image

Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

MAUMIVU YA TUMBO WAKATI WA TENDO LA NDOA

 

Maumivu wakati wa tendo la ndoa hutokea sana na pengine ni kawaida hasa kwa wanawake. Ijapokuwa kwa wanaume sio sana. Maumivu haya yanaweza kuwa ya tumbo, ya kiuno, ama viungo vya siri yaani uume na uke. Pia maumivu haya yanaweza kutokea wakati wa tendo la ndoa ama baada.

 

Je na wewe ni katika wanaopatwa na maumivu makali wakati wa tendo la ndoa. Na je umepata kujuwa chanzo cha tatizo lako?. makala hii ni kwa ajili yako. Katika makala hii tutakwenda kuona maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.

 

Sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.1.Mkao uliotumika. Ipo baadhi ya mikao inaongeza uwezekano wa kupatwa na maumivu ya tumbo wakati wa tendo. Mikao hii ni ile ambayo inaruhusu uume kuingia ndani zaidi. Kama unasumbuliwa na tatizo hili jaribu kutumia mikao ambayo utaweza kudhibiti uingiaji wa uume.

 

2.Kama tumbo la uzazi (uterus) limeinama kidogo. Hii hutokea pale tumbo la uzazi linapolalia nyuma kidogo kuelekea kwenye shingo ya uzazi. Hali hii huwewa kupelekea maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa.

 

3.Maka una tatizo la kuota tishu zinazopaswa kuota kwenye tumbo la uzazi zikaota sehemu nyingine. Hali hii hutambulika kama endometruisis. Haki hii huweza kupelekea maumivu ya mgongo, nyonga na tumbo wakati wa tendo la ndoa. Dalili za hali hii ni pamoja na:-

 

A.Maumivu makali zaidi wakati wa tendo la ndoaB.Kupata hedhi yenye damu nyingiC.Kutokwa na damu kabla na baada ya kumaiza hedhiD.Maumivu ya tumbo

 

4.Kama ovari ina matatizo yaani inajaa maji, hali hii hutambulika kama ovarian cysts. Hii hutokea endapo juu y aovari ama ndani kunkuwa na kama vijifuko vijidogo vinajaa maji. Sasa vikiwa vidogo havinaga maumivu ila vikiwa ni vikubwa vinaweza kupelekea maumivu ya chini ya tumbo. Maumivu haya yanaweza kuwa makali zaidi wakati wa tendola ndoa. Pia mtu anaweza kupata dalili zifuatazo:-

 

A.Maumivu ya mgongo wa chini ama kwenye mapajaB.Unahisi tumbo limejaa ama kushiba, ama tumbo linakuwa zitoC.Tumbo kujaa gezi na kucheua gesi kwa mdomoni.

 

5.Kama kuna mashambulizi kwenye kibofu kitaalamu hali hii huitwa interstial cystitis. Misuli ya kwenye kibofu inashambuliwa na kuvimba na baadaye kutoa dalili kama:-A.Maumivu ya tumbo na nyongaB.Kukojoa mara kwa maraC.Kujihisi kukojoa tena punde baada ya kukojoaD.Kuvuja kwa mkojo yaani kutoka mkojo bila ya wewe kujuwa.E.Maumivu kwenye uke na mashavu ya uke (papa)

 

6.Kuwa na uvimbe kwenye tumbo la mimba kitaalamu huitwa fibroid. Huu ni uvimbe usiosabababishwa na saratani. Uvimbe huuu huweza kuleta dalili kama:-A.maumivu ya tumbo na mgongo sehemu ya chiniB.Kupata damu nyingi ya hedhi pamoja na maumivu makaliC.Maumivu wakati wa tendo la ndoaD.Kukosa choo.

 

7.Kama mtu ana maradhi ya ngono kama gonoria na chlamydia. Hapa mtu anaweza kuona dalili kama:-A.Kutokwa na uchafu ukeniB.Kutoka na harufu mbaya ukeniC.Maumivu wakati wa kukojoa na kuhisi kama unaunguwaD.Maumivu ya tumbo kwa chini pamoja na nyongaE.Maumivu na kutokwa na damu wakati wa hedhi na baada ya hedi

 

8.UTI na PID; kwa pamoja haya ni mashambuizi ya bakteria ama fangasi ama virusi. Mashambulizi haya huathiri mfumo wa uzazi hapa itakuwa na PID na endapo yatashambulia mfumo wa mkojo itakuwa ni UTI. ugonjwa wa UTI na PID huweza kusababisha maumivu wakati wa tendo la ndoa.

 

Dalili za PIDA.Maumivu makali ya nyonga wakatii wa tendo la ndoaB.Maumivu wakati wa kukojoaC.Kutokwa na damu wakati wa hedhi na baada

 

Dalili za UTIA.Maumivu ya tumbo ambayo huongezeka wakati wa tendo la ndoaB.Maumivu wakati wa kukojoaC.Kukojoa mra kwa maraD.Mkojo mchafu na wenye harufu kali.

 

9.kama kuna uvimbe katika tezi dume.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1477


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba,Ni mambo ya kuzingatia ili mama akija kubeba mimba awe mzima kimwili, ki afya na kisaikolojia na hivyo hivyo Mtoto atakayezaliwa atakuwa salama. Soma Zaidi...

Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.
Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo. Soma Zaidi...

KUWAHI KUMALIZA TENDO LA NDOA MAPEMA: kumwaga mbegu mapema
Hii ni hali inayowapata sana wanaume huwa wanamaliza hamu ya tendo la ndoa mapema kabla ya mwenza kuridhika. Soma Zaidi...

Hivi kipimo cha mimba cha mkojo baada ya kutumika Mara 1 ,hakiruhusiw tena kutumika au
Je ni kweli kupima kimoja cha mloka kinaweza kupima mimba zaidi ya mara moka? Soma Zaidi...

Habar doctor mm nahc kuwa ni mjamzito tumbo la chin ya kitovu linaniuma muda mwingine linaacha chuchu zinawasha na cku niliyokutana na mume wangu ni cku 11
Kuna uwezekano una ujauzito ila hujajijuwa, huwenda hujapata dalili zozote. Unataka kujuwa kama una ujauzito baada ya tendo la ndoa. Soma Zaidi...

Je bado unasumbuliwa na nguvu za kiume?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuondoa tatizo la nguvu za kiume Soma Zaidi...

Damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito Soma Zaidi...

Fahamu matatizo yanayowapata watoto waliozaliwa kabla ya wakati au mapema (premature)
Kuzaa kabla ya wakati ni kuzaliwa ambayo hufanyika zaidi ya wiki tatu kabla ya kuzaliwa kwa mtoto au kuzaliwa mapema ni moja ambayo hutokea kabla ya mwanzo wa wiki ya 37 ya ujauzito. Kawaida, ujauzito hudumu kama wiki 40. Soma Zaidi...

Kaka nasumbuliwa saan na tatizo la kuwasha kwenye kichwa Cha uume Sijui nifanyaje
Je kichwa cha uume wako kinawasha, na je kinatoa majimaji kwenye njia ya mkojo, una muda ganinavtatizo hili. Na je ulishiriki ngono zembe siku za hivi karibuni? Soma Zaidi...

Dalili za kujifungua hatua kwa hatua
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za kujifungua hatua kwa hatua Soma Zaidi...

Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID
Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa. Soma Zaidi...

faida za tendo ka ndoa wakati wa ujauzito
Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba Soma Zaidi...