Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza il

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya tatu).

1. Kama tulivyomalizia kwenye sehemu ya pili pale mama wa kijana wa kiume wa mfalme alitaka kumuua binti na bibi ili kupoteza ushahidi ila kijana huyo wa mfalme aliwahi akawaokoa na kumwona kipenzi cha moyo wake na kumchukua nyumbani kama mke wake ila mama hakukubaliana naye ila mfalme kwa kuwa alikuwa anampenda kijana wake akisikiliza kila kitu alichotaka na akaamua kufanya sherehe kubwa na ya kifahari.

 

2 . Na yule bibi kwa kuwa alipenda sana umaarufu na maisha mazuri alijisalimisha kwa wake wenza na akatoa siri zote za yule mke mdogo wa mfalme, wale wake wenza walifurahi sana kusikia habari hiyo na wakapata sehemu ya kumwaibisha adui yao kwa sababu yule mke mdogo wa mfalme alikuwa ni kama kizuizi kwao na mfalme, basi wakapanga njama na kutunza siri ili siku ya kumwapisha mfalme siri itobolewe na kujana wa kiume wa mfalme hasiweze kupata ufalme.

 

3. Katika wakati ule palikuwepo na sheria moja kwamba ili mtu aje kuwa mfalme ni lazima awe ameoa kwenye ukoo ambao hawana undugu hata kidogo ili kuepuka hali ya ufalme kugawanyika kwa hiyo walitaka ufalme ubaki ndani, au kama  kwenye familia ya kifalme hakuna mtoto wa kiume wa kurithi ufalme au yupo ila hana sifa za kuwa mfalme mtoto wa kike anaweza kuwa malkia ila mme wake atoke sehemu tofauti na ile sehemu na hasiweze na undugu wowote na familia ya kifalme iwe kati ya ndugu wa wake wenza yaani pasiwepo na undugu hata chembe.

 

4. Katika maandalizi yote hayo mama wa kijana wa kiume wa mfalme aliona kwamba mwanae hawezi kupata ufalme kwa sababu aliona bibi yupo pale akiwa na ushahidi wote na yuko kati ya maadui zake akapata shida sana akawaza mpaka akakonda , kwa kuwa bibi alikuwa mnafiki na mpenda sifa aliamua kumwita yule mke wa mfalme kwa siri akamwambia kuwa kwamba kwa sasa mwanao hawezi kupata ufalme sasa cha kufanya ni kuhakikisha kuwa tunafanya mbinu ili kijana aweze kuachana na yule binti .

 

5. Kwa kuwa yule Mke wa mfalme alikuwa kwenye hali ngumu akamuuliza bibi tufanye je? Bibi akasema nitakwambia cha kufanya baada ya siku chache, kisha bibi akaenda kwa yule mke wa kwanza wa mfalme akasema andaa binti yako ili yule kijana wa kiume wa mfalme hasipopata ufalme huyu atakuwa malkia. Baadae siku mbili zinafika bibi akaenda kuonana na mke mdogo wa mfalme kwa ajili ya maongezi.



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/07/13/Wednesday - 03:35:03 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1092


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Hadithi ya kisiwa cha mawe yanayolia
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Usichofahamu kuhusu mazoezi
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo hufahamu kuhusu mazoezi,ni mambo ambayo utokea au no matokeo mazuri kwa watu wanaofanya sana mazoezi. Soma Zaidi...

USALITI (sehemu ya pili)
Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya Usaliti kati ya Rhoda na Moses ambapo Moses anampenda sana Rhoda na wakati wa kuoa umefika ila akagikilia kwamba akimuoa Rhoda inawezekana wasipate watoto kwa sababu ya mimba ambazo Rhoda alikuwa anatoa mara kwa mara. Soma Zaidi...

Mtihani penzini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

HADITHI YA SIRI YA UTAJIRI WA AJABU : sehemu ya 01
huu ni ufupisho wa kisa cha utajiri wa ajabu katika kijiji fulani huko zamani za kale. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mtihani unafika ila Jackie hakujiandaa alishutuliwa na marafiki zake baada ya kuona mwenendo wake haueleweki. Soma Zaidi...

Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya Kaka wa kwanza wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Kuingia kwa wageni
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Kwisha kwa chakula
Posti hii inakwenda kukuletea muendelezo wa safari za Sinbad Soma Zaidi...

Mtoto wa Tajiri na maskini ( sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini. Soma Zaidi...

Jaribio la pili la aladini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...