Maana ya kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

 

4.2. Maana ya Kusimamisha Swala.

Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo, sharti zote za swala na kuwa na unyenyekevu (khushui) ndani ya swala. 

 

Nafasi na Umuhimu wa Kusimamisha Swala katika Uislamu.

Swala imesisitizwa na ina umuhimu katika Uislamu kwa sababu zifuatazo;

 

Kusimamisha Swala ni Amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Mwenyezi Mungu (s.w) ameamrisha waumini (waislamu) wote wasimamishe swala zote za faradh na sunnah ipasavyo.

Rejea Quran (29:45), (4:103) na (14:31).

 

Kusimamisha swala ni nguzo ya Pili ya Uislamu.

Baada ya shahada mbili, nguzo ya pili na ya msingi mno katika Uislamu ni kusimamisha swala.

 

Swala humtakasa muislamu na mambo machafu na maovu.

Bila shaka swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mja na mambo machafu na maovu.

Rejea Quran (29:45).

 

Swala ni amali ya mwanzo kabisa kuhesabiwa siku ya Qiyama.

Swala ya muumini ikitengemaa vizuri ndio sababu ya kufaulu kwake Duniani na Akhera pia.

Rejea Quran (23:1-2,9), (87:14-15) na (22:34-35).

 

Kutosimamisha swala ni sababu ya mtu kuingizwa motoni.

Hii ni baada ya muislamu Kupuuza swala kwa kutozingatia sharti na nguzo zake kikamilifu na kukosa unyenyekevu (khushui) ndani ya swala.

Rejea Quran (74:42-47), (68:42-43) na (107:4-5).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2821

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Swala ya witiri na faida zake, na jinsi ya kuiswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali.

Soma Zaidi...
Zijuwe aina kuu 6 za talaka katika uislamu

Talaka zimegawanyika katika makundi mengi. Katika somo hili utakwenda kukifunza aina kuu za talaka katika uislamu.

Soma Zaidi...
Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?

Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh.

Soma Zaidi...
Swala ya tahiyatul masjidi yaani maamkizi ya msikitini, pamoja na swala za qabliya na baadiya

Post hii inakwenda kukujuza kuhusu swala za qabliya, baadiya na tahiyatul masjid.

Soma Zaidi...
Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu

Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli.

Soma Zaidi...
Hizi ndio nyakati za swala tano na jinsi ya kuchunga nyakati za swala.

Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkuchunga nyakatibza swala tano.

Soma Zaidi...
Jinsi Uislamu Ulivyokomesha Biashara ya Utumwa wakati na baada ya Mtume Muhammad (s.a.w)

- Uislamu ulieneza nadharia kuwa wanaadamu wote ni sawa na wote ni watumwa mbele ya Mwenyezi Mungu (s.

Soma Zaidi...