picha

Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa

Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut

Mambo anayopasa kufanyiwa maiti wa kiislami

Mambo yanayostahiki kufanyiwa maiti ya Muislamu
Mambo yaliyo faradhi kufanyiwa maiti ya Muislamu ni manne yafu atayo:
(1)Kuoshwa.
(2)Kuvikwa sanda (kukafiniwa).
(3)Kuswaliwa.
(4)Kuzikwa.

 


Pamoja na haya manne kuna mambo mengine mengi yanayotakiwa afanyiwe Muislamu anayekaribia kufa na aliyekufa kama alivyotuelekeza Mtume (s.a.w). Hivyo, katika kitabu hiki tumeeleza mambo yote ya msingi yanayostahiki afanyiwe Muislamu pale anapokaribia kufa mpaka baada ya kuzikwa.
Mambo muhimu anayofanyiwa Muislamu anayekaribia Kufa.

 


Mauti ni jambo la lazima sana kumtokea mwanaadamu na viumbe vyote na huingia bila taarifa wakati wowote na mahali popote kama anavyotufahamisha Allah (s.w):

 

Popote mlipo mauti yatakufikieni, na hata mkiwa katika ngome madhubuti...” (4:78).

 


Kila nafsi ita onja ma uti. Na bila s haka m tapew a ujira w enu kam ili s iku ya Kiyama. Na aliyewekwa mbali na moto na akaingizwa Peponi, basi amefuzu (amefaulu kweli kweli). Na maisha ya dunia (hii) si kitu ila ni starehe idanganyayo (watu). (3:185).

 


Kutokana na ukweli huu ni jambo la busara mno kwa mwanaadamu mwenye akili timamu kujiandaa kukabili mauti wakati wowote na popote atakapokuwa. Ni kweli kuwa maisha ya ulimwengu yamejaa hadaa lakini hatuna budi kukumbuka kuwa maisha yote ni mtihani kwetu na Muumba wetu anatuchunga barabara na kudhibiti tuyatendayo katika kila pumzi ya maisha yetu. Kumbukumbu ya ukweli huu pamoja na kukikumbuka kifo katika kila sekunde ya maisha ndiyo nguvu pekee ya kumsukuma mja kwenye maisha ya wema anayoridhia Allah (s.w). Kifo ni tukio la lazima lisiloepukika kwa kila kiumbe. Hatuna budi kukifanya kifo kitu cha kawaida na kujiandaa kwacho badala ya kufanya zoezi la kukikimbia jambo ambalo ni muhali.

 


Mtu anapokaribia kufa na baada ya kufa huwa, pamoja na ujanja wake wote na vipaji vyake vyote alivyokuwa navyo, hajimudu kwa chochote na kwa hiyo anahitajia msaada wa kila jambo.

 


Hivyo Uislamu unatufundisha kuwa mtu anayekaribia kufa tumfanyie yafuatayo:
1. Kumuogesha, kumpigisha mswaki na kumpaka manukato iwapo kuna uwezekano.
2. Kumlaza kwa ubavu wa kulia na kumuelekeza Qibla kama kuna uwezekano. Kama hivi haiwezekani mgonjwa alazwe chali na uso wake unyanyuliwe kiasi cha kuelekea Qibla
3. Kumpa maji ya kunywa.

 

4. Kutamka kalima ya Laailaahaillallah bila ya kumuashiria kuwa naye atamke. Lengo la kumtamkia kalima hii ya Tawhiid ni kumkumbusha ili naye aweze kutamka kama ni mtu aliyeishi maisha yote kulingana na kalima hiyo. Kumtamkia kalima Muislamu anayekaribia kufa ni agizo la Mtume (s.a.w):

 


Abu Said na Abu Hurairah (r.a)wamesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Wasomeeni watu wenu wanaokaribia kufa:
“Hapana mola ila Allah”

 


Pia Mu’az bin Jabal amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema:
Yule ambaye maneno yake ya mw isho yatakuwa: (Hapana mola ila Allah) ataingia Peponi. (Abu Daud).

 


Kutokana na Hadithi hii haitakuwa rahisi kwa mtu wa motoni kutamka kalima hii bali ataitamka tu yule aliyeishi maisha yake yote kulingana na kalima hii. Kwa mtu mwema kuitamka kalima hii kunampa maliwazo kuwa amali yake njema imetakabaliwa. Kutamka huku si lazima kuwe kwa wazi. Kutamka kimoyo moyo tu kunatosha, japo ni vizuri kuibanisha kwa ulimi iwapo ipo fursa.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/08/15/Monday - 06:27:22 pm Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2270

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 ai web app    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya swala

Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini

Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi

Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu.

Soma Zaidi...
Aina za Najisi na twahara katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha aina za najis. Pia utajifunza aina za twahara katika uislamu

Soma Zaidi...
Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa

Maana ya TalakaTalaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili.

Soma Zaidi...
Ni zipi najisi katika uislamu

Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.

Soma Zaidi...
Hukumu ya Talaka kabla ya kufanya jimai

Talaka Kabla ya Jimai:Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa.

Soma Zaidi...
Funga ya ramadhan na nyinginezo

Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...