image

Mbinu walizotumia makafiri wa kiqureish katika kuupinga uislamu makkah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.

 

-    Maqureish wa Makkah walitumia kila mbinu kuhakikisha kuwa ujumbe wa Uislamu haufiki na kukubalika katika jamii yao, miongoni ni hizi zifuatazo;

 

  1. Kumkatisha tamaa Mtume (s.a.w) na wafuasi wake.

-  Makafiri walimdhihaki Mtume (s.a.w) na waumini wachache kwa 

    kumuita majina mabaya kama; mwendawazimu, mtunga mashiri, 

    aliyepagawa na mashetani, mchawi, n.k.

 

-  Pamoja na kusimangwa huko Mtume (s.a.w) na waislamu hawakukata 

    tamaa, waliendelea kuutangaza Uislamu katika jamii yote.

 

  1. Mbinu ya Vitisho na Kumkataza Mtume (s.a.w) kuulingania Uislamu kwa kumtumia Ami yake, Abu Talib.

 

-  Wakuu wa Maquraish walimuagiza Abu Talib amkataze Muhammad 

    (mwanae) kuendelea kuutangaza Uislamu kwa kumbadilishia mtoto 

    mwingine la sivyo watamshambulia yeye na Muhammad (s.a.w).

 

-  Mbinu hii haikufanikiwa badala yake Abu Talib alimuunga mkono 

    Mtume (s.a.w) kwa kazi yake baada ya kujua msimamo wake.

 

  1. Mbinu ya Kumhonga na kumrubuni Mtume (s.a.w).

-  Maquraish walitumia diplomasia kwa kumtaka Mtume (s.a.w) aache 

    kazi ya kuutangaza Uislamu kwa kumpa kati ya vitu vifuatavyo; 

    utajiri, mwanamke mzuri, madaraka au yote kama akitaka.

 

-  Mtume (s.a.w) aliwakatalia vyote hivyo kwa kumsomea aya za Qur’an 

    (41:1-37) mjumbe aliyetumwa kazi hiyo, Utbah bin Rabi’ah.

 

  1. Mbinu ya kutaka kumlaghai Mtume (s.a.w).

-  Maqureish walimletea Mtume (s.a.w) pendekezo kuwa washirikiane 

    katika ibada kwa awamu, mwaka mmoja wamuabudu Mungu mmoja 

    kwa pamoja na mwaka unaofuatia waabudu miungu yao pamoja pia.

 

-  Hapo ndipo iliposhuka suratul-Kafiruun kuvunja pendekezo lao hilo la 

    kushiki katika ibada na Mtume akawasomea aya za Qur’an kukataa.

    Rejea Qur’an (109:1-6) na (10:15).

 

  1. Mbinu ya Kuwatesa na kuwaua Waislamu.

-  Baada ya Maqureish kuona mbinu zote zimefeli, walianza kutumia 

   nguvu na mabavu kuwatesa, kuwanyonga na kuwaua Waislamu 

   waliong’ang’ani imani yao kama akina; Bilal bin Rabbah, Sumaiyya,      

   Ammar bin Yasir na baba yake, n.k.

 

- Pamoja na mateso na mauaji, waislamu walibakia na msimamo wao  

   bila kutetereka na kukata tamaa. 

 

  1. Mbinu ya fitina, kuipinga Qur’an na kuzuia watu kukutana na Mtume (s.a.w).

-  Maquraish kwa kuhofia ujumbe wa Qur’an kuenea kwa watu, 

    walianza kuzuia watu kwenda kuonana na Mtume (s.a.w) kwa 

    kuwashawishi kuwa wasisikilize aya za Qur’an kwani ni uchawi, 

    mashairi ya Muhammad.

 

-  Walizidi kufitinisha kwa kumzuia Mtume (s.a.w) kuswali na 

    kuwaambia watu kuwa Muhammad anapinga ibada na miungu wenu, 

    lakini mbinu na ushawishi wao ulifeli pia.

   Rejea Qur’an (31:6), (41:26), (10:38), (11:13) na (96:9-19). 

 

  1. Mbinu ya kuwatenga na kila huduma ya kijamii.

-  Maquraish walizidi kuongeza mateso kwa waislamu kwa kutenga na 

    kuwafukuza Makka na kwenda kuishi katika jangwa la Shi’ab miaka 

    mitatu bila chakula wala mahusiano mengine ya kijamii.

 

-  Mbinu pia ilifeli baada ya baadhi ya Maquiesh kuona huruma kwa 

    ndugu zao waliotengwa bila sababu za msingi, hivyo wakavunja  

    mkataba wa kuwatenga.

 

  1. Mbinu ya kutaka kumuua Mtume (s.a.w).

-  Maquish waliazimia kumuua Mtume (s.a.w) na rafiki yake Abubakar 

   (r.a) walipogundua kuwa waislamu wamehamia mji wa Madinah.

 

-  Mbinu hii pia ilifeli baada ya Allah (s.w) kuwanusu katika pango yeye 

    na sahibu yake Abubakar (r.a).

    Rejea Qur’an (9:40).





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2333


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?
Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri? Soma Zaidi...

Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...

Kuangamizwa Firauni na Majeshi Yake
Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME AL-YASA’A(A.S)
Mtume Alyasa’a(a. Soma Zaidi...

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar
Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nabii Ibrahiim(a.s) Kumlingania Uislamu Baba Yake
Baada ya NabiiIbrahiim(a. Soma Zaidi...

Kuanzishwa kwa mahakama na mahakama ya Kadhi wakati wa makhalifa
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISHAQA NA YAQUB
Soma Zaidi...

Khalifa na Utungaji Sheria, na utiifu juu ya sheria na usimamiaji wa haki
Soma Zaidi...

Imam Ibn Majah na Sunan Ibn Majah
Soma Zaidi...

Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu
KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S. Soma Zaidi...