picha

Malengo ya kutibu ukoma

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kutibu ukoma, ni malengo ambayo yamewekwa na wizara ya afya ili kuweza kutokomeza ukoma kwenye jamii

Malengo ya kutibu ugonjwa wa ukoma.

1.Tunajua kabisa ukoma ni Ugonjwa ambao ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye miguu na mikono na mara nyingi uondoa vidole vya kwenye miguu na mikono na mgonjwa huyo anakuwa hasikii maumivu ila uona kidole kinaondoka kwa sababu wadudu wanaharibu mfumo wa Neva system na kumfanya mgonjwa hasisikie maumivu wakati vidole vinapokuwa vinadondoka, kwa hiyo malengo ni kama ifuatavyo.

 

2.Kuzuia kuaribika kwa nevu na tisu nyingine kwenye mwili wa binadamu, kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria kwenye mwili usababisha nevu kuaribika na kuaribika kwa tishu kwa hiyo dawa mbalimbali zimeweza kupatikana na kuweza kupunguza ugonjwa huu kwa sasa ni Watu wachache ambao wanapatwa na ugonjwa kama huu kwa sababu ya kuwepo kwa dawa.

 

3. Kuzuia ugonjwa huu kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Tunajua kubwa ugonjwa huu una tabia ya kusambaa kwa hiyo ikiwa kwenye familia amepata mtu mmoja na kama haujatibiwa anaweza kumwambikiza mtu mwingine na kusababisha kuwepo kwenye familia na kwa jamii ambazo zina imani potovu wanaweza kusema kuwa ni Ugonjwa wa familia kumbe ni kwa sababu ya kutotibu ugonjwa huu kwa hiyo jamii inapaswa kujua na kutibu ugonjwa huu mapema kabla haujaanza kusambaa.

 

4.Kutokomeza kabisa ugonjwa huu.

Lengo kuu la afya ni kuhakikisha kwamba ugonjwa huu inatokomezwa kwanza kwa kutambua mazingira ambapo Ugonjwa huu upo kwa kiasi kikubwa, kutoa elimu hasa vijijini ili kutowatenga na kuwafukuza majumbani mwao wagonjwa wa ukoma, kuihakikishia jamii kuwa ugonjwa huu unatibika na pia kutibu ugonjwa huu kwa dawa zilizopendekezwa, kwa kufanya hivyo ugonjwa huu utapungua.

 

5.Kws hiyo mpaka sasa kwenye jamii ugonjwa huu umepungua kwa kiwango kikubwa mno kwa hiyo elimu inapaswa kuendelea kutolewa ili kuweza kutokomeza kabisa ugonjwa huu na inawezekana ukatokomezwa kwa hiyo tujue kuwa ugonjwa huu upo na unatibika na dawa zipo na wengi wamepona

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1613

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰4 ai web app     πŸ‘‰5 web hosting     πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Huduma ya kwanza kwa mtu aliyeng,area na wadudu

Posti hii inahusu zaidi huduma ya kwanza kwa mtu aliyengatwa na wadudu. Wadudu ni viumbe vidogo ambavyo hukaa sehemu mbalimbali kama vile kwenye miti na sehemu kama hizo

Soma Zaidi...
Njia za kukabiliana na minyoo

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na minyoo

Soma Zaidi...
Kushiriki ngono na mtu aliye na vvu na ukimwi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kushiriki-ngono-na-mtu-aliye-na-vvu-na-ukimwi

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kulingana na tatizo

Posti hii inahusu sana mambo ya huduma ya kwanza ambayo huduma ya kwanza inapatikana au inatolewa na mtu yeyote katika jamii .

Soma Zaidi...
Mbinu za kuponyesha majeraha

Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo hutumika kuponyesha majeraha kwa haraka zaidi,tunajua majereha utokana na kupona kwa vile vidonda au kupona kwa sehemu ambayo imekuwa na majeraha kwa hiyo ili kuponyesha majeraha hayo tunapaswa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu.

Soma Zaidi...