image

Kwanini lengo la funga halifikiwi na wafungaji wengi

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji wengi?
Pamoja na waislamu wengi kujizatiti katika kufunga mwezi wa Ramadhani na funga zingine za sunnah, lakini wengi wao hafikii lengo la funga kwa sababu zifuatazo;
Wengi wafungao hawajui lengo la funga.
Wafungaji wengi hufunga kwa lengo la kupata thawabu na kufutiwa madhambi tu na sio kuwa wacha-Mungu kama lilivyo lengo la funga.
Rejea Quran (2:183).

Wafungaji wengi chumo lao ni la haramu.
Waislamu wengi wafungao chakula chao, futari yao na daku zao zinatokana na chumo la haramu ambalo ni sababu ya kutopata matunda ya funga zao.

Kutofahamika lengo la maisha na uhusiano na lengo la funga.
Waislamu wengi hutekeleza ibada maalumu kama swala, funga, n.k na kuona kuwa ndio lengo kuu la maisha yao na kuacha nyanja zingine za maisha yao.
Rejea Quran (51:56).

Wengi wafungao hawazingatii miiko na sharti za funga zao.
Waislamu wengi wafungao huishia kushinda njaa na kiu bila kupata faida ya funga zao kwa kutojizuilia na mambo maovu, machafu, laghawi, upuuzi, n.k. 

Wengi wafungao hawatekelezi nguzo na sunnah za funga ipasavyo.
Pamoja na waislamu wengi kufunga, lakini wengi wao hawaswali kabisa swala za faradh na sunnah na kubakia kufuata mkumbo kwa kushinda na njaa.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1926


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Funga ya ramadhan na nyinginezo
Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuandama kwa Mwezi na Kufunga ama kufungua ramadhani, sheria na hukumu za kuangalia mwezi
Soma Zaidi...

Haki za mwanamke katika uislamu
Soma Zaidi...

Zoezi la nne mada ya fiqh.
Maswali mbalimbali kuhusu fiqh. Soma Zaidi...

Kutoa vilivyo halali
Nguzo za uislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hukumu za talaka na eda
Soma Zaidi...

Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)
Soma Zaidi...

Yaliyoharamishwa kwa mwenye kuwa katika ihram
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Swala ya tarawehe jinsi ya kuiswali
Post hii itakwenda kukufundisha kuhusi swala ya tarawehe, faida zake na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Soma Zaidi...

Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala. Soma Zaidi...

Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu
- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n. Soma Zaidi...