Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne.
1. Basi siku ya maongezi ikafika kati ya bibi na mke wa mdogo wa mfalme,bibi akamsalimia vizuri akampa sifa zote ila akamwambia kwamba wafanye utaratibu wa kumshauri kijana wa kiume wa mfalme awe na mke wa pili ili aweze kupata ufalme wa nane kwanza na mke huyu ambaye ni ndugu yake na kadri ya sheria hataweza kupata ufalme.
2. Basi bibi na yule mke mdogo wa mfalme wakamwita yule kijana na kumpasha habari ya kila kitu kinachoendelea ila kijana akasema siwezi kumwacha mke wangu ili niwe mfalme bora nikakosa ufalme ila nikaishi na mpenzi wangu, mama yake baada ya kusikia hivyo akahisi kuchanganyikiwa na siku zinaenda kijana hana mda mpaka mama yake akajuta na kusema bora ningewazaa watoto wangu wakiwa wawili.
3. Basi bibi akamwambia Mama usihofu kila kitu kitakuwa sawa nihaidi utanipa nini ,Mama akamwambia nitakutunza mpaka utakapofariki, akasema iwapo yeye atafariki ataacha ujumbe wa bibi kutunzwa maisha yake yote, bibi akasema tuandikiane wakaandikiana bibi akaanza mbinu za kuhakikisha kuwa ufalme unabaki mikononi mwa uzao wa mke mdogo.
4. Baada ya bibi kutoka kwa yule mke mdogo akaenda kwa yule mke mkubwa ambaye alimwambia aandae binti mkubwa kwa ajili ya kupata umalkia, basi bibi akaenda kwa ndugu wa mfalme akamshawishi kijana wa ndugu wa mfalme akamwambia , mfalme ana mpango wa kugawa mali kwa watoto wake ila mali kubwa zitaenda kwa binti wa kwanza na kwa mme wake akamwambia kijana kwa nini usimtongoze yule binti na ukampa mapenzi ya kweli ili upate zawadi nyingi na kuishi na binti wa mfalme.
5. Kijana akafanya hivyo na akafanikiwa kumpa binti yule mimba na binti akaogopa kuishi kwa mfalme akiwa na mimba kwa sababu siku zile wasichana waliobobea mimba kwa waliuawa na yule kijana akamwoa mtoto wa mfalme . Kwa hiyo sifa za kuwa malkia zikaishia hapo . Bibi baada ya kufanikiwa mbinu hiyo akaenda kwa mke mdogo na kutoa taarifa mke mdogo alifurahi sana ila akaendelea kumwacha bibi akae kwa wake wenza ili kuleta habari zaidi, basi bibi akapanga kukutana na mke mdogo kwa maongezi zaidi,
itaendelea baadae
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Dua za Mitume na Manabii π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π4 Kitabu cha Afya π5 ai web app π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Posti hii inahusu zaidi habari za Mama mmoja aliyekuwa mchoyo akampa mkate mwehu na kuutia Sumu ila kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu sana aliutunza mkate na kuwapatia watoto wa yule mama waliokuwa wakitoka shule na njaa kali
Soma Zaidi...Hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya Binti mfalme ni hadithi ya kusisimua, kuhusu hadithi hii ni kwamba mfalme alihitaji mtoto wa kiume ila wanawake wote hawakumpata ila alitokea mke mdogo mmoja wa mfalme akajifungua watoto wawili mapacha mmoja wa kiume na
Soma Zaidi...Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu.
Soma Zaidi...WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 2
Post hii ni mwendelezo wa hadithi ambayo Kwa jina inaitwa wakati wa Kufumbuka, ni mwendelezo wa pale maria anawekwa mbele ya wazee Ili akili kwamba John sio mtoto wa Mzee maganga ila maria akikumbuka wazi kwamba John ni mtoto wa Mzee maganga anakataa kuki
Soma Zaidi...Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, tunajua kuwa mama yake na binti alimtorisha yule binti mbali kabisa ila kijana naye aliamua kutoroka na kumfuata binti mfalme na hatimaye akampata alipo.
Soma Zaidi...Hadithi katika kijiji cha burugo
Β Posti hii inahusu zaidi jinsi ya watu walivyoishi katika kijiji cha burugo .tunajuwa hadithi ni sehemu mojawapo ya kubirudisha na kujifunza kitu flani kutoka kwenye jamii .
Soma Zaidi...