picha

Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.

Posti huu inahusu zaidi malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama, ni huduma muhimu ambazo zimetolewa kwa akina Mama ili kuweza kuepuka hatari mbalimbali zinazowakumba akina Mama wakati wa ujauzito, kujifu na malezi ya watoto chini ya miaka mitano.

Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.

1.Kuangali Magonjwa yanayoweza kutokea kwa wajawazito na kuwapatia dawa mapema ili wasiweze kuwaambukiza watoto.hili ni lengo mojawapo kuhakikisha kubwa kama kuna dalili yoyote ya ugonjwa ambao unaweza kujitokeza na kuwa tayari kuwapatia dawa ili kutibu na kuepuka kuwaambukiza watoto wakati wa ujauzito, mfano wa magonjwa ni kaswende na HIV kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto na kwa asilimia tisini hili limeweza kufanikiwa katika jamii zilizo nyingi.

 

2.Kuhakikisha kwamba maendeleo ya mtoto na Mama yako vizuri. Kwa kuhakikisha kuwa Mama anakuwa na damu ya kutosha mwilini kwa kupima wingi wa damu, kumpatia Mama dawa za minyoo na kupima kama kuna Malaria na kumpatia Mama vidonge vya sp kwa kila udhulio na kumpatia Mama neti mara tu anapoanza kliniki kwa kufanya hivyo Mama anaweza kuwa na afya nzuri pamoja na mtoto wake.

 

3. Kuhakikisha kuwa Mama anajua Maana ya uzazi wa mpango ili aweze kupata watoto anaowahitaji na kuwa na distansi fulani kama ni kuzidiana miaka minne au mitano kuu kadri ya maamuzi ya wazazi wenyewe kwa kufanya hivyo watoto wanaozaliwa wanapata upendo kutoka kwa wazazi wao na pia Mama anapata nafasi ya kushiriki kwenye shughuli za kiuchumi kwa kupata mda wa kutosha badala ya kubaki katika kulea watoto wanaofuatana bila mpangilio.

 

4.Lengo lingine ni kuhakikisha kuwa  Dalili za hatari wakati wa ujauzito zinapungua kwa kuwapatia akina mama elimu kabla ya kuanza mahudhurio ili mama akiona dalili mojawapo ambayo ni ya hatari aweze kuja hospitali mara moja ili kuepuka madhara kwa mtoto, Dalili hizo ni pamoja na mtoto kushindwa kucheza, kugongwa na kichwa, kizungu Zungu, kutoka damu ukeni, kuhisi maumivu makali ya tumbo, homa kali na mabadiliko mengine ambayo siyo ya kawaida kwa Mwanamke mjamzito.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 1379

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Tofauti za ute kwa mwanamke

Posti hii inahusu zaidi tofauti mbalimbali za uke, kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo mbalimbali kwenye mwili wa binadamu kuna tofauti mbalimbali za ute kutegemea na hali iliyopo.

Soma Zaidi...
Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID

Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke

Soma Zaidi...
SABABU ZA KUTOKA KWA MIMBA (sababu za kuharibika kwa ujauzito)

Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka.

Soma Zaidi...
Dalili za kupasuka kondo la nyuma (placenta)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kupasuka kwa kondo la nyuma (plasenta) (abruptio placentae) ni tatizo lisilo la kawaida lakini kubwa la ujauzito.Kondo la nyuma (Placenta) ni muundo ambao hukua ndani ya uterasi wakati wa ujauzito ili kumlisha mtoto ana

Soma Zaidi...
Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa Mama

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.

Soma Zaidi...