image

Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

-  Mtume (s.a.w) alitumia kila aina ya fursa iliyopatikana katika kuufikisha 

    ujumbe Uislamu kwa watu wengine.

 

-  Mtume (s.a.w) alifikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu na makabila mbali 

    mbali kwa siri na dhahiri kutokana na uadui wa Maquraish dhidi yake.

 

-  Mtume (s.a.w) alitumia mikataba kwa kuandaa ummah wa kiislamu kutoka 

   sehemu mbali mbali hasa mji wa Madinah (Yathrib) kama ifuatavyo;

   -  Hii ilikuwa ni baina ya Mtume (s.a.w) na watu wanaotoka nje ya mji wa   

      Makkah hasa waliokuja kuhiji msimu wa Hija.

 

   -  Mtume (s.a.w) alikutana na kikosi cha kwanza kabisa cha watu sita (6) 

      kutoka Madinah (Yathrib) wa kabila la Khazraj, baada ya kuwafikishia 

      ujumbe wa Uislamu, walisilimu na wakaahidi kuufikisha kwao Madina.

 

  -  Mwaka uliofuata, 621 A.D, kikundi kingine cha waislamu 12 (2 Aus na 

     10 Khazraj) walikutana na Mtume (s.a.w) kwa siri eneo la ‘Jaratul 

     ‘Aqabah’ na kuweka mkataba wa kwanza wa ‘Aqaba na kukubaliana 

      yafuatatayo;

  1. Hawataabudu chochote isipokuwa Allah (s.w) pekee.
  2. Hawataiba wala hawatapokonya misafara ya biashara njiani.
  3. Hawatazini.
  4. Hawatawaua watoto wao tena.
  5. Hawatasema uongo wala hawatawasingizia wengine uovu.
  6. Hawatamuasi Mtume kwa kila atakalowaamrisha na watakuwa waaminifu kwake kwa hali yeyote iwayo.

 

                -  Mtume (s.a.w) aliwapa mwalimu wa kuwafundisha Uislamu, ‘Mus’ab bin 

                             Umair.

                -  Mwaka uliofuata, 622 A.D.walimjia Mtume (s.a.w) waislamu 75   

    (wanawake 2) wakiongozwa na mwalimu wao, ‘Mus’ab na kufunga   

    Mkataba wa pili wa ‘Aqabah sehemu ile ile kwa kukubaliana kuwa;

 

               

                -  Mtume (s.a.w) aliwachagulia viongozi 12 (9 Khazraj na 3 Aus) na watu 

                             watakaokuwa chini ya kila kiongozi, na wanaume wote walimpa Mtume 

                            (s.a.w) mkono wa bai’at kwa maana ya utii wao kwake.

 

                -  Baada ya kikundi hicho kurejea na kufika Madinah salama, ndipo Mtume 

                            (s.a.w) aliwatangazia waislamu wote wa Makkah kuhamia Madinah.

 

                -   Na takriban baada ya miezi miwili hivi, Waislamu wote wenye uwezo wa   

                            kuhama walishahamia Yathrib (Madinah) kwenda kujiimarisha zaidi.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 802


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kuanzishwa kwa Polisi na magereza kati uislamu wakati wa Makhalifa
Kuanzishwa kwa Polisi. Soma Zaidi...

TAREKH, HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
1. Soma Zaidi...

Mbinu Alizozitumia Nabii Shu’ayb(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe Wake
Soma Zaidi...

Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam
“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”. Soma Zaidi...

Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Bani Israil
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SULEIMAN
Soma Zaidi...

Kusingiziwa Nabii Sulaiman Uchawi
Pamoja na Ucha-Mungu aliokuwa nao Nabii Sulaiman watu hawakuacha kumsingizia mambo machafu. Soma Zaidi...

Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...

Imam Bukhari na Sahihul Bukhari
Soma Zaidi...

Kuanzishwa kwa dola ya kiislamu madinah
Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...