Maandalizi ya mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia.
Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.
Yafuatayo Ni maandalizi ya Mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia;
1.kuwepo na usafiri ; mama anapo hudhurua clinic hufundishwa dalili za Hatari hivyo ujauzito sio kitu Cha kushtukiza hvyo unatakiwa kujipanga ili kutafuta usafiri mapema .
2.mtu atakayebaki nyumba; husaidia kulinda nyumba na familia iliyobaki pia na kuangalia usalama wa hapo nyumbani.
3.mtu wa kumsindikiza; mama anapoenda kujifungua awe na msaidizi kwa ajili ya kuenda kumsaidia na msindikizaji huyu awe anajiweza ili aweze kumsaidia mama pale atakapohitajika msaada wake.
4. Vifaa vya kujifungulia; Kawaida mama akiwa anahudhuria cliniki hupewa mwongozo wa kila kitu hivyo anatakiwa awe na vifaa kwa ajili ya kujifungulia ,na vifaa hivyo Ni Kama vile
1. karatasi aina ya nailoni kwaajili ya kutandikia kitanda anachojifungulia mama ili kuepusha kuchafua mazingira.
2. mipira ya Kuvaa mikononi (gloves) hizi hutumika wahudumu wanapokua wanamuhudumia mama akiwa anajifungua.
3. Kiwembe Cha Upasuaji hutumika kukatia kitovu kilichounganisha Mtoto na kondo la nyuma ili kutenganisha pia kukatia nyuzi wakati mama anaposhonwa Kama akiwa amechanika.
4. kibanio Cha kitovu (clamp) hutumika kubania kitovu kikitenganishwa ili kisitoe Damu.
-5. vitenge au khanga ; ambazo hutumika kumfunikia mtoto,kutandikia kwenye nailoni,mama kujifungua na nguo hizi zisiwe mpya ziwe Ni khanga zilizotumika.
6. malapa ambayo atavaa mam anapotaka kwenda kuoga,kufanya mazoezi maana hawezi kutembea bila kitu mguuni.
7. beseni (dishi) au ndoo ndogo hutumika kuwekea ndoo chafu pia kiafa hiki hutumika mama kunisaidia wakati anakaribia kujifungua maana hauruhusiwi kwenda chooni.
8. sabuni na mafuta ya mama
9. Pamba kubwa na nyuzi za upasuaji
10. pedi kubwa za mama ambapo akijifungua anaweza kuitumia Ila so lazima maana mama anaweza kuitumia khanga.
11. vifaa vya Mtoto Kama vile soksi, bebshoo,pampasi,kofia,mafuta ya Nazi ili vimpatie Mtoto joto pia na leso laini kwaajili ya kumfutia Mtoto.
5.fedha; mama na familia kiujumla wanatakiwa kujipanga kwa matumizi ya hela pale zitakapohitajika wawe nazo.
Mwisho; mama mjamzito anapohudhuria kliniki hupewa mwongozo wote na swala la ujauzito sio la kushtukiza Ni kitu ambacho kipo wazi hivi mama au familia unatakiwa kujipanga na maandalizi.
Mwisho; mama mjamzito anapojigundua tu kuwa ana mimba anatakiwa awahi cliniki kwaajili ya kupewa eleimu juu ya kujikinga,Mambo Hatari kujua na vifaa na Mambo mengine mengi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 web hosting 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?
Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa yanaweza kuwa ni dalili ya maradhi fulani, ama shida kwenye mfumo w uzazi. PID na UTI hutuhumiwa kuwa ni katika sababu hizo. Ila zipo nyingine nyingi tu. Kama ina hali hii vyema ukafika kituo cha afya
Soma Zaidi...Je bado unasumbuliwa na nguvu za kiume?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuondoa tatizo la nguvu za kiume
Soma Zaidi...Sababu za kutoona hedhi kwa wakati
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.
Soma Zaidi...Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.
Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h
Soma Zaidi...Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?
Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?
Soma Zaidi...Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi
Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi.
Soma Zaidi...