ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA
Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo.
ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOKUTIBU MALARIA
Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo. Lakini kabla ya kutokea kifo malaria huanza kwa kuathiri maeneo nyeti sana ya kiafya na hivyo hupelekea athari kubwa ambazo huleta kifo. Hebu tuone maeneo ambayo malaria hushambulia:-
Ubongo, vimjidudud vya malaria vinapoingia kwenye mfumo wa damu huanza kushambulia seli hai nyekundu za damu. Kupitia damu vijidudu hivi vinaweza kuingia kwenye ubongo na kusababisha kuziba kwa vimishipa vijidogo ndani ya upongo. Vimishipa hivi ndivyo hupeleka virutubisho na hewa kwenye ubongo. Hali hii inaweza kumfanya mgonjwa achanganyikie na kupoteza fahamu kabisa.
Ini na figo, vijidudu hivi vinaweza kusababisha ini na figo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi, ama tena kufa kabisa. Endapo hali hii ikitikea basi itakuwa ni athari kubwa sana katika afya ya mtu husika.
Mapafu, endapo malaria haitatibiwa na ikiendelea kuwepo mwilini inaweza kusababisha kujaa kwa majimaji kwenye mapafu. Hali hii inaweza kusbabisha mgonjwa kushindwa kupumua kwa ufanisi. Endapo hili litatokea itakuwa ni katika athari mbaya sana za malaria.
Damu, kwakuwa vijidudu hivi hushabulia seli hai nyekundu za damu, na seli hizi ndizo hubeba hewa ya oksijeni na kuisambaza mwilini. Hivyo malaria inaweza kusababisha upungufu wa hewa ya oksijeni mwlini na kusababisha ugonjwa unaotambulika kama anaemia.
Wakati mwingine malaria inaweza kuwa kali zaidi na kusababisha sukari kushuka, hali hii kitaalamu inajulukana kama hypoglycaemia. Na ni katika hali mbaya sana kwani mgonjwa anaweza kupoteza fahamu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Maumivu ya shingo na mabega kutokana na kazi za ofisini.
Msongo wa mawazo (stress) ni hali ya kawaida ya kisaikolojia na kimwili inayotokana na shinikizo la maisha. Ingawa kiasi kidogo cha msongo kinaweza kuchochea ubunifu na utendaji, msongo wa muda mrefu ni hatari kwa afya ya mwili na akili. Makala haya yanachunguza kwa kina dalili za msongo wa mawazo—kuanzia mabadiliko ya kihisia, kimwili, hadi kitabia—pamoja na mikakati ya kitaalamu ya kuyatambua na kuyadhibiti mapema ili kuzuia madhara ya kudumu.
Soma Zaidi...Kisukari cha Aina ya 2: Dalili 10 za awali unazotakiwa kuzijua.
​Kisukari cha Aina ya 2 (Type 2 Diabetes) ni janga la kimataifa la kiafya linalokua kwa kasi, huku watu wengi wakiishi na hali hii bila kujijua. Post hii inachunguza kwa kina dalili 10 za awali, ikitoa mwongozo wa kitaalamu wa jinsi ya kutambua mabadiliko ya mwili, umuhimu wa utambuzi wa mapema, na hatua za kuzuia madhara ya muda mrefu kupitia mabadiliko ya mtindo wa maisha.
Soma Zaidi...Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu kwa wanawake na wanaume
Somo hili linakwenda kukueleza vitu vinavyosababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu
Soma Zaidi...Mzio (aleji) na Dalili zake
Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Jinsi ya kutoa huduma ya kwanz akwa liyeshambuliwa na pumu
Hii ni huduma ya kwanza kwa aliyeshambuliwa na pumu katika mazingira ambayo ni mbali na kituo cha afya, na hakuna dawa.
Soma Zaidi...Matatizo ya tezi ya shingo (Thyroid disorders): Dalili zake.
Tezi ya shingo (Thyroid gland) ni kiungo kidogo chenye umbo la kipepeo kilichopo sehemu ya mbele ya shingo. Ingawa ni ndogo, ina kazi kubwa sana ya kuzalisha homoni zinazodhibiti kila kitu kuanzia kasi ya mapigo ya moyo, joto la mwili, hadi namna tunavyochoma kalori. Matatizo ya tezi hutokea pale tezi hii inapozalisha homoni nyingi sana (Hyperthyroidism) au kidogo sana (Hypothyroidism). Makala haya yanachambua dalili za hali hizi mbili ili kukusaidia kuelewa ishara za mwili wako.
Soma Zaidi...