image

Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Mafunzo yatokanayo na Hijrah ya Mtume (s.a.w) na Maswahaba wake.

  1. Hatuna budi kutunza na kurejesha amana za watu kwa wenyewe bila kujali uadui wao kwetu.

 

  1. Waislamu hawanabudi kuweka mipango na mikakati madhubuti juu ya namna ya kutekeleza mambo yao kabla ya utekelezaji wake.

 

  1. Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari katika kuendesha harakati za kidini kwa kuzingatia kuwa dini ya Uislamu ina maadui wengi.

 

  1. Nusura ya Allah (s.w) na Ushindi hupatikana tu baada ya kufanyika jitihada za dhati katika kuusimamisha Uislamu katika jamii na kumtegemea yeye pia.

 

  1. Waislamu wanalazimika kufanya jitihada ya dhati ya kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yao, kama mazingira yatakuwa ndio kikwazo hawanabudi kuhama (kuhajiri) kwenda sehemu (ardhi) yenye wasaa.

Rejea Qur’an (4:97-99).

 

  1. Kuhajiri (kuhama) kwa ajili ya Uislamu sio ukimbizi, bali ni katika mikakati na mipango ya kwenda kujiimarisha huko na hatimaye kuja kukomboa sehemu mlikotoka.

 

  1. Kutokana na Hijrah ya Mtume (s.a.w), tunajifunza kuwa waislamu wote ni ndugu mmoja bila ya kujali kabila, rangi, taifa, n.k.

 

  1. Uislamu siku zote hauwezi kusimama katika jamii mpaka waislamu tuwe tayari kujitoa muhanga kwa mali na nafsi zetu kadri ya uwezo wetu.

 

  1. Ni haramu kwa muislamu kuishi katika nchi ya kikafiri au utawala wa kikafiri isipokuwa, itakapokuwepo jitihada ya kuundoa ukafiri na kuutawalisha Uislamu au yatakapokuwepo maandalizi ya kuhama sehemu hiyo





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1087


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

MASWALI MUHIMU KUHUSU HISTORIA NA MAISHA YA MTUME (S.A.W)
1. Soma Zaidi...

Mbinu na njia walizotumia maadui wa uislamu dhidi ya waislamu na dola ya kiislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

tarekh 09
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...

tarekh
Soma Zaidi...

Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu
Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s. Soma Zaidi...

Mambo ya Msingi Aliyofanya Mtume(s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah.
Mambo ya Msingi Aliyofanya Mtume(s. Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 05
Soma Zaidi...

Kupigwa vita Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...

Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?
Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri? Soma Zaidi...

Mbinu walizotumia makafiri wa kiqureish katika kuupinga uislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA NA MAISHA YA NABII ISMAIL(A.S)
Ismail(a. Soma Zaidi...

Hitimisho juu ya Historia ya maimam wanne
Soma Zaidi...