Lengo la hijjah na matendo ya ibada ya hijjah na mafunzo yatokanayo

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

 

Lengo la Hijjah.

Kuwa askari Mcha-Mungu aliyekuwa tayari kutumia mali na nafsi yake katika kuipigania Dini ya Mwenyezi Mungu (s.w) kutawala maisha ya jamii.

Rejea Quran (48:18) na (3:96-97).

 

 

Matendo ya ibada ya Hijjah na Mafunzo yatokanayo.

Kabla na wakati wa kutekeleza ibada ya Hijjah, kuna mafunzo na hatua za kuzingatia kama ifuatavyo;

 

Maandalizi na Safari ya Hijjah.

Ni lazima muislamu kabla ya kwenda Hijjah afanye maandalizi ikiwa ni pamoja na kuzidisha ucha-Mungu, kuandaa gharama, mahitaji, n.k.

Rejea Quran (2:197)

 

Ihram.

Ni hali ya kuwa katika vazi rasmi na miiko kwa mwanaume mwenye Kuhiji au kufanya Umrah.

Funzo (49:13):

-  Vazi la Ihram linatufunza usawa baina ya wanaadamu wote.

 

Talbiya.

Ni kuitikia wito wa Mwenyezi Mungu (s.w) kwa kusema yafuatayo, “Labbayka Allahumma Labbayka. Labbayka laashariika laka labbayka. Innal-hamda Wanniimata laka wal-mulka, laashariika laka

 

Mafunzo (22:27) na (48:18):

Talbiya inatufunza kumuitikia Mwenyezi Mungu (s.w) kufuata maamrisho na kuacha makatazo yake.

-     Talbiya inatufunza umoja na usawa baina ya waislamu wote.

 

Tawaf.

Ni kitendo cha kuizunguka Kaaba mara saba kuanzia jiwe jeusi kwa mwelekeo wa kinyume na saa kwa kulibusu au kuligusa au kuashiria.

 

Mafunzo:

Kuchukua ahadi ya utii kwa Mwenyezi Mungu (s.w).

Kumtaja na kumtukuza Mwenyezi Mungu (s.w) kwa wingi.

Inatufunza umoja, udugu na usawa baina ya wanaadamu wote.

 

Sai.

Ni kitendo cha kutembea mara saba baina vilima viwili, Saffaa na Marwaa, kwa kuanzia Saffaa na kumalizia Marwaa.

 

Mafunzo:

Inatufunza utii kwa Mwenyezi Mungu (s.w).

Inatufunza ushujaa na uhodari katika kupigania Uislamu.

Inatufunza kuwa tayari kuhangaika kwa ajili ya kupigania Uislam

 

Kupiga Kambi Mina, Mwezi 8 Dhul-Hijah.

Ni kitongoji kilichopo baina ya Mji wa Makkah na bonde la Arafah. Mahujaji hulala hapo na kuondoka kesho yake kuelekea Arafa asubuhi.

 

Mafunzo:

Huwafunza mahujaji kuwa askari waliotayari kuacha kila chaokwa ajili ya kupigania Uislamu.

Huwafunza mahujaji kuwa askari wanatiifu kwa Muumba wao.

 

Kusimama Arafah, Mwezi 9 Dhul-Hija.

Arafa ni bonde lililo baina ya vilima vitatu. Mahujaji husimama humo tangu Swala ya Adhuhuri hadi Magharibi na kuomba dua mbali mbali. 

 

Mafunzo:

Huwakumbusha mahujaji mkutano mkuu wa siku ya Kiama.

Hutufunza kuwa hakuna aliyebora ila amchae Mungu zaidi.

Kisimamo cha Arafa kinatufunza usawa baina ya wanaadamu.

 

Kupiga Kambi Mzidalfah.

Mzidalfa ni kitongoji kilicho baina ya Mina na Arafa. Mahujaji huswali Magharib na Isha hapo na kuelekea Mina mara tu baada ya swala Alfajir.

 

Mafunzo:

Huwafunza mahujaj kuwa askari waliojiandaa kupambana na maadui wa Mwenyezi Mungu (s.w).

Kuomba dua hutufunza kuwa ushindi ni kwa nusura ya Mungu tu.

 

Kutupa Mawe Mina katika Minara Mitatu, Mwezi 10, Dhul-Hija.

Ni kitendo kinachofanyika kuanzia Mwezi 10-13, Dhul-Hija kwa kutupa vijiwe saba kila Mnara.

 

Mafunzo:

-   Zoezi hili huwafunza mahujaj ujasiri wa kupambana na maadui zao.

-   Huwafunza mahujaj pia mbinu na silaha katika kupigana na maadui.

 

Kuchinja mnyama Mwezi 10, Dhul-Hija.

Katika siku hii Hajj atanyo nywele, kuchinja mnyama, kutupa mawe kwenye Minara mitatu na kutufu Tawaful-Ifaadha (tawafu ya nguzo).

 

Mafunzo:

-   Zoezi hili linawafunza mahujaj utiifu kwa Mwenyezi Mungu (s.w).

-   Tunajifunza kuwa tayari kuua au kuuawa kwa ajili ya Mungu.

-   Inatufunza kuwa na subira na kujitoa muhanga katika kunusuru dini

Rejea Quran (22:37) na (37:111).

 

Siku za Tashriiq Mwezi 11-13, Dhul-Hija.

Ni kilele cha ibada ya Hija, ambapo mahujaj hupumzika kambini na kutathmini vitendo vyote walivyovifanya.

 

Mafunzo:

-   Huwafunza mahujaj kumkumbuka Mungu baada ya kazi ngumu.

-   Huwafunza askari kuwa na mazingatio na yale waliojifunza kwayo.

 

Tawaf ya Kuaga (Tawaful-Widaa).

Ni Tawafu ya kuaga baada ya ibada ya Hija kukamilika na kujiandaa kurejea nyumbani kwa mahujaji.

 

 

Mafunzo:

Huwafunza mahujaj kuwa viongozi (makhalifa) katika ardhi.

Kuwa askari waliochukua mafunzo tayari kwa kuyatekeleza.

Kuchukua ahadi ya utiifu kwa Mwenyezi Mungu (s.w).



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/01/18/Tuesday - 07:22:01 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2101


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maswali juu ya Sunnah na hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu
Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu. Soma Zaidi...

Kutoa zakat
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Tafsiri na mafunzo ya sura zilizochaguliwa - Saratul-fiyl
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mapema, kwa sababu ya kuwepo kwa saratani ya matiti, kuna dalili ambazo zikijitokeza zinapaswa kutolewa taarifa mara moja bila kuchelewa kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Nguzo za kufunga ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat
Nguzo za uislamu, masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya sadaqat
Nguzo za imani, maana ya sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na nini? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo) Soma Zaidi...

Haki za binadamu kwa ujumla (basic human rights)
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...