Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika
DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.
DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO
Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo. Basi HIV nayo ina hatua zake mpaka kuwa UKIMWI.
DALILI ZA MWANZO ZA HIV AMA UKIMW
Dalili hizi huanza kuonekana kuanzia wiki mbili mpaka nne na wakati mwingine mpaka sita toka kuingia mwilini. Mara chache sana huweza kuonekana mwanzoni mwa wiki ya kwanza. Katika kipindi hiki mtu anaweza kuona dalili zifuatazo:
1.kufimba kwa tezi za kwenye makwapa, mapaja na shingo
2.Homa
3.Uchovu
4.Kuharisha
5.Kupungua uzito
6.Kikohozi
7.Pumzi kutoka kidogodogo
8.Mafua
Dalili hizi pia zinaweza kuhusiana na maradhi mengine, hivyo inaweza kuwa vigumu kujuwa nini chanzo zaidi. Wengi katika wanaopata HIV wametaja kuwa kuvimba kwa tezi ndio dalili pekee walioweza kuopata mwanzoni mwa kuathirika kwao. Wengine wanataja mafua kuwa ndio dalili yao ya kwanza.
Baada ya kipindi hiki kupita mgonjwa hatapata dalili yeyote ile. Hiki ni kipindi hatari sana kwani mtu hataweza kujijua kama ameathirika. Kipindi hiki kinaweza kudumi mpaka miaka 10. katika kipindi hiki virusi vinaendelea kuathiri seli za mwili. Baada ya mwili kuwa umeathirika sana na kudhoofu mtu ataanza kupata dalili za UKIMWI.
DALILI ZA UKIMWI
1.kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku
2.Kupata homa za mara kwa mara na kuhisi baridi
3.Kikohozi
4.Kushinwa kupumua vyema
5.Madoa madoa kwenye ulimi na mdomoni
6.Maumivu ya kichwa
7.Uchovu usiokuwa na sababu na usioisha
8.Kutokuona vyema
9.Kupungua uzito
10.Mapele na ukurutu kwenye ngozi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Madrasa kiganjani ๐2 Dua za Mitume na Manabii ๐3 Kitau cha Fiqh ๐4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐5 kitabu cha Simulizi ๐6 ai web app
Post zinazofanana:
Hedhi isiyo na mpangilio: Chanzo chake na nini cha kufanya?
โMzunguko wa hedhi ni kiashiria muhimu sana cha afya ya mwanamke. Hata hivyo, wanawake wengi hukumbana na changamoto ya hedhi isiyo na mpangilio (irregular periods) katika kipindi fulani cha maisha yao. Makala hii inachambua kwa kina vyanzo vikuu vya kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi, kuanzia mabadiliko ya mtindo wa maisha hadi matatizo ya kiafya kama PCOS, na kutoa mwongozo wa hatua za kuchukua ili kurejesha usawa wa mwili wako.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kitovuni
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya tumbo kitovuni
Soma Zaidi...Magonjwa ya kuambukiza.
Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya kuambukiza, ni magonjwa ambayo yanaweza kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kuweza kusababisha madhara yale yale kwa mtu aliyeambukizwa au anayeambukiza kwa hiyo Maambukizi yanaweza kuwa ya moja kwa moja au yasi
Soma Zaidi...โJe, Fangasi Ukeni Huambukiza?
โUgonjwa wa fangasi ukeni (Vaginal Candidiasis) ni miongoni mwa changamoto kubwa za kiafya zinazowasumbua wanawake wengi duniani. Swali kubwa ambalo limekuwa likitatanisha wengi ni iwapo ugonjwa huu unaambukiza, hasa kupitia kushiriki tendo la ndoa. Makala haya yanajibu swali hilo kwa kina, yanachambua jinsi maambukizi yanavyotokea, na kutoa ukweli wa kisayansi (Fact Check) ili kuondoa dhana potofu mitaani.
Soma Zaidi...Maambukizi kwenye mrija wa mkojo(urethritis )
Posti hii inahusu zaidi maambukizi kwenye mrija wa mkojo, maambukizi haya usababishwa na virusi na bakteria.
Soma Zaidi...