Mabadiliko ya Matiti kwa Mama mjamzito
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye Matiti kwa Mama mjamzito, hali hii utokea pale ambapo mama akibeba mimba Kuna mabadiliko kwenye Matiti kama ifuayavyo.
Mabadiliko yanayotokea kwenye Matiti kwa Mama mjamzito.
1. Kiwango Cha damu kusafiri kwenye Matiti uongezeka, Ili kuweza kuanzisha kuzalisha kwa Maziwa kiasi Cha kuongezeka kwa kiwango Cha damu kwenye Matiti usaidiwa na homoni mbili ambazo ni progesterone na oestrogen hii ni kwa sababu ya kuandaliwa kwa kutengenezwa kwa Maziwa.
2. Katika wiki ya tatu mpaka ya nne Kuna miwasho fulani inayotokea kwenye sehemu za Matiti hii ni kwa sababu ya kuongeza kwa kiwango Cha damu kwenye Matiti, na wiki ya sita mpaka ya nane Kuna kuongezeka kwa ukubwa wa Matiti na maumivu kwenye Matiti uanza kujitokeza kwa sababu ya kuongeza kwa kiwango kwa Matiti na mishipa ya veini uanza kuonekana juu ya ngozi
3. Kuanzia wiki ya nane mpaka Kumi na mbili gland uanza kuzalisha sebum ambazo ufanya chuchu za Matiti kuwa na ulaini kwa ajili ya maandalizi ya kumnyonyesha mtoto, na kwa kipindi kingine chuchu uanza kuwa nyeusi kwa Sababu ya maandalizi ya kumnyonyesha mtoto.
4. Katika wiki za mwisho ambazo ni kuanzia wiki ya thelathini na nane na kuendelea majimaji ya njano uanza kujitokeza kwenye Matiti ambayo baadae mtoto akizaliwa ndiyo maziwa ambayo utumiwa na mtoto, kwa hiyo Iwapo Mama akiona maziwa kama haya hasiogope ajue kuwa ni kawaida kwa Maziwa ya Aina hii kutokea.
5. Matiti kuvimba kuliko kawaida
Kwa Mama mjamzito Matiti uongezeka kuliko kawaida kwa sababu ya matengenezo ya maziwa na kwa sababu ya kuongezeka kwa pressure kwenye Matiti, na pia kuongezeka kwa virutubisho kwenye Matiti kwa ajili ya mtoto.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 web hosting 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo chini ya umri wa miaka mitano ili kuweza kuweka afya yake kwenye njia safi.
Soma Zaidi...Mambo ya kuzingatia kwa mama ili apate huduma endelevu.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.
Soma Zaidi...Dalili za kifafa cha mimba.
Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Tatizo la kutanuka kwa tezi dume.
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutanuka kwa tezi dume, ni tatizo ambalo linawakumba wanaume wengi kwa wakati huu kwa sababu ya kuwepo kwa maaambukizi kwenye tezi ambayo Usababishwa na vitu mbalimbali kama tulivyoona.
Soma Zaidi...Kazi na mdalasini katika kutibu matatizo ya homoni.
Posti hii inahusu zaidi kazi ya mdalasini katika matibabu ya homoni kwa wanawake.
Soma Zaidi...Mwanamke anatema mate mara kwa mara je inaweza kuwa ni ujauzito?
Ni kweli kuwa kutema mate mara kwa mara inaweza kuwa ni dlili za ujauzito. Lakini itambulije kuwa pekee sio kithibitishi cha ujauzito.
Soma Zaidi...