picha

Malengo ya kutibu ukoma

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kutibu ukoma, ni malengo ambayo yamewekwa na wizara ya afya ili kuweza kutokomeza ukoma kwenye jamii

Malengo ya kutibu ugonjwa wa ukoma.

1.Tunajua kabisa ukoma ni Ugonjwa ambao ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye miguu na mikono na mara nyingi uondoa vidole vya kwenye miguu na mikono na mgonjwa huyo anakuwa hasikii maumivu ila uona kidole kinaondoka kwa sababu wadudu wanaharibu mfumo wa Neva system na kumfanya mgonjwa hasisikie maumivu wakati vidole vinapokuwa vinadondoka, kwa hiyo malengo ni kama ifuatavyo.

 

2.Kuzuia kuaribika kwa nevu na tisu nyingine kwenye mwili wa binadamu, kwa sababu ya kuwepo kwa bakteria kwenye mwili usababisha nevu kuaribika na kuaribika kwa tishu kwa hiyo dawa mbalimbali zimeweza kupatikana na kuweza kupunguza ugonjwa huu kwa sasa ni Watu wachache ambao wanapatwa na ugonjwa kama huu kwa sababu ya kuwepo kwa dawa.

 

3. Kuzuia ugonjwa huu kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Tunajua kubwa ugonjwa huu una tabia ya kusambaa kwa hiyo ikiwa kwenye familia amepata mtu mmoja na kama haujatibiwa anaweza kumwambikiza mtu mwingine na kusababisha kuwepo kwenye familia na kwa jamii ambazo zina imani potovu wanaweza kusema kuwa ni Ugonjwa wa familia kumbe ni kwa sababu ya kutotibu ugonjwa huu kwa hiyo jamii inapaswa kujua na kutibu ugonjwa huu mapema kabla haujaanza kusambaa.

 

4.Kutokomeza kabisa ugonjwa huu.

Lengo kuu la afya ni kuhakikisha kwamba ugonjwa huu inatokomezwa kwanza kwa kutambua mazingira ambapo Ugonjwa huu upo kwa kiasi kikubwa, kutoa elimu hasa vijijini ili kutowatenga na kuwafukuza majumbani mwao wagonjwa wa ukoma, kuihakikishia jamii kuwa ugonjwa huu unatibika na pia kutibu ugonjwa huu kwa dawa zilizopendekezwa, kwa kufanya hivyo ugonjwa huu utapungua.

 

5.Kws hiyo mpaka sasa kwenye jamii ugonjwa huu umepungua kwa kiwango kikubwa mno kwa hiyo elimu inapaswa kuendelea kutolewa ili kuweza kutokomeza kabisa ugonjwa huu na inawezekana ukatokomezwa kwa hiyo tujue kuwa ugonjwa huu upo na unatibika na dawa zipo na wengi wamepona

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1567

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Huwezi kuambukizwa Ukimwi kwa mambo yafuatayo

Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k

Soma Zaidi...
Utaratibu wa lishe kwa vijana

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa vijana

Soma Zaidi...
Sababu za zinazosababisha kuwepo kwa vidonda

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa vidonda, kwa sababu tunaona vidonda vinashambulia sehemu mbalimbali za mwili ila tunakuwa hatuna sababu kwa hiyo zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa vidonda.

Soma Zaidi...
Mkojo wa kawaida

Posti hii inahusu zaidi mkojo wa kawaida kwa kila mwanadamu na unavyopaswakuwa, mkojo wa kawaida kwa binadamu huwa na sifa zifuatazo.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa aliyepatwa na presha ya kushuka

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na presha ya kushuka

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Soma Zaidi...