picha

Kwanini wengi wanaohijji hawafikii lengo la hijjah zao

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)


Kwa nini wengi wanaohiji hawafikii lengo la Hijah zao?
Pamoja na mkusanyiko wa mamilioni wa mahujaj katika Mji wa Makka kila mwaka lakini matunda ya Hija hayafikiwi. Zifuatazo ni baadhi ya sababu;

Kuhiji kwa chumo la haramu.
Waislamu wengu hufunga safari ya kwenda hija kwa fedha za pato la haramu ambazo ni kikwazo cha kupata matunda ya hija zao.

Kutochunga miiko, nguzo na sharti za Hijah.
Pamoja na kufunga safari ya Hijah au Umrah, mahujaj wengi hawachungi miiko, nguzo na masharti ya Hijah au Umrah ipasavyo.
Rejea Quran (2:197).

Kutokuwa na elimu na ujuzi sahihi juu ya ibada ya Hijah.
Mahujaji wengi hufunga safari ya kwenda Hija au Umrah ili hali hawana ujuzi wowote wa ibada watakazozitekeleza ila kufuata mkumbo tu.

Kutojulikana kwa lengo halisi la Hijah au Umrah.
Waislamu wengi hufunga safari ya Hijah au Umrah kwa lengo la kupata thawabu na kufutiwa madhambi tu na sio kuwa askari wa kupigania dini.
Rejea Quran (51:56).

Kufunga safari ya Hijah kwa Malengo mengine.
Waislamu wengi hufunga safari kwa ajili ya biashara, utalii au kutafuta umaarufu wa kujiita majina ya Al-Hajj ambayo ni nje na lengo la Hijah.  

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/18/Tuesday - 07:24:49 pm Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3629

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 web hosting    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?

Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh.

Soma Zaidi...
Taratibu za kutaliki katika uislamu.

Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu

- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.

Soma Zaidi...
Lengo la hijjah na matendo ya ibada ya hijjah na mafunzo yatokanayo

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kwanini lengo la funga halifikiwi na wafungaji wengi

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Taratibi za malezi ya watoto wadogo baada ya talaka katika uislamu

Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?

Soma Zaidi...
Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu

Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.

Soma Zaidi...