwili kwa muda wote wa maisha yake uliobakia.
(ii)Anaweza kumtaliki mkewe mgonjwa wakati ambapo anahitajia uangalizi, huruma na mapenzi ya hali ya juu kutoka kwake, iii aoe mke mwingine atakaye tosheleza mahitaji yake, au.
(iii)Anaweza kubakia na mkewe mgonjwa na kufanya uzinifu kwa sin na wanawake wengi nje ya ndoa, au.
(iv)Ataoa mke wa pili atakayemsaidia kumuhudumia mkewe mgonjwa.

 


Hebu tuzijadili hizi hatua tatu za mwanzo kwa mtazamo wa mafundisho ya Uislamu.
Hatua ya kwanza inakwenda kinyume na umbile Ia mwanaadamu. Mwenyezi Mungu (s.w) analifahamu fika umbile Ia mwanaadamu na haja yake ya kutosheleza matamanio ya jimai na ameweka utaratibu mzuri wa sheria ya ndoa wa kutosheleza mahitajio haya ya kimaumbile.

 


Hatua ya pili ni kinyume kabisa ha ubinaadamu. Kumwacha mke kwa sababu amekuwa mgonjwa, badala ya kumuhudumia kwa upendo na huruma, ni kinyume kabisa na utu.
Hatua ya tatu ni haramu na ni uchafu katika Uislamu.

 


Utaona kuwa hatua ambayo itamuwezesha mume huyu aendelee kumtunza mkewe kwa huruma na wakati huo huo aweze kutosheleza mahitajio yake ya kimaumbile kwa utaratibu mzuri wa heshima na ucha-Mungu ni kuoa mke wa pili.

 


(c)Wanawake Wajane:
Wajane ni wanawake waliofiwa na waume zao au waliotalakiwa. Hakuna jamii isiyo na wajane, na idadi yao huongezeka zaidi nyakati za vita ambapo wanaume wengi huuliwa vitani. Je, wanawake hawa warudishwe kwa wazazi au walezi wao na kukaa hivyo hivyo bila ya kukidhi matashi yao ya kimaumbile mpaka wazeeke? Au waachwe wawe Malaya na kuitokomeza jamii kutokana na matatizo mbali mbali yanayosababishwa na zinaa? Kwa vyovyote vile utaona kuwa njia pekee ya kuwahifadhi wanawake wajane na watoto wao ni hii ruhusa ya kuoa mke zaidi ya mmoja hadi wane - kwa kufuata masharti yaliyowekwa.

 


(d)Wanawake wakiwa wengi katika Jamii:
Inatokea katika jamii nyingi wanawake kuwa wengi zaidi kuliko wanaume. Katika jamii hizi, kama tutaweka sheria ya mume mmoja - mke mmoja, kama wanavyodai watetezi wa usawa wa mwanamke, wanawake watakao kosa wanaume wa kuwaoa watakwenda wapi? Watafanyaje ili kukidhi matashi yao ya kimaumbile? Je, kama watajizuilia mpaka wazeeke huoni hii itawaathiri kimwili, na kisaikologia na kuwafanya wasiwe watu wenye manufaa katika jamii? Nani atakayetoa hifadhi kwa wanawake hawa kiuchumi na kimaadili? llivyo katika maumbile ya mwanaadamu, kila mwanamke wa kawaida anahitajia kuwa na mwanamume anayempenda na kumhurumia. Hivyo, wanawake hawa watakapowakosa wanaume wa ndoa, watafanya kila hila ya kuwashawishi wanaume kwa kuwawekea mitego mbali mbali kama vile kujipitisha mbele yao wakiwa wamejipodoa na kujiremba, kutembea mbele yao uchi, kuzurura kwenye majumba ya sinema, n.k., ambayo itawanasa na kuwatumbukiza katika zinaa.

 


Mfikirie mwanamke anayeishi kwa kuvizia wanaume. Je, atakuwa na utulivu na usalama katika maisha yake? Je, jamii yenye wanawake wa namna hii wa kuwavizia na kuwateka kwa tashiwishi waume za watu, inaweza kuwa jamii yenye amani na furaha? Wanawake wa namna hii mara nyingi wamekuwa ndio chanzo cha vurugu katika unyumba wa watu, kuwafitinisha watu na kusababisha vifo. Ikitokea mwanamke wa namna hii kupata mimba, jukumu Ia kumlea mtoto ni lake mwenyewe. Hivyo, watoto wanaozaliwa nje ya ndoa mara nyingi hukosa malezi mazuri na wengi wao huishia kuwa wezi wavuta bangi, na wahuni wa kupindukia katika jamii.

 


Kwa vyovyote vile iko haja kwa kila mwanamke kupata mume wa kukidhi haja zake na kuhifadhi maisha yake na utu wake. Uislamu umetoa ruhusa ya kuoa wake zaidi ya mmoja hadi wanne ili kumfanya kila mwanamke anayetaka kuolewa, aolewe na kupata hifadhi na haki zake zote zinazomstahiki.
Kwa nini mwanamke asiruhusiwe kuolewa na Mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja?

 


Wapinzani wa ukewenza, wanadai kuwa ili pawe na usawa, wanawake waruhusiwe kuolewa na mume zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja endapo wanaume wataruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja.

 


Kimaumbile na kisaikolojia, mwanamke ni wa mwanamume mmoja. llivyo, takriban katika jamii zote za ulimwenguni, mwanamume ndiye kiongozi wa familia. Fikiria ingalikuwaje kama familia moja ingalikuwa na viongozi wawili au zaidi!

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 943


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?
Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga? Soma Zaidi...

Nadharia ya uchumi wa kiislamu
Dhana ya uchumi wa kiislamu imejegwa jui ya ukati na kati. Dhana hii imetofautiana sana na dhana nyinginezo kama ubepari na ujamaa. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUSWALI
13. Soma Zaidi...

Kutoa vilivyo vizuri
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ni nini maana ya uchumi katika uislamu
Katikabuislamu dhana ya uchumi imetofautiana na dhana ya kidunia hivi leo ambapo kamari na riba ni moja ya vitu muhimu katika uchumi. Soma Zaidi...

Namna lengo la zakat linavyofikiwa
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda
Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi Soma Zaidi...

Wanaowajibika kuhijji
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nguzo za kufunga ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani
Utangulizi:Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii. Soma Zaidi...

Kusimamisha swala za faradh katika nyakati za dharura.
Kipengele hichi tutajifunza namna ya kusimamisha swala ukiwa safarini na vitani na nguzo zake. Soma Zaidi...

Haki ya kumiliki mali na mipaka yake katika uislamu
Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo Soma Zaidi...