Namna ya kumfanyia usafi Mgonjwa kwa mwili mzima.
Posti hii inahusu namna ya kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima, ni njia ambazo utumika kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima au kumwosha Mgonjwa hasa wale walio mahututi na hawawezi kuamka kitandani.
Namna ya kumwosha Mgonjwa.
1.Kwanza kabisa tunajua kuwa kama mgonjwa hajiwezi na hawezi kuamka mara nyingi usahaulika kwa upande wa usafi, nimeshuhudia mara nyingi wagonjwa wa hivi ukiwaosha hali zao zinabadilika na anapata nafuu na mgonjwa hasipooga kwa mwezi mzima anaweza hasipone haraka kwa hiyo tunapaswa kuwasafisha wagonjwa kama ifuatavyo.
2. Kwanza kabisa unaondoa mashuka ya juu ya mgonjwa na hakikisha hakuna Watu ambao hawahusiki na labda msaidizi tu na siku zote tumia maji ya moto na pia ondoa mito na bakiza kidogo ambayo inaweza kumfanya aweze ku kukaa vizuri.
3.Anza kutoa mashuka ya upande mmoja wakati mgonjwa umemlaza upande na mashuka hayo umeyasogeza kwa upande ambao ameulalia na chukua maji na sabuni weka kwenye Dodoki na anza kusafisha upande mmoja na pia hakikisha chini kuna mpira ili kuepuka kulowanisha kitanda na suhuza sehemu hiyo kwa kitambaa ambacho kimekamuliwa vizuri na hakikisha upande unatakata.
4.Mgeuze vizuri mgonjwa kwa upande wa pili na Isha upande huo vizuri kwa kuweka maji na sabuni kwenye Dodoki na sugua vizuri na baadae suuza kwa kitambaa kisafi kilichokamuliwa na ukimaliza upande wa pili, nenda kwenye sehemu za siri weka maji kwenye kutimbaa pangusa vizuri pia suuza nenda kwenye miguu na fanya hivyo hivyo ila kama mgonjwa anaweza kujifanyia usafi kwenye sehemu za siri mwache afanye mwenyewe.
5.Baada ya hapo mpake mafuta na ondoa mashuka machafu yaliyokuwepo wakati unamsafisha mvalishe nguo na pia mtandikie vizuri na mgonjwa akifanyiwa hivyo mara kwa mara kama alikuwa mahututi na hali yake itakuwa nzuri kabisa na wakati mgonjwa unamsafisha maji lazima yabadilishwe kutoka sehemu moja kwenda nyingine
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 ai web app 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Kumsaidia mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote machoni
Posti hii inahusu hasa jinsi uchafu, wadudu na vitu vingine vinavyoweza kuingia machoni.macho ni mojawapo ya milango mitano ya fahamu ambapo kazi yake ni kuona.
Soma Zaidi...Ijue rangi za mkojo na maana zake katika mwili kuhsu afya yako
Posti hii inahusu zaidi rangi za mkojo na maana zake, hizi ni rangi ambazo uweza kutokea kwenye mkojo wa mtu mmoja na mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa, chakula,na mtindo wa maisha inawezekana unywaji wa maji au kutokunywa maji.
Soma Zaidi...Jinsi ya kujikinga na U.T.I inayijirudia rudia.
Endapo U.T.I inajirudiarudia baada yavkutibiwa inawezabkuwa ikakupa mawazo mengi. Katika post hii nitakufafanulia nini ufanye.
Soma Zaidi...Namna ya kujikinga na kifua kikuu
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia au kujikinga na kifua kikuu, hizi ni njia ambazo utumika ili kujikinga na kifua kikuu
Soma Zaidi...Utaratibu wa maisha kwa aliye athirika
Somo hili linakwenda kukuletea utaratibu wa maisha kwa aliye athirika
Soma Zaidi...Njia za kukabiliana na presha ya kupanda/hypertension
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kupanda
Soma Zaidi...