MADHARA YA TIBA MIONZI


image


Post hii inahusu zaidi madhara ya Tiba mionzi kwa wagonjwa wa saratani, ni madhara yanayotokea kwa wagonjwa wanaotumia mionzi katika matibabu ya saratani.


1. Kupoteza hamu ya chakula.

Hii ni mojawapo ya madhara ambayo utokea kwa watumiaji wa mionzi kwa sababu ya kuwepo kwa dawa kwenye damu usababisha kuingilia mfumo wa  hamu ya kula kwa hiyo mgonjwa ushindwa kula, kwa hiyo mgonjwa anapaswa kula kidogo kidogo na kwa kila mara na pia anapaswa kula vyakula kama vile supu  na vyakula vingine vilaini Ili aweze kuruhusu dawa kufanya kazi maana dawa bila chakula mambo hayaendi vizuri.

 

2. Mgonjwa usikia uchovu mara kwa mara.

Kwa sababu mionzi uharibifu seli zinazosababisha saratani na vile vile zile ambazo ni nzima nazo uharibiwa na mionzi kwa hiyo  tunajua kabisa maisha yetu msingi wake ni seli kwa hiyo seli zikifa  bila kufikia mda wake na mambo mengine mwilini yanakwama ndo maana mtu uhisi uchovu kwa hiyo wanaotumia mionzi wanapaswa kupumzika kwa mda wa kutosha, kutembea walau dakika Kumi na Tano kwa siku na kunywa maji mengi, kula chakula Cha kutosha Ili kuupatia mwili nguvu.

 

3.Mabadiliko ya ngozi.

Kwa wagonjwa wanaotumia mionzi huwa na mabadiliko kwenye ngozi zao , pengine ngozi ubadilika na kuwa pinki, nyeusi, kuhisi moto kwenye ngozi, ngozi kuwa kavu, kuwasha na ngozi kuwa na upele au malengelenge kwa mgonjwa anayetumia mionzi akiona dalili kama hizi hasiogope Bali achukue dawa za kawaida zinazotumika kutibu magonjwa ya ngozi na pia apate ushauri wa daktari Ili kuweza kujua Cha kufanya maana madhara mengine kwenye ngozi huwa yanatisha na kumnyima mgonjwa amani.

 

4. Mgonjwa huisi kichefuchefu.

Kwa sababu dawa hizi za mionzi  zinaharibu seli na pia uingilia mfumo wa chakula na kumfanya mgonjwa kutaka kutapika kila kitu, kwa hiyo mgonjwa anapaswa kukaa woman Ili asitapike, pia anapaswa kula chakula kidogo kidogo kwa wakati b tofauti na pia anapaswa kujiadhari na vyakula vile ambavyo huwa havipendelei Ili kuepuka kutapika kwa kufanya hivyo mgonjwa ataweza kula chakula na dawa zitaweza kufanya kazi.

 

5. Tukumbuke kuwa mionzi huua seli zinazosababisha saratani na pamoja na zile ambazo ziko kawaida na pia mwili wa binadamu unapaswa kuwa na seli zinatosha Ila kwa sababu ya magonjwa seli zinaharibika kwa mionzi kwa hiyo wagonjwa hawa wanahitaji uangalizi wa karibu na kupewa chakula chenye virutubisho vyote Ili waendelee kuishi na pia jamii inapaswa kuwasaidia na kuwapa ushirikiano wa karibu.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    3 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya php    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Dalili za Kiharusi Cha joto la mwili.
Kiharusi cha joto ni hali inayosababishwa na joto la juu la mwili wako, kwa kawaida kama matokeo ya kufichuliwa kwa muda mrefu au bidii ya mwili katika joto la juu. Aina hii mbaya zaidi ya jeraha la joto, kiharusi cha joto kinaweza kutokea ikiwa joto la mwili wako litapanda hadi 104 F (40 C) au zaidi. Soma Zaidi...

image Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani, Soma Zaidi...

image Fida za kula uyoga
Uyoga pia ni katika vyakula vya asili, ijapokuwa upatikanaji wake umekuwa mchache siku hizi. Shukrani ziwaendee wataalamu wa kilimo, kwa sasa tunaweza kuzipata mbegu za uyoga kutoka maabara na kulima uyoga popote pale. Wataalamu wa mimea wanaamini kuwa uyoga si katika mimiea kwani uyoga upo katika kundi la viumbe liitwalo fungi (kingdom fungi). ila tunapozungumzia vyakula uyoga tunauweka kwenye kundi la mbogamboga. Uyoga una virutubisho vingi na vizuri kwa afya. Soma Zaidi...

image Huduma kwa wasioona hedhi
Posti hii inahusu zaidi msaada au namna ya kuwahudumia wale wasioona hedhi na wamefikiwa kwenye umri wa kuweza kuona hedhi. Soma Zaidi...

image Zijue faida za mate mdomoni
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa mate mdomoni, mate ni majimaji ambayo hukaa mdomoni na husaidia katika kazi mbalimbali mdomoni. Soma Zaidi...

image Virusi vinavyopelekea Kuharisha Sana na Kutapika Sana(norovirus)
Maambukizi ya Norovirus yanaweza kusababisha kutapika sana na Kuhara. Virusi huambukiza sana na kwa kawaida huenea kupitia chakula au maji ambayo yamechafuliwa na kinyesi wakati wa kutayarisha. Unaweza pia kuambukizwa kwa kuwasiliana kwa karibu na mtu aliyeambukizwa. Kuhara, maumivu ya tumbo na kutapika kwa kawaida huanza saa 24 hadi 48 baada ya kuambukizwa. Dalili za Norovirus hudumu siku moja hadi tatu, na watu wengi hupona kabisa bila matibabu. Hata hivyo, kwa baadhi ya watu hasa watoto wachanga, watu wazima na watu walio na ugonjwa wa msingi kutapika na Kuhara huweza kukosa maji mwilini kwa kiasi kikubwa na kuhitaji matibabu. Maambukizi ya Norovirus hutokea mara nyingi katika mazingira yaliyofungwa na yenye watu wengi kama vile hospitali, nyumba za wauguzi, shule na meli za kusafiri. Soma Zaidi...

image Namna ya kuepuka Ugonjwa wa ngiri.
Posti hii inahusu zaidi namna au njia za kuepuka na Ugonjwa huu wa ngiri ambao uleta madhara kwa watoto, vijana na watu wazima, kwa hiyo ili tuweze janga hili ni lazima tufanye yafuatayo. Soma Zaidi...

image Zifahamu sofa za seli
Seli ni chembechembe hai ambazo zimo ndani ya mwili wa binadamu na hufanya kazi mbalimbali kwenye mwili, binadamu hawezi kuishi bila seli. Soma Zaidi...

image Faida za chanjo
Posti hii inahusu zaidi faida ya chanjo, tunajua wazi kuwa chanjo Ina faida kubwa kwenye mwili wa binadamu na vile vile kwenye jamii kama tutakavyoona hapo chini. Soma Zaidi...

image Sababu za mwanamke kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa
Posti hii inazungumzia kuhusiana na sababu zinazosababisha kukosa hamu ya kushiriki tendo la ndoa. Soma Zaidi...