picha

Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa

Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi.

Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kila mtu anaweza kuwa na mgonjwa kwa hiyo wagonjwa hao wanapaswa kufanyiwa usafi hasa wale walio mahututi na hawawezi kujifanyia usafi wenyewe kwa hiyo tunapaswa kufuata njia zifuatazo ili tusiweze kuleta madhara mengine kwa sababu pengine wanakuwa hawajiwezi hata kuongea hawawezi.

 

2. Kwanza kabisa  kama mgonjwa anaweza kusikia au kuongea ujamwambia unakuja kumfanyia nini kwa mda huo kusudi aweze kujua kinachoendelea.

 

3.Baada ya kumwambia unaosha mikono yako na unahakikisha kubwa unamjengaea mazingira ya kuwepo nyingi wawili yaani wewe na mgonjwa au na msaidizi wako kwa kufanya hivyo mgonjwa ataweza kuwaamini na kuwa huru ili umsafishe na sio kila mtu atakayepita ajue mnafanya nini.

 

4. Mwekee mgonjwa mto kwa nyuma na uso wake uangalie chini  ili kuhakikisha kuwa maji yanaweza kutiririka chini kwa urahisi kutoka mdomoni na hakikisha maji yasiingie kwenye mfumo wa hewa hasa kwa wagonjwa wale ambao hawajiwezi kabisa au hawawezi kuongea kabisa.

 

5. Weka kitambaa chini ili kuepuka kuchafua mashuka yaliyotandikwa, weka dawa ya meno kwenye maswaki, anza kumsafisha mgonjwa kwenye sehemu zote za kinywa sugua ulimi na fizi zote vizuri.

 

6.Suuza mdomo kwa kutumia maji safi kama mgonjwa hawezi hata kutema maji hakikisha unaruhusu maji yanamwagika kwenye beseni na ukitaka kuhakikisha kubwa maji yameisha chukua kitambaa kisafi na pangusa vizuri ili kuhakikisha kubwa maji yameisha ili yasije kuingia kwenye koo la hewa.

 

7.Baada ya kumaliza safisha vifaa vyote na virudishwe kwenye sehemu safi ili uweze kuvitumia tena

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1675

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 web hosting     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Athari za mkojo mwilini.

Posti hii inahusu zaidi athari za mkojo mwilini, kwa kawaida tunafahamu kwamba mkojo ni matokeo ya mkusanyiko wa uchafu wa maji maji yanayokusanyika kutoka mwilini ikiwa mkojo umebaki mwilini usababisha madhara mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Aina za vidonda

Posti hii inahusu zaidi Aina mbalimbali za vidonda kwenye mwili wa binadamu, ni vidonda ambavyo utokea kwenye mwili wa binadamu kwa Aina tofauti.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu kazi za ini.

Posti hii inahusu zaidi kazi za ini, kwa kawaida tunafahamu kwamba ini ni sehemu muhimu kwenye mwili wa binadamu kwa sababu ni.likikosa kufanya kazi yake maisha ya binadamu yanakuwa hatarini kwa sababu mbalimbali.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEANGUKA KIFAFA

Kifafa kinaweza kumpata mtu muda wowte.

Soma Zaidi...
Njia za kuingiza chanjo mwilini

Posti hii inahusu njia mbalimbali ambazo utumika kupitisha chanjo, njia hizo utegemea na kazi ya chanjo kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...