Mafunzo ya hadithi zilizochaguliwa
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
7.2. Mafunzo ya Hadith Zilizochaguliwa.
- Hadith ya Kwanza; Kuamrisha mema na Kukataza Maovu.
Kutoka kwa Abi Saidil-Khudhur (r.a) amesema: Nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi Mungu anasema;
“Mwenye kuuona uovu miongoni mwenu na auondoshe kwa mkono wake, ikiwa hawezi (na aondoshe) kwa ulimi wake iwapo hawezi (na aondoshe) kwa moyo wake (achukie) na hiyo ndiyo imani dhaifu.”
(Ameipokea Muslim).
Hatua za kuondosha uovu:
- Hatua ya kwanza na bora ni kuondosha kwa mikono.
- Hatua ya pili kwa ubora ni kuondosha kwa kusema.
- Na hatua ya mwisho na dhaifu ni kuchukia moyoni.
Mafunzo ya Hadith kwa Ufupi:
- Ni wajibu kuondosha maovu kwa kisaidizi chochote kile kiwacho kulingana na mazingira.
- Jukumu la kuamrisha mema na kukataza maovu linaanzia kwa mtu mmoja mmoja na ummah kwa ujumla
- Kutochukia uovu na kuridhika nao ni dalili ya kukosa imani moyoni.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Simulizi za Hadithi Audio π2 Kitabu cha Afya π3 kitabu cha Simulizi π4 ai web app π5 Madrasa kiganjani π6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
DUA 113 - 126
DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu βLAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-βADHIMUL-HALIIMU.
Soma Zaidi...ni nyakati zipi ambazo dua hukubaliwa kwa haraka?
Dua ni moja ya ibada ambazo zinamfanya mja awe karibu na Mweznyezi Mungu. Allah amesisitiza tumuombe dua kwa shida zetu zote, pia akaahidi kuwa atatujibu maombi yetu muda wowote tutakao muomba. Sasa ni zipi nyakati nzuri zaidi kuomb adua?
Soma Zaidi...