picha

Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.

Posti huu inahusu zaidi malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama, ni huduma muhimu ambazo zimetolewa kwa akina Mama ili kuweza kuepuka hatari mbalimbali zinazowakumba akina Mama wakati wa ujauzito, kujifu na malezi ya watoto chini ya miaka mitano.

Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.

1.Kuangali Magonjwa yanayoweza kutokea kwa wajawazito na kuwapatia dawa mapema ili wasiweze kuwaambukiza watoto.hili ni lengo mojawapo kuhakikisha kubwa kama kuna dalili yoyote ya ugonjwa ambao unaweza kujitokeza na kuwa tayari kuwapatia dawa ili kutibu na kuepuka kuwaambukiza watoto wakati wa ujauzito, mfano wa magonjwa ni kaswende na HIV kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto na kwa asilimia tisini hili limeweza kufanikiwa katika jamii zilizo nyingi.

 

2.Kuhakikisha kwamba maendeleo ya mtoto na Mama yako vizuri. Kwa kuhakikisha kuwa Mama anakuwa na damu ya kutosha mwilini kwa kupima wingi wa damu, kumpatia Mama dawa za minyoo na kupima kama kuna Malaria na kumpatia Mama vidonge vya sp kwa kila udhulio na kumpatia Mama neti mara tu anapoanza kliniki kwa kufanya hivyo Mama anaweza kuwa na afya nzuri pamoja na mtoto wake.

 

3. Kuhakikisha kuwa Mama anajua Maana ya uzazi wa mpango ili aweze kupata watoto anaowahitaji na kuwa na distansi fulani kama ni kuzidiana miaka minne au mitano kuu kadri ya maamuzi ya wazazi wenyewe kwa kufanya hivyo watoto wanaozaliwa wanapata upendo kutoka kwa wazazi wao na pia Mama anapata nafasi ya kushiriki kwenye shughuli za kiuchumi kwa kupata mda wa kutosha badala ya kubaki katika kulea watoto wanaofuatana bila mpangilio.

 

4.Lengo lingine ni kuhakikisha kuwa  Dalili za hatari wakati wa ujauzito zinapungua kwa kuwapatia akina mama elimu kabla ya kuanza mahudhurio ili mama akiona dalili mojawapo ambayo ni ya hatari aweze kuja hospitali mara moja ili kuepuka madhara kwa mtoto, Dalili hizo ni pamoja na mtoto kushindwa kucheza, kugongwa na kichwa, kizungu Zungu, kutoka damu ukeni, kuhisi maumivu makali ya tumbo, homa kali na mabadiliko mengine ambayo siyo ya kawaida kwa Mwanamke mjamzito.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/02/08/Tuesday - 08:21:00 am Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1270

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 web hosting    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Madhara ya fangasi ukeni.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi ukeni, madhara mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo mtu hakutibiwa fangasi mapema.

Soma Zaidi...
Sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, hili ni tatizo ambalo uwapata akina Mama wengi wanapomaliza kujifungua kwa hiyo tutaweza kuziona sababu zinazosababishwa na tatizo hili.

Soma Zaidi...
Huduma kwa mama mwenye mimba Inayotishia kutoka.

Post hii inahusu zaidi huduma ambayo Mama anapaswa kutolewa pindi mimba inapotishia kutoka huduma hii utolewa kulingana na Dalili tulizoziona zinazohusiana na mimba kutishia kutoka.

Soma Zaidi...
Dalili 10 za kukaribia kujifungua pamoja na uchungu wa kujifungua

Download Kitabu cha elimu ya Ujauzito na malezi ya mimba.

Soma Zaidi...
Namna ya kutunza uke

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke.

Soma Zaidi...
UTI na ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI kwa wajawazito

Soma Zaidi...
Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.

Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n

Soma Zaidi...
Fahamu dalili za mapacha walio unganishwa

Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa fetusi mbili zitakua kutoka kwa kiinitete hiki, zitabaki zimeunganishwa mar

Soma Zaidi...