Msaada kwa Mgonjwa aliyeshindwa kupitisha mkojo.
Posti hii utokea huduma ya kwanza kwa mtu aliye na shida ya kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo,
Huduma ya kwanza kwa mtu Mwenye tatizo la kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo.
1. Muweke mgonjwa kwenye hali ya kutaka kukojoa.
Kwa kufanya hivyo tunaweza kusababisha mkojo kutoka au msaidie mgonjwa kumwekea kwenye kufaa Cha kukojolea kwa kufanya hivyo mkojo unaweza kupita na mgonjwa anaweza kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo na anaweza kuwa kawaida na kuendelea kukojoa.
2. Mpatie mgonjwa vitu vya moto vya kunywa kama vile chai ya moto, kahawa,na kufaa Cha kukojolea kiwe Cha moto.
Kwa kufanya hivyo tunaweza kusababisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo na mgonjwa anaweza kukojoa na kurudia kwenye hali ya kawaida, kwa sababu maji ya moto au vitu vya moto vinaweza kushutua mishipa ambayo inakuwa imebana na kumfanya mgonjwa akawa kawaida.
3. Mpeleke Mgonjwa kwenye bomba la maji na fungua maji kwa speed kubwa na mkojo unaweza kutoka.
Kwa kufungua maji ya bomba kwa speed kubwa mno usababisha kuamsha sehemu za kibofu Cha mkojo na kusababisha mgonjwa aweze kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu kitendo hiki ufanyiwa hasa kwa watu wale waliofanyiwa upasuaji na huwa wanaweza kukojoa kwa kawaida.
4. Mpatie mgonjwa dawa ya maumivu.
Mgonjwa anayeshindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo anapaswa kupewa dawa za maumivu kama vile parnadol, Asprini, tramadol na dawa nyingine ambazo zote za maumivu kwa sabat labda kitendo Cha kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo ni kwa sababu ya maumivu kwa pale alipofanyiwa upasuaji kwa kumpatia dawa ya maumivu subiri kwa mda na uangalie kama anaweza kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo na kuendelea na maisha yake ya kawaida.
5. Kama mgonjwa amepewa kila njia na mkojo ukashindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo, mgonjwa anaweza kuwekewa milija wa kupitisha mkojo ambao kwa kitaamu huitwa catheter hiki ni kifaa ambacho upitishwa mkojo Moja kwa Moja kutoka kwenye kibofu Cha mkojo na kuingia kwenye sehemu ambayo imeandaliwa na kisha kumwaga. Kwa hiyo njia hii utumika ikiwa zote zimeshindikana.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.
Soma Zaidi...Dalili na ishara za Ugonjwa wa kuambukiza.
Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe
Soma Zaidi...tatizo la kushindwa kujaza misuli ya mwilini na kusinyaa kwa misuli mwilini
Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kusinyaa kwa Misuli. Ni maradhi yanayopelekea uzalishwaji hafifu wa misuli, hivyo kupelekea misuli kukosa protini, kushunwa kukuwa na kusinyaa.
Soma Zaidi...Je minyoo inaweza kusababisha mmeng'enyo wa chakula kuwa dhaifu?
Mfumo wa chakula unaweza kuwa dhaifu kwa sababu nyingi ikiwepo vyakula vyenyewe, vinywaji ama maradhi. Vipi kuhusu minyoo? Endelea na makala hii utajifunza zaidi.
Soma Zaidi...Yaani minasumbuliwa na mgongo kuuma pia kuchoka mgongo na homa zisizo isha
Maumivu ya mgongo yanaweza kuwa ni dalili inayoonyesha tatizo fulani la kiafya ikiwemo magonjwa au majeraha.
Soma Zaidi...