Masharti ya kukubaliwa kwa dua
Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua.
MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.
1.kuchunga adabu za dua kama zilivyotajwa hapo juu.
2.Kuwa twahara nje na ndani. Yaani kujiepusha na mambo maovu na machafu ya siri na yasiyo ya siri. Amesema Mtume صلّي الله عليه وسلّم “hakika Allah ni mzuri na anapenda (vitu) vizuri.…”. (amepekea Bukhari na Muslim) Hivyo mtu anatakiwa ahakikishe ni mzuri ndani na nje.
3.kujiweka mbali na yaliyo haramu yote, na kujiepusha kula na kunywa bya haramu au kuvaa vilivyo haramu. Amesema Mtume صلّي الله عليه وسلّم “ukitaka dua maombi yako basi kifanye kizuri chakula chako (kisiwe cha haramu) “ (amepekea Bukhari na Muslim). Na pia katika hadithi ndefu iliyo sahihi katika kuwa mtume anashangaa mtu ambaye chakula chake haramu, kinywaji chake haramu, a mavazi yake haramu. Isitoshe mtu huyu amechafuka na manywele yapo timtim. Vipi atajibiwa dua yake mtu huyu. (amepekea Bukhari na Muslim). 4.Kuzingatia nyakati ambazo dua hujibiwa. Tutaziona hapo mbele.
5.Sifa ya dua yenyewe. Tutaona dua zenye sifa ya kujibiwa.
6.Hali inayozunguruka dua. Tutaona hali ambazo dua hujibiwa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 web hosting 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Hadithi Muhimu Kuhusu Ndoa Katika Uislamu
Ndoa katika Uislamu ni mkataba mtakatifu (mithaqan ghaliza) unaounganisha watu wawili kwa lengo la kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu, utulivu wa nafsi, na kuendeleza kizazi. Makala hii inachambua Hadithi muhimu za Mtume Muhammad (S.A.W) zinazotoa mwongozo kuhusu vigezo vya kuchagua mwenzi, haki za wanandoa, na umuhimu wa kuhifadhi mahusiano haya kwa upendo na busara.
Soma Zaidi...Darsa 5: Kujiepusha na tabia za unafiki na kutimiza ahadi
Katika Darsa hii tutajifnza kuhusu kujiepusha na tabia za unafiki na kitimiza ahadi.
Soma Zaidi...Dars 2: Salamu inaleta mapenzi.
Katika darsa hii tutakwenda kujifunza maneno ya Mtume kuhusu salamu kama chanzo cha kuleta upendo baina ya watu.
Soma Zaidi...