Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Mtazamo wa Makafiri juu ya Dini.
Mtazamo wa kikafiri juu ya dini uko katika sehemu kuu tatu zifuatazo;
Maana ya dini.
Chimbuko, Asili au Chanzo cha dini.
Kazi ya dini katika jamii.
Maana ya dini.
Ni imani juu ya kuwepo Mungu Muumba Muweza na Mwenye nguvu juu ya kitu.
Rejea tafsiri ya neno Religion katika Kamusi ya Kiingereza.
Belief in the existence of a supernatural ruling power the creator …..”
Tafsiri:
Dini ni imani ya kuwepo Mungu Muumba aliyemuweza na mwenye nguvu..
Chimbuko, Chanzo au Asili ya dini.
Makafiri wanadai kuwa chimbuko la dini linatokana na mawazo na fikra finyu za mwanaadamu alipokuwa katika maisha ya ujima (primitive age).
Dini ni fikra na dhana alizoibua mwanaadamu baada ya kushindwa kutatua matatizo ya kijamii, uchumi, siasa, n.k.
Dini ni dhana iliyoibuliwa na mwanaadamu kutokana na uduni wa maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Rejea kitabu cha Kafiri, F. Angels kiitwacho Anti-Duhring
“Religion arose from primitive conceptions of men
Tafsiri:
Dini imeibuka kutokana na ujima (uduni) wa mawazo ya mwanaadamu
(c) Kazi ya dini katika jamii.
Ukirejea historia ya Ulaya na nchi za Magharibi, Kanisa kama dini lilitumika kwa kazi zifuatazo;
- Ni chombo kinacholeta unyonyaji, ukandamizaji na dhuluma katika jamii.
Rejea Quran (28:4).
Ni chombo cha kuleta matabaka na ubaguzi kati ya viongozi (mabwana) na waongozwa, matajiri na masikini katika jamii.
Pia dini inaaminika kuwa ni chombo cha kulinda na kutetea maslahi ya watawala kupitia mafundisho yake.
Dini inatumika kama chombo cha kuchuma na kujilimbikizia mali kwa wakuu (viongozi) wake kwa kuwatumia wafuasi wake.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu).
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti.
Soma Zaidi...Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:“Kwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere..
Soma Zaidi...Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.
Soma Zaidi...“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilicho kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele).
Soma Zaidi...