Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme

Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu.

Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme.

1. Fundisho la kwanza ni kwamba ukipata watoto wakiwa kwenye jinsia tofauti, watoto wote ni sawa.

Kwa mfano kuna mama anaweza kupata watoto wa kiume tu au wa kike tu mshukuru Mungu kwa sababu huwezi kujua nani atakusaidia kwa sababu tumeona jinsi mke mdogo wa mfalme alivyokuwa na wasiwasi sana baada ya kuona tatizo lake linagundulika la kumtupa Mtoto wa kike na kubakiza wa kiume ingawa alichokipenda alikipata ila kwa kutumia nguvu na mda hata kama angejifungua wote wawili me sioni shida bali mmoja angerithi ufalme na mwingine angebaki kawaida.

 

2. Pia fundisho la pili kutokana na hadithi hii ni kwamba wasichana acheni tabia ya kutupa watoto kwa sababu ujui unayemtupa ndiye atakufa upoteze amani baadae , kwa mfano unaweza kutoa mimba ukaitoa vibaya na kizazi kikapitiwa kwa hiyo utaumia maisha yako yote , kama mke mdogo alivyoangaika kwa kitendo cha kutomtambulisha mtoto wa kike kwa mfalme.

 

3 fundisho la tatu ni kwamba tunapaswa kuachana na usaliti katika maisha kwa sababu mtoto wa kiume wa mfalme baada ya kuona yule binti kwa mzee aliweza kushawishika na kuamua kumwacha mkewe mpandwa aliyepigania na kukosa uhusiano mzuri na mama yake akaona msichana wa kwa mzee.

 

4. Fundisho la nne ni kwamba wivu ni mbaya kwa sababu wake wenza walimwonaea wivu mke mdogo akaamua kutoroka na kuzaa watoto wawili msichana na mvulana , mmoja akamwacha kwa bibi, labda hasingeonewa wivu na kutoroka angezalia kwa mumewe hasingemtupa kwa bibi yule msichana.

 

5.  Katika maisha yetu tuache kuwa ndumila kuwili kama bibi mara yuko kwa mtoto wa kiume wa mfalme, mara kwa mke mdogo wa mfalme, mara yuko kwa mke mkubwa wa mfalme, mara yuko kwa mzee lengo lake ni kupata maslahi yake na alifanikiwa.

 

6. Fundisho la mwisho wanaume wanapaswa kuwa na msimamo mkubwa kwenye familia zao bila kuendesha na wanawake sawa ingawa kushauriana ni kuzuri ila kuna mambo mengine makubali tu bila kuchunguza kama mfalme alivyokuwa anakubali kila kitu kutoka kwa mke mdogo.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF Views: 2618

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 ai web app     πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

USALITI (sehemu ya pili)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya Usaliti kati ya Rhoda na Moses ambapo Moses anampenda sana Rhoda na wakati wa kuoa umefika ila akagikilia kwamba akimuoa Rhoda inawezekana wasipate watoto kwa sababu ya mimba ambazo Rhoda alikuwa anatoa mara kwa mara.

Soma Zaidi...
Hadithi katika kijiji cha burugo

Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii .

Soma Zaidi...
Mahusiano ya vijana wawili

Posti hii inahusu zaidi mahusiano yaliyotokea kati ya vijana wawili ila yanafika baadae mmoja akamsaliti mwenzake.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tatu)

Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya kijana Frank na Amisa pia na wapenzi wawili ambao ni James na Amina.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.

Soma Zaidi...
NIMLAUMU NANI (sehemu ya nne)

Post hii inahusu zaidi kijana Frank anayelazimishwa kuolewa na Amisa yeye hayuko tayari ila kwa sababu ya maisha kuwa magumu anaamua kulala na Amina na kumbebesha Mimba ya watoto mapacha.

Soma Zaidi...