picha

Madhara ya Tiba kemikali kwa wagonjwa wa saratani

Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba kemikali, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wa saratani, madhara haya yanayoweza kuwa ni kwa Sababu mbalimbali kama vile kuaribika kwa seli zinazoendelea kufanya kazi kwenye mwili.

Madhara ya Tiba kemikali.

1. Miwasho ndani ya pua na mdomoni, miwasho hii utokea sehemu za pua na midomoni ambayo uendana na kuwepo kwa vipengele ndani ya pua na midomoni na puani hali hii ikitokea kwa wagonjwa wa saratani wanapaswa kutumia dawa za kawaida zinazotumika kutibu maupele kwenye mdomo na puani na pengine hali ikiendelea mgonjwa anapaswa kuonana na daktari wake kwa ushauri zaidi na pia mgonjwa anapaswa kutumia  sana vyakula vya kujenga mwili.

 

2. Kupoteza nywele kichwani.

Wagonjwa wa saratani upotea nywele kichwani hii ni kwa sababu ya kemikali ambayo uharibu mfumo wa seli na kusababisha nywele kuisha kwa mda kichwani, lakini baadae urudi tena hali hii ikitokea kwa wagonjwa wa saratani jamii inabidi kuelewa kuwa ni Sababu ya madawa na waepuke kuwa na Imani potofu kuhusu wagonjwa wa Aina hii na pia wanapaswa kutumia vyakula vya kutosha Ili kuweza kurudisha afya zao kwenye hali ya kawaida na vyakula viwe na virutubisho vya kutosha.

 

3. Mgonjwa anakuwa na uchovu 

Kwa kawaida wagonjwa wanaotumia dawa hii ya Tiba kemikali huwa na uchovu wa mara kwa mara kwa Sababu seli zao huwa zimearibiwa na kemikali na kwa hiyo wakati wa Tiba mgonjwa uhisi kuwa na uchovu kwa hiyo anapaswa kupumzika na sio kupumzika mda wote Bali anapaswa kutembea kwa mda wa dakika Kumi na Tano Ili kuupatia mwili mazoezi ya kutosha ingawa mazoezi yasiwe ya mda mrefu Bali kidogo kidogo na pia kutumia vyakula vinavyoongeza nguvu mwilini Ili kuondoa uchovu wa mara kwa mara.

 

4. Mgonjwa anayetumia Tiba kemikali huwa na kichefuchefu .hali hii utokea kwa sababu ya dawa zinazotumika kuharibu mfumo wa umengenyaji ambapo mgonjwa uhisi kurudisha kila kitu anachokula kwa hiyo mgonjwa anapaswa kula kidogo kidogo na mara kwa mara, anapaswa kutumia vitu vigumu kama vile mkate na chapati na anapaswa kuepuka kuinama akae wima na kuepuka vyakula ambavyo huwa havipendelei vinaweza kusababisha kutapika .

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2344

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Sababu za Kutokwa na Uchafu Ukeni

Posti hii inachunguza hali ya kawaida ya kutokwa na uchafu ukeni, ikitofautisha kati ya uchafu wa kawaida (wa kisaikolojia) na ule unaoashiria matatizo ya kiafya. Tutajadili visababishi vikuu, dalili za hatari, na umuhimu wa kuona daktari kwa uchunguzi sahihi.

Soma Zaidi...
Aina mbalimbali za michubuko

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za michubuko,kwa Sababu michubuko utokea sehemu tofauti tofauti na pia Kuna aina mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Soma Zaidi...
Mbinu za kupunguza Magonjwa ya kuambukiza.

Posti hii inahusu zaidi mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu ambazo zinapaswa kutumika ili kupunguza kiwango cha magonjwa ya kuambukiza.

Soma Zaidi...
Fangasi wa sehemu za Siri

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu fangasi wa sehemu za Siri

Soma Zaidi...
Virusi vya Homa ya Ini (Hepatitis B): Dalili na chanjo.

Homa ya ini aina ya B (Hepatitis B) ni maambukizi makubwa ya virusi yanayoathiri ini. Virusi hivi vinaweza kusababisha ugonjwa wa papo hapo (wa muda mfupi) au sugu (wa maisha yote). Maambukizi sugu ya Hepatitis B yanaweza kusababisha uharibifu mkubwa wa ini, ikiwemo makovu (cirrhosis), saratani ya ini, na kushindwa kwa ini kufanya kazi. Makala haya yanakupa uelewa wa dalili zake na umuhimu wa chanjo kama njia kuu ya kujikinga.

Soma Zaidi...