Maswali juu ya Nguzo za uislamu

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Zoezi la 4.

(a)  Ni upi mtazamo wa Uislamu juu ya maada ya ibada?

(b)  Ni lipi malengo ya ibada maalumu?

(a)  Swala katika Uislamu ina umuhimu gani?

(b)  Kwa ushahidi wa aya ainisha lengo kuu la swala.

(c)  Bainisha jinsi lengo la swala linavofikiwa kwa mwenye kuswali.

(a)  Dhihirisha matunda ya kusimamisha ibada ya swala kikamilifu.

(b)  Tofautisha baina ya kuswali na kusiamamisha swala.

Kwa hakika swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mwenye kuswali na mambo machafu na maovu (29:45).

Toa sababu tano ni kwa nini waislamu pamoja na kuswali kwao mara tano kwa siku hawajapata matunda ya swala zao?

 

(a)  Eleza maana ya zakat kilugha na kisheria.

(b)  Bainisha nafasi ya Zakat katika Uislamu.

(c)  Fafanua lengo la Zakat na jinsi linavyofikiwa.

Pamoja na waislamu wachache kutoa Zakat, lakini matunda yake hayaonekani katika jamii.  

Bainisha sababu zinazopelekea kukosekana matunda ya Zakat ndani ya jamii.

(a)  Eleza maana ya swaumu kilugha na kisheria.

(b)  Ni upi umuhimu na nafasi ya funga kwa muislamu?

Kwa ushahidi wa aya, bainisha lengo la funga na onesha jinsi linavyofikiwa na mfungaji.

(a)  Onesha zinazopatikana kutokana na funga ya mwezi wa Ramadha.

(b) Mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa wale waliokuwa kabla yenu (2:183).

Toa sababu zinazoonyesha funga ya mwezi wa Ramadhan kufaradhishwa katika mwezi huo.

 

Wengi wafungao mwezi wa Ramadhan hawafikii malengo ya fungo zao. Unafikiri ni kwa nini?

 

(a)  Ni ipi maana ya Hijja kilugha na kisheria.

(b)  Hijja ni ibada ya muda maalumu. Fafanua miezi ya Hijjah na tarehe ambayo ibada za Hijja huanza rasmi huko Makkah.

 

Toa mafunzo yatokanayo na vitendo vya ibada ya Hijjah vifuatavyo:

  (i)  Tawafu   (ii)  Sai  (iii)  Kisimamo cha Arafa  (iv)  Kupiga kambi Mina 

  (v)  Kutupa mawe  (vi)  Kuchinja mnyama.

 

(a) Ni lipi lengo kuu la ibada ya Hijjah au Umrah?

(b) Bainisha sababu tano, pamoja na waislamu kukusanyika mamilioni kila mwaka katika mji wa Makkah kwa ajili ya Hijjah, bado matunda yake hayaonekani katika jamii.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/01/18/Tuesday - 07:28:30 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1442

Post zifazofanana:-

Dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU
Somo hili linakwenda kukuletea dawa ya kuzuia kuathirika kwa watu walio hatarini kupata VVU Soma Zaidi...

Historia ya bi Khadija na familia yake na chanzo cha utajiri wake.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake. Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo. Soma Zaidi...

Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, ni madhara ambayo yanaweza kutokea iwapo maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo hayatatibiwa kwa wakati. Soma Zaidi...

Dalili za saratani ya kibofu Cha nyongo
Saratani ya kibofu cha nyongo ni Saratani inayoanzia kwenye kibofu cha nyongo. Nyongo yako ni kiungo kidogo, chenye umbo la peari upande wa kulia wa tumbo lako, chini ya ini lako. Kibofu cha nyongo huhifadhi nyongo, Kioevu cha usaga Soma Zaidi...

Mishipa ya machozi kufunga kwa mtoto.
Posti inahusu nzaidi kufunga kwa mishipa ya machozi ya mtoto kwa kawaida mishipa ya mtoto inapaswa kufunguka baada ya mwaka mmoja lakini kwa wengine ubaki imefungwa hata baada ya mwaka mmoja na kusababisha madhara mbalimbali kwa mtoto. Soma Zaidi...

Kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren. Soma Zaidi...

Mie ni mwanamke ninamaumivu chini ya kitovu upande wa kushoto, na nikishika tumbo nahisi kitu kigumu upande huo huo wa kushoto... hii itakua ni nini?
Je unasumbuliwa na maumivuvya tumbo chini ya kitovu upande wa kushito. Post hii itakuletea sababu za maukivubhayo na nini ufanye. Soma Zaidi...

Ndoa ya Siri yafanyika
Posti hii inakwenda kukuendelezea hadithi kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

Madhara ya maambukizi kwenye tumbo
Posti hii inahusu zaidi madhara ya maambukizi kwenye tumbo,hasa pale ambapo mgonjwa hakutibiwa Soma Zaidi...

Huduma kwa mtoto mwenye matatizo ya upumuaji
Posti hii inahusu zaidi huduma kwa mtoto mwenye shida ya kupumua, mtoto kama ana shida ya kupumua tunaangalia dalili kwanza na baadaye tunaweza kutoa huduma kulingana na Dalili. Soma Zaidi...

Nini husababisha maumivu ya uume
Kama uume wako unauma ama unahisi kuwa unaunguza ama kuchoma choma, post hii imekuandalia somo hili. Soma Zaidi...