MBINU ZA KUTOA HUDUMA YA KWANZA KWA WAGONJWA WALIO NA MAJERAHA YA MACHO.


image


Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa walio na majeraha ya macho kutokana na aina mbalimbali ya jeraha


Ishara na Dalili za jeraha la jicho.


1. Kuwa na Maumivu kwenye jicho.
2. Uwekundu na uvimbe kwenye jicho.
3. Kutokuwa na uwezo wa kufungua jicho.
 4.Kuwashwa kwa jicho
5. Kupungua kwa uwezo wa kuona
6.jicho kutoa machozi.

 

  Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho.

 Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho yaliyoingiliwa na uchafu Kama vile wadudu,kijiti,n.k
1. Mwambie mgonjwa aketi chini kwenye kiti anyanyue kichwa juu aangalie mwanga.

2. Simama nyuma ya mgonjwa ili iwe rahisi kumtoa uchafu Tumia Kidole gumba , kwa upole, tenganisha kope na uchunguze kilichopo ndani ya jicho.
3. Mwambie mgonjwa aangalie kushoto, kulia, juu na chini.
4.mwagia macho maji Safi na salama.
5. Ondoa kwa kutumia pamba au kitambaa Safi ili kuondoa uchafu.


 Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa wenye majeraha ya macho yanayohusiana na kemikali iliyomwagika kwenye jicho.

1. Ondoa mgonjwa kutoka eneo hilo, funga chombo cha kemikali
2. Mwagilia jicho la mgonjwa kwa maji baridi ya bomba kwa angalau dakika 10.
3. Usiruhusu maji yaliyochafuliwa kumwagika kwenye jicho ambalo halijaathirika
4. Mwambie mgonjwa atunze jicho lisilojeruhiwa kwa sababu Kuna uwezekano wa kuambikiza jicho lingine.
5 inapaswa utambue Ni aina ganu ya kemikali imeingia jichoni.
6. Mpeleke mgonjwa hospitali kwa usimamizi zaidi.


 Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa wenye majeraha ya macho yanaliyoingiliwa na vitu vyenye ncha Kali Kama vile Pini,sindano,n.k
 1. Weka kitambaa Safi juu ya jicho lililopata jeraha.
2. Mwombe mgonjwa atunze jicho lisilojeruhiwa kwa sababu harakati hii itasababisha msogeo wa jicho lililojeruhiwa ambalo linaweza kuongezea kupata Maumivu.
4. Mpeleke mgonjwa hospitali kwa usimamizi zaidi.


 Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa wenye majeraha ya macho yanayohusiana na gesi
1. Hakikisha ulinzi wako mwenyewe kutoka kwa gesi
2. Mtoe mgonjwa kwenye Hilo eneo na kumweka sehemu yenye hewa nzuri.
3.mwambie mgonjwa kuwa atapona 
4. Mkataze mgonjwa kusugua jicho
5. Mpeleke mgonjwa hospitali kwa usimamizi zaidi



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya php    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Faida za uzazi wa mpango kwa jamii
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa jamii, tunapaswa kujua kuwa uzazi wa mpango ukitumiwa vizuri na jamii nayo inapata faida kwa hiyo zifuatazo ni faida za uzazi wa mpango kwa jamii. Soma Zaidi...

image Njia za kuzuia upele
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia upele, ni njia ambazo utumiwa Ili kupunguza tatizo la upele kwenye jamii, kwa hiyo jamii inapaswa kutumia njia hizi Ili kuweza kupambana na ugonjwa huu ambao unatibika. Soma Zaidi...

image Dondoo za afya 1-20
Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya Soma Zaidi...

image Fahamu sababu za ugonjwa unanipeleka Kuvimba kwa mishipa ya Damu
posti hii inazungumzia kuhusiana na ugonjwa wa kuvimba kwa mishipa ya damu katika mwili wako wote. Kuvimba kwa Mishipa ya Damu hujulikana Kama Behcet amboyo husababisha dalili nyingi ambazo hapo awali zinaweza kuonekana kuwa hazihusiani. Dalili na ishara za ugonjwa huu ambazo zinaweza kujumuisha vidonda vya mdomo, kuvimba kwa macho, upele wa ngozi na vidonda, na vidonda vya sehemu za siri hutofautiana kati ya mtu na mtu na huenda zikaja na kwenda zenyewe. Soma Zaidi...

image Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuzuia Malaria kwa wajawazito. Soma Zaidi...

image Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mtoto. Soma Zaidi...

image Mambo ya kuzingatia unapokuwa unatoa huduma ya kwanza
Huduma ya kwanza ni huduma inayotolewa kwa mtu yeyote aliyepata ajali au mgonjwa yeyote kabla hajapelekwa hospitalini Soma Zaidi...

image Vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo Soma Zaidi...

image Dalili za fizi kuvuja damu
Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa fizi ambapo fizi huweza kuwa na maumivu, kuambukizwa, kuvuja damu kwenye fizi na Vidonda. Soma Zaidi...

image Viungo vinavyoathiriwa na malaria
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya viungo vinavyoathiriwa na ugonjwa wa malaria Soma Zaidi...