huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database.
Katika somo lililotangulia tumejifunza amna a kupangilia taarifa za kwenye databse. Tuliona namna ya kutumia ORDER BY. Isha tukapanga data zetu kutoka kubwa kwenda ndogo na kinyume chake. Sasa katika somo hili tutatkwenda kuendelea na nnamna ya kupangilia data hizo ila kwa kutumia WHERE .
Kwa nini tunatumia where ?
Tunatumia WHERE endapo tuna masharti yanatakiwa yafikiwe ili data kuonekanna. Kwa mfano unataka kusoma menu zote ambazo gharama yake ni zaidi ya 1000. hapa hili tunaita ni sharti ama condition. Sasa ili sharti hili liweze kufanya kazi kwenye SQL tunatumia where.
1. Mfano wa kwanza
Tunahitaji kusoma data zote ambazo price yake ni sawa na 1000.
Kufanya hivyo tutatumia alama ya = mbele ya where. Hivyocommand nzima itaonekana.
SELECT * FROM `menu` WHERE price =1000
hapo menu itakayoonekana ni ile tu ambayo proce yake ni sawa na 1000.
2. Mfano wa pili
Tunataka kusoma data ambazo id yake ni 3, 4, na 8. yaani data tu zenye id hizo ndizo tunataka kuziona na si nyinginezo. Hivyo tunatarajia kuwa na row tatu tu. Kufanya hivyo tutatumia OR kwa maana au. Yaani eidha id iwe 3 au id iwe 4 au id iwe 8. Na command yote itaonekana hivi
SELECT * FROM `menu` WHERE id =3 OR id =4 OR id =8; pia unweza kuondoa nyota na kupunguza column
SELECT name, price FROM `menu` WHERE id =3 OR id =4 OR id =8;
3. Mafno wa tatu
Chukulia mfano kwenye menu kuna ugali mbili. Kuna ugali nyama abayo ni 1500 na kuna ugali ng’onda ambaypo ji 1000. sasa mimi nataka kusoma ile ambayo ni ugali nyama ya 1500. kumbuka zote ni ugali na kwenye menu zitanasomeka hivyo hivyo. Ili kuona ya ugali 1500 tu tunatakiwa tutumie AND yaani tuselect ugali lakini kwa ulazima kuwa na id yake iwe 1. ambapo kwenye menu yetu id 1 ni ugali hivyo itakuwa hivi:-
SELECT * FROM menu WHERE name = 'ugali' AND id =1
Kuna jambo hapa unatakiwa ulijuwe. Tunapotumia string (sting ni mkusanyiko wa herufi na namba, rejea mafunzo ya php) value inatakiwa ikae ndani ya alama za kufnga na funguwa semi ‘’ kama ulivyo kwenye mfano 'ugali'.
4. Tofauti ya AND na OR.
Unapotumia AND maana yake ni lazima masharti yafikiwe ili data kuonekana. Ila unapotumia OR hata shart moja likifikiwa data zitaonekana. Kwa mfano kwenye mfano namba 2 hapo hata kama kusingekuwa na id 3 data zingeonekana lakini kama tungetumia AND endapo id tatu isingekuwepo kwenye database yetu data zote zisingesoma.
5. Mfano wa nne
Tunahitaji kusoma menu ambazo tu majina yake yameanziwa na herufi u. chukulia mfano kuna orodha ya majina ya vyakula 50 kwenye hoteli moja kubwa sana. Sasa nataku kuona vyakula vinavyoanziwa na herufi u tu, hapo nikiwa naamini nitaona bei ua ugali kwa haraka zaidi tofauti na kuanza kusoma kutoka kwanzo hadi mwisho.
Kufanya hivi tutatumia LIKE kisha tutaweka hiyo heru u kikifuatiwa na alama ya asilimia %. na ikiwa unahitaji kufatuta menu iliyoishiwa na herufi u basi alama ya asilimia % utaiweka mwanzo mfano %u. mfano huu pia utaweza kuutumia kama unataka kusearch kitu kwenye database ambacho kinaanziwa na herufi fuani. Hivyo kulingana na mfano wetu command itakuwa hivi:-
SELECT * FROM menu WHERE name LIKE 'u%'
Tutajifunza zaidi somo hili tutakaposoma namna ya kutafuta kitu kwenye database. Hila unaweza kutumia mfano huu pia kutafuta kitu kama mpangilio hapo unavyouona. Mfano unataka kutafuta neno supu utaweka ‘supu%’
6. Mfano wa tano
Kwa kutumia SQL pia unaweza tumia mathematical operation kama >, <, !=, == na nyinginezo. Hapa nitatumia < na >. kwa ufupi > humaanisha kubwa kuliko na < humaanisha ndogo kuliko. Hapa nitatuia mifano miwili tu ya > na < .
A. Tunahitaji kuona menu ambazo price zake ni kubwa kuliko 1000 hapa tutatumia > .hivyo menu itakayokuja ni ile tu ambayo price yake imezidi 1000. hivyo itakuwa hivi
SELECT * FROM menu WHERE price >1000
B. Tunataka kuona menu ambazo price yake ni ndogo kuliko 900. hapa tutatumia <, hivyo menu tutakazoona ni zile tu ambazo price yake haijafika 900. hivyo itakuwa hivi:-
SELECT *FROM menu WHERE price <900
Tukutane somo la 12 tutajifunza kanuni kadhaa za kihesabu kwa kutumia SQL. Tafadhali usikose somo la 12 kwani ndio somo letu la mwisho wa course hii ta mafunzo ya database kwa kutumia MySQl.
Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email: mafunzo@bongoclass.com
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.
Soma Zaidi...Hii ni tafiti ambayo itakushangaza, kwa namna ambavyo matumizi ya AI yalivyo na athari kwenye uwezo wa kufikiri
Soma Zaidi...Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako.
Soma Zaidi...Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.
Soma Zaidi...katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment
Soma Zaidi...Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.
Soma Zaidi...Hili ni somo la Tatu katika mfululizo wetu wa mafunzo ya HTML kwa basic level kwa wanaoanza kujifunza. Hapa tutakwenda kujifunza tag za html ambazo huwa zinatumika katika uandishi.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.
Soma Zaidi...Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass
Soma Zaidi...Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP
Soma Zaidi...