picha

Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Zoezi la 7.

  1. (a)    Nini maana ya ‘zama za Jahiliyyah’?

(b)  Bainisha baadhi ya mambo aliyoyakuta Mtume (s.a.w) katika jamii ya waarabu wa Makkah zama za Jahiliyyah.

  1. Mji wa Makkah ni mji mkongwe na mtukufu tangu zama za Nabii Ibrahim (a.s). Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu ya utukufu wa mji wa Makkah.
  2. (a)  Bainisha sababu zilizopelekea Muhammad (s.a.w) alipokuwa mdogo   kwenda kulelewa nje ya mji wa Makkah.
    1.     Taja baadhi ya sifa au tabia za Mtume (s.a.w) alizokuwa nazo tangu utotoni zilizokuwa kama ishara ya kuandaliwa kuwa Mtume wa Allah.

 

  1. (a)  Bainisha maandalizi ya Mtume (s.a.w) kabla ya kupewa Utume (mafunzo ya Ki-Ilhamu).

(b)  Ni yapi mafunzo yatokanayo na Maandalizi ya Mtume (s.a.w) ya Ki-Ilhamu?

  1. Mtume (s.a.w) alianza kupewa mafunzo ya Ki-wahyi mara tu baada ya kuanza kumshukia sura tatu za mwanzo, (96:1-5), (73:1-10) na (74:1-7).

    Kutokana na aya hizi ainisha mafunzo yatokanayo.

  1. (a)  Ni sababu zipi za msingi ziliwafanya Maquraish wa Makkah kuupinga Ujumbe wa Qur’an?
    1. Ainisha njia na mbinu walizotumia Maquraish katika kuupinga na kuuzuia ujumbe wa Uislamu kuenea katika jamii na mafunzo yatokanayo.

 

  1. Changanua njia alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuandaa ummah wa Kiislamu Makkah kwa kutumia mikataba ya ‘Aqabah.

 

  1. Katika kuendesha harakati za kuusimamisha Uislamu, hatuna budi kuwa na mikakati madhubuti. Kwa kurejea historia ya Mtume (s.a.w) onyesha jinsi alivyotumia stretejia madhubuti wakati wa kuhama kwenda Madinah.

 

  1. ‘Hijra katika Uislamu si sawa na Ukimbizi, bali na stretejia za kuunganisha nguvu ya kuusimamisha Uislamu’. 

Kwa kutumia Hijra ya Mtume (s.a.w), mambo gani waislamu wa leo tunajifunza katika hatua za kuupigania Uislamu. 

 

**********************************************

Wabillah Tawfiiq

**********************************

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 2144

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 ai web app     👉3 web hosting     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Mitihani aliyopewa Nabii Ibrahimu kutoka kwa Allah

Tumeona katika historia yake kuwa Nabii Ibrahiim(a.

Soma Zaidi...
Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.

Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.

Soma Zaidi...
Kusilimu kwa Wachawi wa Firaun

Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as).

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake

Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s.

Soma Zaidi...