picha

Mafunzo ya php level 1 somo la tatu (3)

hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.

SOMO LA TATU

NAMNA YA KUWEKA VARIABLE

Variable ni moja katika kitu mihimu kwenye faili la php. Huwezi kuunganisha tovuti yako kwenye database, huwezi kuzifikia data kwenye database bila kutumia variable. Huwezi kuweka function bilakutumia variable. Kwa ufupi php inazungumza kwa kutumia variable.

 

Variable ni nini?

Ni ngumu kutoa maana ya hili neno likafahamika bila maswali, ila niseme tu kwa ufupi variable unaweza kuwema ni chombo cha kuhifadhia data kwenye program. Unaweza kuzikusanya data nyingi zinazofanana kwa kutumia variable moja.

 

Kwa mfano unaweza kusema neno gari likawa na mgawanyiko kama toyota, benzi, basi na pikap. Sasa badala ya kuyaida majina yao unaweza tu kuweka variable ya gari hala fu compyuta ikadisplay magariyote. Badala ya kuanza tena kutaja, majina ya magari unaweka variable gari yanakuja yote.

 

Cheki mfano huu:

<?php

$gari = array("basi", "benzi", "toyota","tractor", "isuzu");

echo "tunauza magari aina ya ". $gari[2].",". $gari[1].".";?>

Kwa kutumia variable gari naweza kutaja vina la gari lolote kati ya hayo bila ya kuandika jina lake halisi. Hii inasaidia kusave time.

 

Kanuni za kuweka variable

  1. Kwanz aunatakiwa uanze na alama ya dola ambayo ni $
  2. Kisha utaandika jina la variable usianze na namba
  3. Kisha ruka nafasi kisha weka alama ya =
  4. Kisha weka alama za kunukuu “   ”
  5. Ndani ya alama za kunukuu andiak thamani ya variable yako, yaani unataka variable hiyo iwakilishe nini?
  6. Weka alama ya semi colon ambayo  ni ;
  7. Baada ya hapo ni kuitumia variable yako.

 

Mafano 1

<?php

$chakula = "ugali wa sembe iliyonyeupe na samaki wa bwawani pamoja na kachumbari yenye ndimu nyingi";

echo " napenda kula $chakula";

?>

 

Kw akutumia mfano huu, baada ya kuyaudia maneno yaliyopo kwenye variable ambayo ni “ugali wa sembe iliyonyeupe na samaki wa bwawani pamoja na kachumbari yenye ndimu nyingi” sasa badala ya kuyaridia rudia nitatumia neno chakula kisha maneno hayo yatatolea. Haijalshi nimeyarudia mara ngapi.

 

Mfano 2

<?php

$a = "kaka";

$b = "mama";

$c = "baba";

$d = "shamba";

echo "$a, $b, na $c wamekenda $d kulima mihogo";

?>

Hapa utaona sentensi hii inasomeka kaka, dada na baba wamekwenda shamba kulima mihogo. Kwa kutumia variable hakuna haja ya kuandika tena kaka, dada na baba.

 

Unaweza kutumia variable kwenye elementi za HTML na kuleta matokeo kulingana na element ya HTML iliyotumika na style ambazo zimetumika. Angalia mfano namba 3 hapo chini:-

Mfano 3

<?php

$a = "kaka";

$b = "mama";

echo "

<h1><b>hiini hadithi ya $a na $b </b><h1>";

?>

 

Katika sentenzi hii hii hadithi ya kaka na baba, tag ya HTML <h1> na <b> zitatumika kuifanya sentensi iwe heading 1 na kuwa bolded.

 

Unaweza pia kutumia variable kufanyia hesabu, angalia mfano wa nne hapo chini

Mfano 4

<?php

$e = "5";

$f = "7";

$g = "5";

 

echo $e + $f;

echo "<br>";

echo $f * $g;

 

?>

Hapa utapata jibu la hesabu ya kwanza

5  + 7 ambalo ni 12

Na hesabu ya pili ambayo ni

7 * 5 ambalo ni 35

 

Kwa ufupi hivi ndivyo variable zinavyoweza kuhifadhi taarifa katika gaili la php. Ttajifunzamengi zaidi kuhusu variable katika masomo yanayokuja.

 

 

LINE BREAK KWENYE PHP

Katika html tulijifunza kuwa tag ya <br> ndio hutumika kukata msitari. Katika php endapo utaitumia tag hii inaweza kukupa error. Hivyo ili uweze kuitumia unatakiwa uiweke ndani ya echo ama print. Angalia mfano namba tano hapo chini

 

Mfano 5

<?php

echo "hi my budy are you drinking?";

echo "<br><br>";

echo "welcome at bongoclass";

?>

 

Hapo kama <br> itakuwa nje ya echo faili halitaweza kufunguka. Katika masomo yanayofata tujifunzapia namna ya kuongeza space zaidi ya moja kwenye php.

 

Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email:mafunzo@bongoclass.com

Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tehama Main: Post File: Download PDF Views 1265

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 web hosting     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 4 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 4)

Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la kumi (10)

Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 3 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la Tatu katika mfululizo wetu wa mafunzo ya HTML kwa basic level kwa wanaoanza kujifunza. Hapa tutakwenda kujifunza tag za html ambazo huwa zinatumika katika uandishi.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la sita (6)

Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 5

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako.

Soma Zaidi...