Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini.
Mtoto wa Tajiri na maskini .
1.watoto hawa walikuwa majirani, na walikuwa wanasoma shule moja , kila siku mtoto wa tajiri alikuwa anaamshwa anaoshwa, anasaidiwa kupiga mswaki anavalishwa anaangaliwa cha na baadae anawekwa kwenye gari mpaka shuleni na kufungiwa juice na maanda kwenye begi kwa ajili ya kula baadae , na mda wa saa nne alikuwa anafuatwa shule anaenda kunywa maziwa nyumbani na kurudishwa kuendelea na masomo na baada ya kumaliza masomo mtoto alifuatwa kwa gari mpaka nyumbani baada ya kufika nyumbani alibadilisha nguo akala chakula alichokuwa ameagizwa kupokwe mara nyingi zilikuwa ni Chipsi.
2. Baada ya kumaliza kula aliwekewa tv akaanza kuangalia katuni na michezo mingine na alipokuwa anachoka anaenda kuogelea kwenye swimming pool na baadaye alikula kila alichopenda kula na baadae alikwenda kulala hata bila kukumbushwa kufanya home work hiyo ndiyo iliyokuwa ratiba ya mtoto wa tajiri.
3. Kama nilivyotangulia kusema kwamba palikuwepo pia mtoto wa maskini, yeye ratiba yake ilikuwa tofauti kabisa na mtoto wa tajiri yeye kila siku alijiamsha mwenyewe akanawa uso akajipaka sabini kwa sababu mafuta yalikuwa shida ,akasafisha nyumba kwa kufagia huku akisubiria chai aliyoweka kwenye mafiga akimaliza kufagia anakunywa chai bila sukari pamoja na kiporo kidogo cha ugali kilichobaki na akikumbuka kumbakizia mdogo wake ambaye bado amelala na akimaliza anaosha vyombo anavaa uniform na kuacha amekunja shuka lake maana alikuwa na Moja la kulalia Kisha anawaaga wazazi anakimbia shuleni kugonga kengere kwa sababu alikuwa time keeper .
4. Akifika shuleni anawasimamia darasa la kwanza na la pili kwa sababu yeye na mtoto wa tajiri waliokuwa darasa la tano, na baadae anaingia darasani na kuanza kusoma na alikuwa anabaki shuleni mpaka saaa na zikifika saa nane anaenda nyumbani akifika nyumbani ana Kuta wazazi wake bado wako shamba anabadilisha nguo anachukua ndoo anaenda kisomani kuchota maji anayaleta anachemsha maji na kusonga ugali na kupika mboga kwa ajili ya kulisha ugali, akimaliza anakula anawabakizia wazazi wake ila yeye anakula na ndugu yake akimaliza kabla ya jua kuisha anafanya homework mapema na kujisomea kidogo kabla ya giza kuingia kwa sababu hawakuwa na umeme.
5, giza likiingia tu anawaosha ndugu zake na yeye anaoga na akimaliza asaidiana kuandaa chakula cha jion na Mama yake na baadae wanawasha tochi wanaenda kula na kulaa na hayo ndiyo maisha na ratiba ya mtoto wa maskini.
Itaendelea.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 web hosting 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu
Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambao walipoteana katika hali za kukimbizwa na wazazi Ili waweze kutimiza ndoto zao na siku wakakutana wakiwa watu wazima.
Soma Zaidi...WAKATI WA KUFUMBUKA
Post hii ni mwendelezo wa hadithi inayohusu Kufumbuka ambapo , John anaonekana kama sio mtoto wa Mzee maganga kwa sababu na miungu imekili kwa sababu chakula chote kimeliwa na kuisha.
Soma Zaidi...Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya tatu)
Post hii inahusu zaidi mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini wakipanda gari kuelekea shule kuanza maisha mapya.
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.
Soma Zaidi...