Madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu
Post hii inahusu Zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea Kwa mgonjwa mweye usaha kwenye mapafu.
Madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kazi ya mapafu ambayo ni kuruhusu hewa safi kuingia kwenye mwili na kuruhusu hewa chafu kutoka kwenye mwili na kwenda nje,Kwa kufanya hivyo,mtu anaweza kupata hewa safi na kutoa hewa chafu nje,Kwa kawaida mapafu yasipofanya kazi vizuri madhara mengi utokea Kwa mtu,hata mtu akija kukata roho kwenye dakikia zake za mwisho Huwa tunaangali hewa,kwa hiyo hewa ni kitu Cha muhimu sana ,Kwa hiyo mapafu yasipofanya kazi vizuri ni rahisi kupata matatizo Zaidi na madhara mengi kama hasa kama mapafu yakishambuliwa na kuwepo Kwa usaha tunapata matatizo yafuatayo kama vile.
2. Kusambaza Kwa maambukizi kwenye mfumo mzima wa upumuaji.
Kwa kawaida ili hewa iweze kutoka na kuingia Kuna mfumo ambao hewa upitia hatua Kwa hatua Kwa mfano kwenye trachea,bronch,bronchiole, alveoli, alveolar sacs,mapafu na sehemu mbalimbali,kwa hiyo basi kama sehemu ya kwenye mapafu imepata shida na kuwa na usaha lazima bakteria watasambaa sehemu nyingine za mfumo wa upumuaji na kuleta maambukizi,Kwa hiyo Kwa kuwa tumeshaona dalili, nja za kutumia kutambua kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu ni vizuri kabisa kutibu tatizo mapema ili kuepuka hali ya kusambaza kwenye mfumo mzima wa upumuaji na kuleta madhara makubwa Zaidi.
3. Vile Vila maambukizi yanaweza kusambambaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili kupitia kwenye mzunguko wa damu.
Kwa kawaida tunafahamu kwenye mwili wa binadamu ni Kama machine,mwili wabinadamu una mishipa ya artery, vein na mishipa midogo midogo, mishipa ya artery usabaza damu safi kwenye mwili kutoka kwenye moyo,mishipa ya veini utoa damu chafu kwenye mwili mpaka sehemu mbalimbali za mwili, Kwa hiyo basi na vile vile kwenye mapafu Kuna mishipa hiyo ya artery na vein naufanya kazi hiyo, ikitokea Kuna maambukizi kwenye mapafu na wadudu ubebwa kwenye mzunguko wa damu,mpaka sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye ubongo na kusababisha usaha sehemu hizo hizo nazo zinaweza kupata matatizo hayo hayo,Kwa hiyo wapendwa wasomaji matibabu ni lazima ili kuweza kuepuka madhara makubwa Zaidi.
4. Kuharibika Kwa mishipa inayopeleka na kutoa damu kwenye mapafu .
Kwa sababu ya kuwepo Kwa usahaa kwenye mapafu na pia pengine Kwa Sababu ya kuwepo Kwa maambukizi kwenye mapafu ambayo usababisha kuwepo Kwa damu usababisha kuharibika Kwa mishipa inayopeleka damu kwenye mapafu na kutoa damu kwenye mapafu, Kwa hiyo hali ya mgonjwa inawezekana kuwa mbaya Kwa sababu ya kukosa damu ya kutosha kwenye mapafu.na pengine hiyo mishipa inawezekana kushambulia na bakteria walipo Kwa sababu ya kukosa Kwa matibabu.
5. Upungufu wa hewa safi ambayo Kwa kitaalamu huitwa oxygen na kupngezeka Kwa hewa chafu kwenye mapafu ambayo Kwa kitaalamu huitwa carbon dioxide.
Kwa sababu ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu na kuharibika Kwa mishipa ambayo upeleka damu kwenye mapafu hali hii usababisha damu ya oxygen kupungua na kusababisha kuongezeka Kwa damu ya carbon dioxide kwenye mapafu hali ambayo usababisha maisha ya mgonjwa kuwa magumu, Zaidi Kwa hiyo matibabu ni lazima kabisa ili kuweza kuokoa maisha ya mgonjwa.
6. Baada ya kuona madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu kuwa ni mengi na matibabu yanahitajika Kwa mgonjwa ili kuweza kuokoa maisha ya mgonjwa na kujaribu kuelimisha jamii kuhusu kuwepo Kwa ugonjwa huu na kwamba unatibika na kujaribu kutoa Mila mbaya za kuwatenga wale walio na ugonjwa huu kwenye jamii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 web hosting π3 Dua za Mitume na Manabii π4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π5 Kitau cha Fiqh π6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Sababu za Hedhi Kuchelewa Bila Mimba
βKuchelewa kwa hedhi ni jambo linaloweza kuleta hofu na wasiwasi, hasa kwa wanawake wanaohisi kuwa mimba ndiyo sababu pekee. Hata hivyo, kuna sababu nyingi za kibiolojia na mtindo wa maisha zinazoweza kusababisha mzunguko wa hedhi kuvurugika. Post hii inachunguza visababishi hivi na kutoa mwongozo wa wakati mwafaka wa kuona daktari.
Soma Zaidi...Dalilili za maumivu ya kifua
Maumivu ya kifua huja kwa aina nyingi, kuanzia kuchomwa na kisu hadi kuuma kidogo. Baadhi ya Maumivu ya kifua yanafafanuliwa kama kuponda kuungua. Katika baadhi ya matukio, maumivu husafiri juu ya shingo, hadi kwenye taya.
Soma Zaidi...Sababu za wanawake kuwa na maumivu kwenye kiuno
Posti hii inahusu zaidi sababu za wanawake kuwa na maumivu kwenye viungo, ni ugonjwa unaowapata na wanaume ila kwa wanaweza unaowapata sana ukilinganisha na wanaume.
Soma Zaidi...fangasi, aina zao, dalili zao na matibabu yao
Fangasi na Aina zao Fangasi wa kwenye kucha Fangasi wa Mapunye Fangasi aina ya candida Fangasi wa Mdomoni na kooni Fangasi wa kwenye uke Fangasi wanaoshambulia mfumo wa damu na ogran kama moyo, figo n.
Soma Zaidi...Sababu za homa kwa watoto wachanga
Muhtasari (Executive Summary) βHoma kwa mtoto mchanga si ugonjwa wenyewe, bali ni ishara kwamba mfumo wa kinga ya mwili unapambana na kitu kigeni. Ingawa homa inaweza kuwatia hofu wazazi wengi, mara nyingi husababishwa na maambukizi ya virusi, bakteria, mabadiliko ya mwili kama kuota meno, au matokeo ya kawaida ya chanjo. Makala haya yanachambua sababu hizi kwa kina na kutoa mwongozo wa lini unapaswa kukimbilia hospitali haraka.
Soma Zaidi...