Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa
Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi.
Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa.
1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kila mtu anaweza kuwa na mgonjwa kwa hiyo wagonjwa hao wanapaswa kufanyiwa usafi hasa wale walio mahututi na hawawezi kujifanyia usafi wenyewe kwa hiyo tunapaswa kufuata njia zifuatazo ili tusiweze kuleta madhara mengine kwa sababu pengine wanakuwa hawajiwezi hata kuongea hawawezi.
2. Kwanza kabisa kama mgonjwa anaweza kusikia au kuongea ujamwambia unakuja kumfanyia nini kwa mda huo kusudi aweze kujua kinachoendelea.
3.Baada ya kumwambia unaosha mikono yako na unahakikisha kubwa unamjengaea mazingira ya kuwepo nyingi wawili yaani wewe na mgonjwa au na msaidizi wako kwa kufanya hivyo mgonjwa ataweza kuwaamini na kuwa huru ili umsafishe na sio kila mtu atakayepita ajue mnafanya nini.
4. Mwekee mgonjwa mto kwa nyuma na uso wake uangalie chini ili kuhakikisha kuwa maji yanaweza kutiririka chini kwa urahisi kutoka mdomoni na hakikisha maji yasiingie kwenye mfumo wa hewa hasa kwa wagonjwa wale ambao hawajiwezi kabisa au hawawezi kuongea kabisa.
5. Weka kitambaa chini ili kuepuka kuchafua mashuka yaliyotandikwa, weka dawa ya meno kwenye maswaki, anza kumsafisha mgonjwa kwenye sehemu zote za kinywa sugua ulimi na fizi zote vizuri.
6.Suuza mdomo kwa kutumia maji safi kama mgonjwa hawezi hata kutema maji hakikisha unaruhusu maji yanamwagika kwenye beseni na ukitaka kuhakikisha kubwa maji yameisha chukua kitambaa kisafi na pangusa vizuri ili kuhakikisha kubwa maji yameisha ili yasije kuingia kwenye koo la hewa.
7.Baada ya kumaliza safisha vifaa vyote na virudishwe kwenye sehemu safi ili uweze kuvitumia tena
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π3 Kitau cha Fiqh π4 Simulizi za Hadithi Audio π5 ai web app π6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Aina za kuungua
Post hii inahusu Aina za kuungua, kuungua ni Hali ya kubabuka kwa ngozi ya mwili na kusababisha madhara mbalimbali
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENGβATWA NA NYOKA
Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu.
Soma Zaidi...Dalili za shambulio la hofu
Shambulio la hofu ni tukio la ghafla la hofu kali ambayo husababisha athari kali za kimwili wakati hakuna hatari halisi au sababu inayoonekana. Mashambulizi ya hofu yanaweza kuwa ya kutisha sana. Mashambulizi ya hofu yanapotokea, unaweza kufikiri kwamba
Soma Zaidi...Namna ya kujikinga na kifua kikuu
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia au kujikinga na kifua kikuu, hizi ni njia ambazo utumika ili kujikinga na kifua kikuu
Soma Zaidi...Kazi ya chanjo ya kifua kikuu
Posti hii inahusu kazi ya chanjo ya kifua kikuu kwa kitaalamu huitwa BCG. Ni chanjo ambayo uzuia kifua kikuu na ukoma.
Soma Zaidi...