picha

Maana ya kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

 

4.2. Maana ya Kusimamisha Swala.

Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo, sharti zote za swala na kuwa na unyenyekevu (khushui) ndani ya swala. 

 

Nafasi na Umuhimu wa Kusimamisha Swala katika Uislamu.

Swala imesisitizwa na ina umuhimu katika Uislamu kwa sababu zifuatazo;

 

Kusimamisha Swala ni Amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Mwenyezi Mungu (s.w) ameamrisha waumini (waislamu) wote wasimamishe swala zote za faradh na sunnah ipasavyo.

Rejea Quran (29:45), (4:103) na (14:31).

 

Kusimamisha swala ni nguzo ya Pili ya Uislamu.

Baada ya shahada mbili, nguzo ya pili na ya msingi mno katika Uislamu ni kusimamisha swala.

 

Swala humtakasa muislamu na mambo machafu na maovu.

Bila shaka swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mja na mambo machafu na maovu.

Rejea Quran (29:45).

 

Swala ni amali ya mwanzo kabisa kuhesabiwa siku ya Qiyama.

Swala ya muumini ikitengemaa vizuri ndio sababu ya kufaulu kwake Duniani na Akhera pia.

Rejea Quran (23:1-2,9), (87:14-15) na (22:34-35).

 

Kutosimamisha swala ni sababu ya mtu kuingizwa motoni.

Hii ni baada ya muislamu Kupuuza swala kwa kutozingatia sharti na nguzo zake kikamilifu na kukosa unyenyekevu (khushui) ndani ya swala.

Rejea Quran (74:42-47), (68:42-43) na (107:4-5).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/18/Tuesday - 01:25:14 pm Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3366

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 web hosting    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu

Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala vitani

Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani.

Soma Zaidi...
Maana ya zakat

Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Wanaostahiki kupewa sadaqat

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
Mambo yanayobatilisha funga au yanayoharibu swaumu.

Hapa utajifunza mambo ambayo akiyafanya mtu aliyefunga, basi funga yake itaharibika.

Soma Zaidi...
Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.

Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.

Soma Zaidi...