image

Mtazamo wa makafiri juu ya dini

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Mtazamo wa Makafiri juu ya Dini.

Mtazamo wa kikafiri juu ya dini uko katika sehemu kuu tatu zifuatazo;

Maana ya dini.

Chimbuko, Asili au Chanzo cha dini.

Kazi ya dini katika jamii.

 

 Maana ya dini.

Ni imani juu ya kuwepo Mungu Muumba Muweza na Mwenye nguvu juu ya kitu.

Rejea tafsiri ya neno Religion katika Kamusi ya Kiingereza.

 

Belief in the existence of a supernatural ruling power the creator …..”

Tafsiri: 

Dini ni imani ya kuwepo Mungu Muumba aliyemuweza na mwenye nguvu..

 

Chimbuko, Chanzo au Asili ya dini.

Makafiri wanadai kuwa chimbuko la dini linatokana na mawazo na fikra finyu za mwanaadamu alipokuwa katika maisha ya ujima (primitive age).

 

Dini ni fikra na dhana alizoibua mwanaadamu baada ya kushindwa kutatua matatizo ya kijamii, uchumi, siasa, n.k.

 

Dini ni dhana iliyoibuliwa na mwanaadamu kutokana na uduni wa maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Rejea kitabu cha Kafiri, F. Angels kiitwacho Anti-Duhring

 

“Religion arose from primitive conceptions of men

Tafsiri:

Dini imeibuka kutokana na ujima (uduni) wa mawazo ya mwanaadamu

 

           (c) Kazi ya dini katika jamii.

Ukirejea historia ya Ulaya na nchi za Magharibi, Kanisa kama dini lilitumika kwa kazi zifuatazo;

 

- Ni chombo kinacholeta unyonyaji, ukandamizaji na dhuluma katika jamii.

Rejea Quran (28:4).

 

Ni chombo cha kuleta matabaka na ubaguzi kati ya viongozi (mabwana) na waongozwa, matajiri na masikini katika jamii.  

 

Pia dini inaaminika kuwa ni chombo cha kulinda na kutetea maslahi ya watawala kupitia mafundisho yake.

 

Dini inatumika kama chombo cha kuchuma na kujilimbikizia mali kwa wakuu (viongozi) wake kwa kuwatumia wafuasi wake.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2019


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?
Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu) Soma Zaidi...

NGUZO ZA IMAN
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...

Shahada mbili
Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku. Soma Zaidi...

Mtazamo wa uislamu juu ya dini
Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini. Soma Zaidi...

Nafsi ya mwanaadamu
Soma Zaidi...

“Allah (s.w) humwingiza katika rahma zake amtakaye na kumwacha kupotea amtakaye”
Soma Zaidi...

Mgawanyiko wa Elimu kwa mtazamo wa kikafiri
Kwa mtazamo wa kikafiri elimu imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Elimu ya dunia na Elimu ya akhera. Soma Zaidi...

Maamrisho ya kushikamana nayo
Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s. Soma Zaidi...

Athari za vita vya Uhud
Vita vya uhudi viliweza kuleta athari nyingi. Post hii itakuletea athari baadhi za vita hivyo. Soma Zaidi...

KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s. Soma Zaidi...

Muhtasari wa madili malezi ya jamii kama ilivyobainishwa katika Qur-an
(v)Kuwaombea dua wazazi. Soma Zaidi...

Humtegemea Mwenyezi Mungu peke yake
Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu. Soma Zaidi...