Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Zoezi la 4.
(a) Ni upi mtazamo wa Uislamu juu ya maada ya ibada?
(b) Ni lipi malengo ya ibada maalumu?
(a) Swala katika Uislamu ina umuhimu gani?
(b) Kwa ushahidi wa aya ainisha lengo kuu la swala.
(c) Bainisha jinsi lengo la swala linavofikiwa kwa mwenye kuswali.
(a) Dhihirisha matunda ya kusimamisha ibada ya swala kikamilifu.
(b) Tofautisha baina ya kuswali na kusiamamisha swala.
Kwa hakika swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mwenye kuswali na mambo machafu na maovu (29:45).
Toa sababu tano ni kwa nini waislamu pamoja na kuswali kwao mara tano kwa siku hawajapata matunda ya swala zao?
(a) Eleza maana ya zakat kilugha na kisheria.
(b) Bainisha nafasi ya Zakat katika Uislamu.
(c) Fafanua lengo la Zakat na jinsi linavyofikiwa.
Pamoja na waislamu wachache kutoa Zakat, lakini matunda yake hayaonekani katika jamii.
Bainisha sababu zinazopelekea kukosekana matunda ya Zakat ndani ya jamii.
(a) Eleza maana ya swaumu kilugha na kisheria.
(b) Ni upi umuhimu na nafasi ya funga kwa muislamu?
Kwa ushahidi wa aya, bainisha lengo la funga na onesha jinsi linavyofikiwa na mfungaji.
(a) Onesha zinazopatikana kutokana na funga ya mwezi wa Ramadha.
(b) Mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa wale waliokuwa kabla yenu (2:183).
Toa sababu zinazoonyesha funga ya mwezi wa Ramadhan kufaradhishwa katika mwezi huo.
Wengi wafungao mwezi wa Ramadhan hawafikii malengo ya fungo zao. Unafikiri ni kwa nini?
(a) Ni ipi maana ya Hijja kilugha na kisheria.
(b) Hijja ni ibada ya muda maalumu. Fafanua miezi ya Hijjah na tarehe ambayo ibada za Hijja huanza rasmi huko Makkah.
Toa mafunzo yatokanayo na vitendo vya ibada ya Hijjah vifuatavyo:
(i) Tawafu (ii) Sai (iii) Kisimamo cha Arafa (iv) Kupiga kambi Mina
(v) Kutupa mawe (vi) Kuchinja mnyama.
(a) Ni lipi lengo kuu la ibada ya Hijjah au Umrah?
(b) Bainisha sababu tano, pamoja na waislamu kukusanyika mamilioni kila mwaka katika mji wa Makkah kwa ajili ya Hijjah, bado matunda yake hayaonekani katika jamii.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowPost hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.
Soma Zaidi...Hizi ni sifa za ziada za mchumba katika uislamu. Sifa hizi wengi hawazijui ama hawazingatii.
Soma Zaidi...Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu.
Soma Zaidi...MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha kuhusu swala ya sinnah ya tawba.
Soma Zaidi...