Malengo ya kutibu ukoma
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kutibu ukoma, ni malengo ambayo yamewekwa na wizara ya afya ili kuweza kutokomeza ukoma kwenye jamii
Malengo ya kutibu ugonjwa wa ukoma.
1.Tunajua kabisa ukoma ni Ugonjwa ambao ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye miguu na mikono na mara nyingi uondoa vidole vya kwenye miguu na mikono na mgonjwa huyo anakuwa hasikii maumivu ila uona kidole kinaondoka kwa sababu wadudu wanaharibu mfumo wa Neva system na kumfanya mgonjwa hasisikie maumivu wakati vidole vinapokuwa vinadondoka, kwa hiyo malengo ni kama ifuatavyo.
2.Kuzuia kuaribika kwa nevu na tisu nyingine kwenye mwili wa binadamu, kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria kwenye mwili usababisha nevu kuaribika na kuaribika kwa tishu kwa hiyo dawa mbalimbali zimeweza kupatikana na kuweza kupunguza ugonjwa huu kwa sasa ni Watu wachache ambao wanapatwa na ugonjwa kama huu kwa sababu ya kuwepo kwa dawa.
3. Kuzuia ugonjwa huu kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Tunajua kubwa ugonjwa huu una tabia ya kusambaa kwa hiyo ikiwa kwenye familia amepata mtu mmoja na kama haujatibiwa anaweza kumwambikiza mtu mwingine na kusababisha kuwepo kwenye familia na kwa jamii ambazo zina imani potovu wanaweza kusema kuwa ni Ugonjwa wa familia kumbe ni kwa sababu ya kutotibu ugonjwa huu kwa hiyo jamii inapaswa kujua na kutibu ugonjwa huu mapema kabla haujaanza kusambaa.
4.Kutokomeza kabisa ugonjwa huu.
Lengo kuu la afya ni kuhakikisha kwamba ugonjwa huu inatokomezwa kwanza kwa kutambua mazingira ambapo Ugonjwa huu upo kwa kiasi kikubwa, kutoa elimu hasa vijijini ili kutowatenga na kuwafukuza majumbani mwao wagonjwa wa ukoma, kuihakikishia jamii kuwa ugonjwa huu unatibika na pia kutibu ugonjwa huu kwa dawa zilizopendekezwa, kwa kufanya hivyo ugonjwa huu utapungua.
5.Kws hiyo mpaka sasa kwenye jamii ugonjwa huu umepungua kwa kiwango kikubwa mno kwa hiyo elimu inapaswa kuendelea kutolewa ili kuweza kutokomeza kabisa ugonjwa huu na inawezekana ukatokomezwa kwa hiyo tujue kuwa ugonjwa huu upo na unatibika na dawa zipo na wengi wamepona
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 ai web app 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Huduma ya kwanza kwa mwenye jeraha linalotoa damu
Posti inahusu huduma ya kwanza kwa mwenye jeraha linalotoa damu.huduma ya kwanza Ni kumsaidia mtu alie pata jeraha au ajali kabla hajamwona dactari au kufika hospitalinia.
Soma Zaidi...Namna ya kujikinga na kifua kikuu
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia au kujikinga na kifua kikuu, hizi ni njia ambazo utumika ili kujikinga na kifua kikuu
Soma Zaidi...Kumsaidia mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote machoni
Posti hii inahusu hasa jinsi uchafu, wadudu na vitu vingine vinavyoweza kuingia machoni.macho ni mojawapo ya milango mitano ya fahamu ambapo kazi yake ni kuona.
Soma Zaidi...Mambo yanayochangia Ili dawa kuingia kwenye damu vizuri
Post hii inahusu zaidi mambo yanayochangia Ili dawa iingie vizuri kwenye damu, na mambo yanayoweza kusababisha dawa kuingia au kutoingia vizuri kwenye damu.
Soma Zaidi...Athari za mkojo mwilini.
Posti hii inahusu zaidi athari za mkojo mwilini, kwa kawaida tunafahamu kwamba mkojo ni matokeo ya mkusanyiko wa uchafu wa maji maji yanayokusanyika kutoka mwilini ikiwa mkojo umebaki mwilini usababisha madhara mbalimbali kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...