Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi.
Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa.
1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kila mtu anaweza kuwa na mgonjwa kwa hiyo wagonjwa hao wanapaswa kufanyiwa usafi hasa wale walio mahututi na hawawezi kujifanyia usafi wenyewe kwa hiyo tunapaswa kufuata njia zifuatazo ili tusiweze kuleta madhara mengine kwa sababu pengine wanakuwa hawajiwezi hata kuongea hawawezi.
2. Kwanza kabisa kama mgonjwa anaweza kusikia au kuongea ujamwambia unakuja kumfanyia nini kwa mda huo kusudi aweze kujua kinachoendelea.
3.Baada ya kumwambia unaosha mikono yako na unahakikisha kubwa unamjengaea mazingira ya kuwepo nyingi wawili yaani wewe na mgonjwa au na msaidizi wako kwa kufanya hivyo mgonjwa ataweza kuwaamini na kuwa huru ili umsafishe na sio kila mtu atakayepita ajue mnafanya nini.
4. Mwekee mgonjwa mto kwa nyuma na uso wake uangalie chini ili kuhakikisha kuwa maji yanaweza kutiririka chini kwa urahisi kutoka mdomoni na hakikisha maji yasiingie kwenye mfumo wa hewa hasa kwa wagonjwa wale ambao hawajiwezi kabisa au hawawezi kuongea kabisa.
5. Weka kitambaa chini ili kuepuka kuchafua mashuka yaliyotandikwa, weka dawa ya meno kwenye maswaki, anza kumsafisha mgonjwa kwenye sehemu zote za kinywa sugua ulimi na fizi zote vizuri.
6.Suuza mdomo kwa kutumia maji safi kama mgonjwa hawezi hata kutema maji hakikisha unaruhusu maji yanamwagika kwenye beseni na ukitaka kuhakikisha kubwa maji yameisha chukua kitambaa kisafi na pangusa vizuri ili kuhakikisha kubwa maji yameisha ili yasije kuingia kwenye koo la hewa.
7.Baada ya kumaliza safisha vifaa vyote na virudishwe kwenye sehemu safi ili uweze kuvitumia tena
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo mbalimbali ambayo husababisha kizunguzungu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi ajali ya jicho na visababishi vyake, ajali ya jicho ni pale jicho linavyoingiliwa na uchafu na vitu vingine ambavyo havistahili kuwa kwenye jicho
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuyatunza macho
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Soma Zaidi...Hii post inahusu zaidi kazi za wahudumu wa afya wakati wa kutoa dawa, ni kanuni zinazopaswa kufuata wakati wa kutoa dawa kwa wagojwa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mabadiliko katika umri wa kubarehe kwa wsichana, ni kipindi ambacho watoto huelekea ujana, utokea Kati ya miaka kuanzia Kumi na kuendelea.
Soma Zaidi...