picha

Madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu

Post hii inahusu Zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea Kwa mgonjwa mweye usaha kwenye mapafu.

Madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kazi ya mapafu ambayo ni kuruhusu hewa safi kuingia kwenye mwili na kuruhusu hewa chafu kutoka kwenye mwili na kwenda nje,Kwa kufanya hivyo,mtu anaweza kupata hewa safi na kutoa hewa chafu nje,Kwa kawaida mapafu yasipofanya kazi vizuri madhara mengi utokea Kwa mtu,hata mtu akija kukata roho kwenye dakikia zake za mwisho Huwa tunaangali hewa,kwa hiyo hewa ni kitu Cha muhimu sana ,Kwa hiyo mapafu yasipofanya kazi vizuri ni rahisi kupata matatizo Zaidi na madhara mengi kama hasa kama mapafu yakishambuliwa na kuwepo Kwa usaha tunapata matatizo yafuatayo kama vile.

 

 

 

2. Kusambaza Kwa maambukizi kwenye mfumo mzima wa upumuaji.

Kwa kawaida ili hewa iweze kutoka na kuingia Kuna mfumo ambao hewa upitia hatua Kwa hatua Kwa mfano kwenye trachea,bronch,bronchiole, alveoli, alveolar sacs,mapafu na sehemu mbalimbali,kwa hiyo basi kama sehemu ya kwenye mapafu imepata shida na kuwa na usaha lazima bakteria watasambaa sehemu nyingine za mfumo wa upumuaji na kuleta maambukizi,Kwa hiyo Kwa kuwa tumeshaona dalili, nja za kutumia kutambua kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu ni vizuri kabisa kutibu tatizo mapema ili kuepuka hali ya kusambaza kwenye mfumo mzima wa upumuaji na kuleta madhara makubwa Zaidi.

 

 

 

 

3. Vile Vila maambukizi yanaweza kusambambaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili kupitia kwenye mzunguko wa damu.

Kwa kawaida tunafahamu kwenye mwili wa binadamu ni Kama machine,mwili wabinadamu una mishipa ya artery, vein na mishipa midogo midogo, mishipa ya artery usabaza damu safi kwenye mwili kutoka kwenye moyo,mishipa ya veini utoa damu chafu kwenye mwili mpaka sehemu mbalimbali za mwili, Kwa hiyo basi na vile vile kwenye mapafu Kuna mishipa hiyo ya artery na vein naufanya kazi hiyo, ikitokea Kuna maambukizi kwenye mapafu na wadudu ubebwa kwenye mzunguko wa damu,mpaka sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye ubongo na kusababisha usaha sehemu hizo hizo nazo zinaweza kupata matatizo hayo hayo,Kwa hiyo wapendwa wasomaji matibabu ni lazima ili kuweza kuepuka madhara makubwa Zaidi.

 

 

 

 

4. Kuharibika Kwa mishipa inayopeleka na kutoa damu kwenye mapafu .

Kwa sababu ya kuwepo Kwa usahaa kwenye mapafu na pia pengine Kwa Sababu ya kuwepo Kwa maambukizi kwenye mapafu ambayo usababisha kuwepo Kwa damu usababisha kuharibika Kwa mishipa inayopeleka damu kwenye mapafu na kutoa damu kwenye mapafu, Kwa hiyo hali ya mgonjwa inawezekana kuwa mbaya Kwa sababu ya kukosa damu ya kutosha kwenye mapafu.na pengine hiyo mishipa inawezekana kushambulia na bakteria walipo Kwa sababu ya kukosa Kwa matibabu.

 

 

 

 

5. Upungufu wa hewa safi ambayo Kwa kitaalamu huitwa oxygen na kupngezeka Kwa hewa chafu kwenye mapafu ambayo Kwa kitaalamu huitwa carbon dioxide.

Kwa sababu ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu na kuharibika Kwa mishipa ambayo upeleka damu kwenye mapafu hali hii usababisha damu ya oxygen kupungua na kusababisha kuongezeka Kwa damu ya carbon dioxide kwenye mapafu hali ambayo usababisha maisha ya mgonjwa kuwa magumu, Zaidi Kwa hiyo matibabu ni lazima kabisa ili kuweza kuokoa maisha ya mgonjwa.

 

 

6. Baada ya kuona madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu kuwa ni mengi na matibabu yanahitajika Kwa mgonjwa ili kuweza kuokoa maisha ya mgonjwa na kujaribu kuelimisha jamii kuhusu kuwepo Kwa ugonjwa huu na kwamba unatibika na kujaribu kutoa Mila mbaya za kuwatenga wale walio na ugonjwa huu kwenye jamii.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1453

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰2 ai web app     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     ๐Ÿ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii     ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Fahamu Dalili zinazotokana na kuzama kwenye majj kwa watoto.

Kuzama hufafanuliwa kama mchakato unaosababisha upungufu mkubwa wa kupumua kutokana na kuzamishwa kwenye chombo cha kuogelea (kioevu). Kuzama hurejelea tukio ambalo njia ya hewa ya mtoto huzamishwa kwenye kioevu, na kusababisha kuharibika kwa kupumua.

Soma Zaidi...
Je kwa mfano mimi nmeupata ukimwi leo na sihitaji kwenda kupima yaaan uanza kujionyesha baada ya muda gani

Watu wengi wamekuwa wakijiuliza kuwa ukimwi huonekana baada ya muda gani toka kuathirika?

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa gonoria (gonorrhea)

UGONJWA WA GONORIA NA DALILI ZAKE (GONORRHEA)Gonoria (gonorrhea) ni katika maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

Soma Zaidi...
Ujue Ugonjwa wa homa ya ini yenye sumu.

Homa ya ini yenye sumuร‚ย ni kuvimba kwa ini lako kutokana na kuathiriwa na vitu fulani ambavyo umeathiriwa navyo. Homa ya ini yenye sumuร‚ย inaweza kusababishwa na pombe, kemikali, dawa za kulevya au viongeza vya lishe.

Soma Zaidi...
Aina za kifua kikuu.

Posti hii inahusu zaidi aina mbili za kifua kikuu, aina ya kwanza ni ile ya kawaida ambayo ushambulia mapafu na aina ya pili ni ile ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye limfu node, kwenye sehemu za moyo, kwenye uti wa mgongo, kwen

Soma Zaidi...