picha

Minyoo Ni nini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya minyoo

MINYOO NI NINI?

Minyoo ni katika vimelea ama wadudu wanaoishi ndani ya kiumbe aliye hai. Wanaweza kuishi kwenye wanyama kama ngo’ombe, ngurue na mbuzi, pia wanaweza kuishi ndani ya binadamu. Wanajipatia mahitaji humo kama chakula, hewa na kila wanachohitaji. Wakiwa wanaishi ndani ya mwili wa kiumbe hai wanaweza kusababisha madhara makubwa sana katika afya ya mtu. Wadudu hawa kitaalamu wanatambulika kama parasitic worm.

 

 

 

Katika makala hii tutakwenda kujifunza, dalili, sababu, matibabu na njia za kupambana na minyoo katika mazingira yetu. Pia tutaona madhara ya kiafya yanayoletwa na kuishi na minyoo mwilini. Endelea kuwa nasi upate faida hii

 

 

 

Hatari ya kupata minyoo ni kubwa sana maeneo ya vijijini ama katika maeneo ambayo hali ya usafi sionzuri. Nchi zinazoendelea kama nchi za afrika ni katika maeneo ambayo yanakabil;iwa sana na minyoo kuliko nchi zilizo endelea.

 

 

 

Wataalamu wanatueleza kuwa kuna aina zaidi ya 300,000 (laki tatu) za minyoo. Na katika aina hizi kuna aina 300 (mia tatu) za minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa mwanadamu na kumuathiri kwa namna moja ama nyingine.

 

 

 

Minyoo wanazaliana kwa kutaga mayai, na mayai yao yanatofautiana ukubwa, kuna ambayo yanaonekana kwa macho na mengine ni madogo zaidi kwa kuonekana kwa macho. Kuna aina za minyoo hutaga mayai bila ya kuhitaji kuwepo kwa dume, kwani kuna minyoo ambayo ina jinsia zote kwa pamoja (hermaphroditc).

 

 

 

Minyoo huweza kutaga mayai zaidi ya mara sita kwa siku. Na idadi ya mayai yao ni kati ya mayai 3000, mpaka 700000. na mayai yao yanaweza kudumu kwa miezi mingi biala ya kufa, na yanaweza kuvumialia hali mbalimbali za joto.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2275

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰3 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Hasira za asubuhi (Morning irritability): Nini cha kufanya?

​Je, unajikuta ukiwa na hasira, msongo wa mawazo, au hali ya kutotaka kuongea na mtu yeyote kila unapoamka? Hii hali inajulikana kama "Morning Irritability." Gundua sababu zake za kisaikolojia na kibaolojia, na jifunze mikakati ya kitaalamu ya kuanza siku yako kwa utulivu, furaha, na tija zaidi.

Soma Zaidi...
VIPI VIDONDA VYA TUMBO VINATOKEA

VIPI VIDONDA VYA TUMBO VINATOKEA 1.

Soma Zaidi...
Chakula kinachosaidia kupunguza gesi tumboni.

​Gesi tumboni (bloating au flatulence) ni tatizo la kawaida linaloweza kusababisha usumbufu mkubwa na kupoteza kujiamini. Makala haya yanachunguza kwa kina vyakula bora vinavyosaidia kupunguza uzalishaji wa gesi, kuelezea sayansi nyuma ya usagaji chakula, na kutoa mikakati ya lishe kwa maisha yenye afya na utulivu wa tumbo.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za anemia ya minyoo

Posti hii inshusiana na dalili za anemia ya minyoo

Soma Zaidi...
AFYA NA MAGONJWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...