Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho.
Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa walio na majeraha ya macho kutokana na aina mbalimbali ya jeraha
Ishara na Dalili za jeraha la jicho.
1. Kuwa na Maumivu kwenye jicho.
2. Uwekundu na uvimbe kwenye jicho.
3. Kutokuwa na uwezo wa kufungua jicho.
4.Kuwashwa kwa jicho
5. Kupungua kwa uwezo wa kuona
6.jicho kutoa machozi.
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho.
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho yaliyoingiliwa na uchafu Kama vile wadudu,kijiti,n.k
1. Mwambie mgonjwa aketi chini kwenye kiti anyanyue kichwa juu aangalie mwanga.
2. Simama nyuma ya mgonjwa ili iwe rahisi kumtoa uchafu Tumia Kidole gumba , kwa upole, tenganisha kope na uchunguze kilichopo ndani ya jicho.
3. Mwambie mgonjwa aangalie kushoto, kulia, juu na chini.
4.mwagia macho maji Safi na salama.
5. Ondoa kwa kutumia pamba au kitambaa Safi ili kuondoa uchafu.
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa wenye majeraha ya macho yanayohusiana na kemikali iliyomwagika kwenye jicho.
1. Ondoa mgonjwa kutoka eneo hilo, funga chombo cha kemikali
2. Mwagilia jicho la mgonjwa kwa maji baridi ya bomba kwa angalau dakika 10.
3. Usiruhusu maji yaliyochafuliwa kumwagika kwenye jicho ambalo halijaathirika
4. Mwambie mgonjwa atunze jicho lisilojeruhiwa kwa sababu Kuna uwezekano wa kuambikiza jicho lingine.
5 inapaswa utambue Ni aina ganu ya kemikali imeingia jichoni.
6. Mpeleke mgonjwa hospitali kwa usimamizi zaidi.
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa wenye majeraha ya macho yanaliyoingiliwa na vitu vyenye ncha Kali Kama vile Pini,sindano,n.k
1. Weka kitambaa Safi juu ya jicho lililopata jeraha.
2. Mwombe mgonjwa atunze jicho lisilojeruhiwa kwa sababu harakati hii itasababisha msogeo wa jicho lililojeruhiwa ambalo linaweza kuongezea kupata Maumivu.
4. Mpeleke mgonjwa hospitali kwa usimamizi zaidi.
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa wenye majeraha ya macho yanayohusiana na gesi
1. Hakikisha ulinzi wako mwenyewe kutoka kwa gesi
2. Mtoe mgonjwa kwenye Hilo eneo na kumweka sehemu yenye hewa nzuri.
3.mwambie mgonjwa kuwa atapona
4. Mkataze mgonjwa kusugua jicho
5. Mpeleke mgonjwa hospitali kwa usimamizi zaidi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Yajue malengo ya kusafisha vidonda.
Posti hii inahusu zaidi malengo ya kusafisha vidonda, kwa sababu Kuna watu wengine huwa wanajiuliza kwa nini nisafishe kidonda hospitalini au kwenye kituo chochote Cha afya, yafuatayo ni majibu ya kwa Nini nisafishe kidonda.
Soma Zaidi...Njia za kuzuia kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuzuia kiungulia
Soma Zaidi...Zijue faida za mate mdomoni
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa mate mdomoni, mate ni majimaji ambayo hukaa mdomoni na husaidia katika kazi mbalimbali mdomoni.
Soma Zaidi...Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyezimia
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyezimia
Soma Zaidi...Haya hayawezi kuambukiza UKIMWI
Somo hili linakwenda kukuletea Mambo ambayo hayawezi kuambukiza UKIMWI
Soma Zaidi...Jinsi ya kujikinga na U.T.I inayijirudia rudia.
Endapo U.T.I inajirudiarudia baada yavkutibiwa inawezabkuwa ikakupa mawazo mengi. Katika post hii nitakufafanulia nini ufanye.
Soma Zaidi...