MTOTO WA TAJIRI NA MTOTO WA MASKINI ( SEHEMU YA NNE)


image


Post hii inahusu zaidi watoto Hawa wawili wakiwa kwenye kituo cha mapumziko ambapo mtoto wa tajiri anabugia soda aliyopewa na yule mwalimu pia tumbo linaanza tena na anaanza kuendesha


Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini .

1. Basi baada ya wale watoto wawili kukutana na mwalimu wa Ile shule, Hawa watoto hawakujua kwamba ni mwalimu Bali ni msamaria mwema tu, basi watoto Hawa walinunuliwa soda , mtoto wa maskini kwa sababu alikuwa na kiasi na wazazi wake walimwambia kwamba asitumie vitu vya kula njiani  kwa mara nyingi alitunza Ile soda ila mtoto wa tajiri kwa sababu ya kula kula kila mara alibugia Ile soda na kwa sababu tumbo lilikuwa halijakaa vizuri alianza kuendesha tena.

 

2. Basi yule mtoto badala ya kukimbilia chooni alijichafua kwenye nguo zake na akasubilia kusafishwa kama kawaida yake , Bali yule mwalimu alimwambia mwanangu hauko nyumbani na pia wazazi wako hawapo hapa jikaze ujisafishe kwa sababu yule mtoto wa maskini aliona jinsi wale makonda walivyomsafisha na yeye akachukua maji akammwagia maji na mwalimu akamwambia ajisafishe na yeye akajisafisha na kwa sababu ilikuwa usiku kidogo baridi lilikuwa ni kama lote  mwalimu akamwonea huruma akaamua kumuomba number ya wazazi wake na kuwapigia.

 

3. Basi baada ya kusikia sauti ya wazazi wake alilia kwa sauti kubwa na kuanza kusema kwa nini mmenitesa kwa nini hamkunifundisha maisha na mbona watoto wenzangu hawana shida hapa mimi mtaniua kama maisha ni hivi hamjanitendea haki mwenzangu aliambiwa kila kitu hata hajaaibika hata kidogo na wazazi wakalaumiana wao kwa wao, basi mtoto akasema sitapanda tena gari la jumla nataka gari la binafsi , kwa sababu baba Ela zilikuwepo aliongea na yule mwalimu Ili wakodi gari la binafsi na yule mtoto wa maskini pamoja na yule mwalimu walikodiwa gari na wakasafiri mpaka shuleni, yule mtoto wa tajiri alifurahi sana na yule mtoto wa maskini alikuwa akishangaa kila kitu.

 

4. Basi baada ya kufika pale shuleni mwalimu akajitambulisha wazi kwamba yeye ni mkuu wa shule pale yule mtoto wa tajiri aliumia sana kwa sababu alikuwa hataki kuhaibika na akikumbuka alichokifanya shuleni, kwa hiyo wanafunzi wakapelekwa bwenini, wakaweka vitu vyao mwalimu alishangaa kuona mtoto wa maskini akiwa na ki mzima kidogo na mtoto wa tajiri ana kila kitu na begi kubwa na ka thamani kubwa kwa hito mwalimu akaona tofauti kati ya wake watoto kati ya vitu walivyonavyo na kati ya tabia zao. 

 

5. Basi wakapelekwa mezani kupata chakula wakakuta ni ugali wa Dona maharage na pia maji ya kunywa , yule mtoto wa maskini akamshukuru Mungu kwa kuona chakula cha aina Ile na mtoto wa tajiri aliangua kilio kuona chakula kile kwa sababu alikuwa hajawahi kuona na watu wote wakaamka na wafanyakazi wakashangaa yule mtoto.

Itaendelea



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    2 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    6 Hadiythi za alif lela u lela    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Hatma ya kinyozi maishani mwangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Hadithi ya binti mwenye kufichwa mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Familia mpya baada ya harusi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Hadithi iliyosimuliwa na mshona nguo
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Jaribio la pili la aladini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Safari ya tatu ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Kila kitu ambacho wanaume wanatakiwa kufahamu kuhusu wanawake.
Hii ni siri kubwa kuhusu wanawake. Hapa utajifunza jinsi ya kumfanya mwanamke asikuache. Soma Zaidi...

image Hadithi ya binti wa pili mwimba mashairi mwenye makovu
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Safari ya pili ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano, baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kuona udhaifu wake kwamba anapenda sana mali. Soma Zaidi...