picha

Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini.

Mtoto wa Tajiri na maskini .

1.watoto hawa walikuwa majirani, na walikuwa wanasoma shule moja , kila siku mtoto wa tajiri alikuwa anaamshwa anaoshwa, anasaidiwa kupiga mswaki anavalishwa anaangaliwa cha na baadae anawekwa kwenye gari mpaka shuleni na kufungiwa juice na maanda kwenye begi kwa ajili ya kula baadae , na mda wa saa nne alikuwa anafuatwa shule anaenda kunywa maziwa nyumbani na kurudishwa kuendelea na masomo na baada ya kumaliza masomo mtoto alifuatwa kwa gari mpaka nyumbani baada ya kufika nyumbani alibadilisha nguo akala chakula alichokuwa ameagizwa kupokwe mara nyingi zilikuwa ni Chipsi.

 

 

 

 

 

2. Baada ya kumaliza kula aliwekewa tv akaanza kuangalia katuni na michezo mingine na alipokuwa anachoka anaenda kuogelea kwenye swimming pool na baadaye alikula kila alichopenda kula na baadae alikwenda kulala hata bila kukumbushwa kufanya home work hiyo ndiyo iliyokuwa ratiba ya mtoto wa tajiri.

 

 

 

 

3. Kama nilivyotangulia kusema kwamba palikuwepo pia mtoto wa maskini, yeye ratiba yake ilikuwa tofauti kabisa na mtoto wa tajiri yeye kila siku alijiamsha mwenyewe akanawa uso akajipaka sabini kwa sababu mafuta yalikuwa shida ,akasafisha nyumba kwa kufagia huku akisubiria chai aliyoweka kwenye mafiga akimaliza kufagia  anakunywa chai bila sukari pamoja na kiporo kidogo cha ugali kilichobaki na akikumbuka kumbakizia mdogo wake ambaye bado amelala na akimaliza anaosha vyombo anavaa uniform na kuacha amekunja shuka lake maana alikuwa na Moja la kulalia Kisha anawaaga wazazi anakimbia shuleni kugonga kengere kwa sababu alikuwa time keeper .

 

 

 

 

 

4. Akifika shuleni anawasimamia darasa la kwanza na la pili kwa sababu yeye na mtoto wa tajiri waliokuwa darasa la tano, na baadae anaingia darasani na kuanza kusoma na alikuwa anabaki shuleni mpaka saaa na zikifika saa nane anaenda nyumbani akifika nyumbani ana Kuta wazazi wake bado wako shamba anabadilisha nguo anachukua ndoo anaenda kisomani kuchota maji anayaleta anachemsha maji na kusonga ugali na kupika mboga kwa ajili ya kulisha ugali, akimaliza anakula anawabakizia wazazi wake ila yeye anakula na ndugu yake akimaliza kabla ya jua kuisha anafanya homework mapema na kujisomea kidogo kabla ya giza kuingia kwa sababu hawakuwa na umeme.

 

 

 

 

5, giza likiingia tu anawaosha ndugu zake na yeye anaoga na akimaliza asaidiana kuandaa chakula cha jion na Mama yake na baadae wanawasha tochi wanaenda kula na kulaa na hayo ndiyo maisha na ratiba ya mtoto wa maskini.

 

 

Itaendelea.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF Views 4682

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 ai web app     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

SAFARI YA MUUJIZA ( SEHEMU YA PILI)

Post hii ni mwendelezo wa hadithi ya safari yenye muujiza ,ni pale mtoto ya Mungu mengi anafika kwenye kituo Cha ntonga na kuona yake mazingira na kufahamu njia ya kwenda kule.

Soma Zaidi...
Hadithi hii inahusu hasara za wivu na kutokuwa wazi

Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu, kwa sababu ya kuwepo kwa marafiki wasio waaminifu wanasababisha kuharibiana maisha bila kujua kwa sababu ya kuonekana wivu na kutokuwa wazi.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu zaidi vijana wawili ambao ni msichana na mvulana walioingia kwenye mahusiano wakiwa sekondari na wakahaidiana kuoana ila kwa sababu mbalimbali walizokutana nazo kwenye safari yao ya mahusiano mmoja akamsaliti mwingine na kusababisha kupo

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya pili)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya Usaliti kati ya Rhoda na Moses ambapo Moses anampenda sana Rhoda na wakati wa kuoa umefika ila akagikilia kwamba akimuoa Rhoda inawezekana wasipate watoto kwa sababu ya mimba ambazo Rhoda alikuwa anatoa mara kwa mara.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, tunajua kuwa mama yake na binti alimtorisha yule binti mbali kabisa ila kijana naye aliamua kutoroka na kumfuata binti mfalme na hatimaye akampata alipo.

Soma Zaidi...