picha

Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1

Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.

MAFUNZO YA DATABASE SQL (MYSQL)

haya ni mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MYSQL. Katika mafunzo haya utajifunza namna ya kuthibiti taarifa kwnye database kwa kutumia software ya mysql.  Pamoja na mafunzo ya php na html utaweza pia kuzitumia taarifa hizi moja kwa oja kwenye blog ama website yako.

 

 

Mafunzo haya yatakujia kupitia mfundishaji wako Mr. Rajabu kutoka bongoclass. Mwisho wa mafunzo haya utaweza kumilii database yeko ya online ambapo utaweza kuweka na kupata taarifa popote ulipo kutoka kwenye kifaa chochote kile. Kumbukacourse hii inakuji free kabisa bila ya malipo. Unachotakiwa ni kushiriki vyema tu.

 

 

VIGEZO VYA KUSHIRIKI MAFUNZO:

  1. Uwe na simu janja yenye kiendeshi cha Android au uwe na kompyuta
  2. Uwe mjanja
  3. Una uzoefu wa kutumia software ama android App mbalimbali kama excel,
  4. Uweze kusoma na kuandika angalau maneno marahisi ya kiiingereza kama create, drop, user, select, where, into, update, order na mengine yanayofanana na haya.

 

 

MAANDALIZI YA SOMO:

Ili kuweza kuendelea na somo hili hakikisha kuwa umesakinisha App zifutazo kwenye kifaa chako.

  1. Kama unatumia simu AWEBSERVER tumia link hii https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sylkat.apache

 

  1. Kama unatumia kompyuta download wampserver ama xamp vyema ukaanza na xamp maana wampserver wakati mwingine inasumbuwa kwenye kuinstall kama kompyta haipo update.

 

Baada ya kufukia hapo utakuwa umeshamaliza maandalizi ya somo.

 

 

JINSI YA KUANZA:

KAMA UNATUMIA SIMU:

  1. Funguwa App yako
  2. Bofya start kuanza huduma ya server iwe active
  3. Kwenye menu upande wa juu kuna kapicha kama suka sufuria kameandika Mysql bofya hapao.
  4. Bofya start ili kuanza huduma
  5. Utaona kulia mwa neno admin kuna link yenye sura hii 0.0.0.0:8080/mysqladmin
  6. Bofya kwenye link hiyo
  7. Utyaona kuna ukurasa ukekuja unakuhitaji kuweka user name na password
  8. Username weka root na password weka root
  9. Kisha bofya log in
  10. Utafunguka ukurasa mpya ambao utaona neno database kwa juu.

 

 

Kama umefika hatuwa hii HONGERA somo letu la kwanza litaanzia hapo

 

 

KAMA UNATUMIA KOMPYUTA:

Kama unatumia xamp

  1. Funguwa software ya xamp
  2. Kutafunguka kiukurasa kadogo kenye menu.
  3. Kwenye apache bofya start
  4. Kwenye Mysql bofya start
  5. Kisha kwenye Mysql bofya Admin
  6. Utaona kuna ukurasa mkubwa umefunguka kwenye browser yako.
  7. Neno databases utaliona kwa juu
  8. Hapa utakuwa upo tayari kwa somo lijalo.

 

 

KAMA UNATUMIA WAMPSERVER

  1. Ifunguwe hiyo software
  2. Nenda kwenye tray upande wa kulia utaikuta ipo active
  3. Right click
  4. Kwenye menu bofya phpmyadmin
  5. Ukurasa mpya utafunguka na neno database litaonekana kwa juu.
  6. Kama umefuka hatuwa hii upo tayari kwa somo linalofata.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/11/14/Sunday - 09:51:12 am Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 2653

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Utangulizi wa Android App Development

Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8

Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tano (5)

Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tisa (9).

Somo la nane mafunzo ya php, katika somo hili utajifunza kuhusu array na jinsi ya kutengeneza array.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza (basic level)

Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL somo la 3

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la pili (2)

hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php.

Soma Zaidi...