Namna ya kumfanyia usafi Mgonjwa kwa mwili mzima.
Posti hii inahusu namna ya kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima, ni njia ambazo utumika kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima au kumwosha Mgonjwa hasa wale walio mahututi na hawawezi kuamka kitandani.
Namna ya kumwosha Mgonjwa.
1.Kwanza kabisa tunajua kuwa kama mgonjwa hajiwezi na hawezi kuamka mara nyingi usahaulika kwa upande wa usafi, nimeshuhudia mara nyingi wagonjwa wa hivi ukiwaosha hali zao zinabadilika na anapata nafuu na mgonjwa hasipooga kwa mwezi mzima anaweza hasipone haraka kwa hiyo tunapaswa kuwasafisha wagonjwa kama ifuatavyo.
2. Kwanza kabisa unaondoa mashuka ya juu ya mgonjwa na hakikisha hakuna Watu ambao hawahusiki na labda msaidizi tu na siku zote tumia maji ya moto na pia ondoa mito na bakiza kidogo ambayo inaweza kumfanya aweze ku kukaa vizuri.
3.Anza kutoa mashuka ya upande mmoja wakati mgonjwa umemlaza upande na mashuka hayo umeyasogeza kwa upande ambao ameulalia na chukua maji na sabuni weka kwenye Dodoki na anza kusafisha upande mmoja na pia hakikisha chini kuna mpira ili kuepuka kulowanisha kitanda na suhuza sehemu hiyo kwa kitambaa ambacho kimekamuliwa vizuri na hakikisha upande unatakata.
4.Mgeuze vizuri mgonjwa kwa upande wa pili na Isha upande huo vizuri kwa kuweka maji na sabuni kwenye Dodoki na sugua vizuri na baadae suuza kwa kitambaa kisafi kilichokamuliwa na ukimaliza upande wa pili, nenda kwenye sehemu za siri weka maji kwenye kutimbaa pangusa vizuri pia suuza nenda kwenye miguu na fanya hivyo hivyo ila kama mgonjwa anaweza kujifanyia usafi kwenye sehemu za siri mwache afanye mwenyewe.
5.Baada ya hapo mpake mafuta na ondoa mashuka machafu yaliyokuwepo wakati unamsafisha mvalishe nguo na pia mtandikie vizuri na mgonjwa akifanyiwa hivyo mara kwa mara kama alikuwa mahututi na hali yake itakuwa nzuri kabisa na wakati mgonjwa unamsafisha maji lazima yabadilishwe kutoka sehemu moja kwenda nyingine
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Njia za kujikinga na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari
Soma Zaidi...Umuhimu wa pua kama mojawapo ya mlango wa fahamu
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa pua kama mojawapo ya mlango wa fahamu.pua ni mlango wa fahamu ambao uhusika na kupumua.
Soma Zaidi...Kazi za chanjo ya polio
Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo za polio na kazi zake,hii ni chanjo ambayo unazuia maambukizi ya Virusi vinavyosababisha polio.
Soma Zaidi...Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walioingiliwa na uchafu puani.(foreign body).
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa mgonjwa alieye ingiwa na uchafu puani (foreign body)
Soma Zaidi...Mambo ya kuzingatia unapokuwa unatoa huduma ya kwanza
Huduma ya kwanza ni huduma inayotolewa kwa mtu yeyote aliyepata ajali au mgonjwa yeyote kabla hajapelekwa hospitalini
Soma Zaidi...Aina kuu tatu za mvunjiko wa viuno vya mwilini na mifupa
Posti hii inahusu zaidi Aina kuu tatu za mvunjiko ni Aina za kuvunjika ambazo uwakumba watu mbalimbali na watu ushindwa kutambua hizi Aina tatu za mvunjiko, zifuatazo ni Aina za mvunjiko.
Soma Zaidi...