Madhara ya Tiba kemikali kwa wagonjwa wa saratani
Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba kemikali, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wa saratani, madhara haya yanayoweza kuwa ni kwa Sababu mbalimbali kama vile kuaribika kwa seli zinazoendelea kufanya kazi kwenye mwili.
Madhara ya Tiba kemikali.
1. Miwasho ndani ya pua na mdomoni, miwasho hii utokea sehemu za pua na midomoni ambayo uendana na kuwepo kwa vipengele ndani ya pua na midomoni na puani hali hii ikitokea kwa wagonjwa wa saratani wanapaswa kutumia dawa za kawaida zinazotumika kutibu maupele kwenye mdomo na puani na pengine hali ikiendelea mgonjwa anapaswa kuonana na daktari wake kwa ushauri zaidi na pia mgonjwa anapaswa kutumia sana vyakula vya kujenga mwili.
2. Kupoteza nywele kichwani.
Wagonjwa wa saratani upotea nywele kichwani hii ni kwa sababu ya kemikali ambayo uharibu mfumo wa seli na kusababisha nywele kuisha kwa mda kichwani, lakini baadae urudi tena hali hii ikitokea kwa wagonjwa wa saratani jamii inabidi kuelewa kuwa ni Sababu ya madawa na waepuke kuwa na Imani potofu kuhusu wagonjwa wa Aina hii na pia wanapaswa kutumia vyakula vya kutosha Ili kuweza kurudisha afya zao kwenye hali ya kawaida na vyakula viwe na virutubisho vya kutosha.
3. Mgonjwa anakuwa na uchovu
Kwa kawaida wagonjwa wanaotumia dawa hii ya Tiba kemikali huwa na uchovu wa mara kwa mara kwa Sababu seli zao huwa zimearibiwa na kemikali na kwa hiyo wakati wa Tiba mgonjwa uhisi kuwa na uchovu kwa hiyo anapaswa kupumzika na sio kupumzika mda wote Bali anapaswa kutembea kwa mda wa dakika Kumi na Tano Ili kuupatia mwili mazoezi ya kutosha ingawa mazoezi yasiwe ya mda mrefu Bali kidogo kidogo na pia kutumia vyakula vinavyoongeza nguvu mwilini Ili kuondoa uchovu wa mara kwa mara.
4. Mgonjwa anayetumia Tiba kemikali huwa na kichefuchefu .hali hii utokea kwa sababu ya dawa zinazotumika kuharibu mfumo wa umengenyaji ambapo mgonjwa uhisi kurudisha kila kitu anachokula kwa hiyo mgonjwa anapaswa kula kidogo kidogo na mara kwa mara, anapaswa kutumia vitu vigumu kama vile mkate na chapati na anapaswa kuepuka kuinama akae wima na kuepuka vyakula ambavyo huwa havipendelei vinaweza kusababisha kutapika .
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Maambukizi ya mfumo wa mkojo (UTI): Dalili zake kwa wanaume na wanawake.
​Maambukizi ya mfumo wa mkojo (Urinary Tract Infection - UTI) hutokea wakati bakteria wanapoingia kwenye mfumo wa mkojo na kusababisha maambukizi. Mfumo huu unajumuisha figo, mirija ya mkojo (ureters), kibofu cha mkojo, na mrija wa kutolea mkojo (urethra). Ingawa wanawake wako katika hatari zaidi ya kupata UTI kutokana na maumbile ya mwili wao, wanaume pia wanaweza kupata maambukizi haya. Makala haya yanafafanua dalili za kawaida na wakati wa kutafuta msaada.
Soma Zaidi...Mzio (aleji) na Dalili zake
Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kitomvuni, sababu zake na dalili zake
Hapa utajifunza sababu za kuwepo na maumovu ya tumbe kitomvuni.
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster. Kwa hiyo ili kugundua kubwa mtu ana Ugonjwa huu Dalili kama hizi zifuatazo zinaweza kutokea kwa mgonjwa.
Soma Zaidi...Magonjwa yanayowashambulia watoto wachanga
Watoto wachanga ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, watoto hawa hushambulia na maginjwa mara kwa mara na kusababisha ukuaji wao kuwa dunk,
Soma Zaidi...Ukweli Kuhusu Kupima HIV Nyumbani
Katika jitihada za kuongeza kasi ya upimaji wa VVU, njia ya kupima nyumbani (HIV Self-Testing) imekuwa suluhisho muhimu linalotoa faragha na urahisi. Makala hii inachambua ukweli kuhusu jinsi vipimo hivi vinavyofanya kazi, usahihi wake, na umuhimu wa kuelewa matokeo unayopata ili kuhakikisha afya yako inalindwa kwa njia sahihi.
Soma Zaidi...