Namna ya kumsaidia mtoto mwenye degedege

Degedege ni ugonjwa unaoshambulia sana watoto chini ya miaka mitano,na uwaletea matatizo mengi pamoja na kuwepo kwa ulemavu na vifo vingi vinavyosababishwa na ugonjwa huu.

Zifuatazo ni njia za kumsaidia mtoto kama amepatwa na degedege,

1. Mlaze mtoto kwenye sehemu ambayo itazuia kungata ulimi, kwa sababu mtoto akiachwa na degedege atasikia maumivu  kwenye ulimi na anaweza kushindwa kunyonya au kula

 

2. Kama Kuna makohozi yoyote yanayombana kifuani au kohoni inabidi yatolewe kwa sababu yanaweza kuingia kwenye mfumo wa hewa na kuleta matatizo mengine

 

3.mpatie mtoto dawa ambazo zinahitajika kwa ajili ya kuzuia degedege, dawa hizi ziwe zimeagizwa na daktari hizo dawa zipo hospitalini na uponyesha ugonjwa huu.

 

4. Hakikisha kwamba kiasi Cha sukari kwenye mwili ni Cha kawaida, kama sukari haiko kwenye kiwango chake jaribu kufanya iwe kwenye kiwango na pia angalia kiasi Cha madini kwenye mwili

 

5. Angalia kama joto la mwili liko kawaida, kama  haliko kawaida mpatie dawa za kushusha joto la mwili, angalia pia msukumo wa damu, pia upumuaji,mapigo ya moyo yanaendaje, hakikisha kila kitu kwenye mwili Kiko kawaida

 

6. Hakikisha mtoto Yuko sehemu nzuri ambayo hawezi kuanguka na hakikisha mtoto anaangaliwa mda wote Ili kuepuka madhara mbalimbali yanayoweza kutokea wakati anahudumiwa

 

7. Endelea kuangalia chanzo Cha degedege kama ni maambukizi kutokana na magonjwa nyemelezi au ni bakteria au ni virusi, kama ni ugonjwa wowote inabidi kutibiwa mara Moja.

Angalisho kama mtoto bado ana degedege usimpe kitu chochote Cha kula kwa kupitia mdomoni maana chakula kinaweza kuingia kwenye mfumo wa hewa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 3220

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Hatua za kufuata baada ya kuhisi kuwa umeambukizwa na virusi vya HIV

Posti hii inahusu zaidi hatua za kufuata unapohisi umeambukizwa na virus vya ukimwi. Kwa sababu watu wengi wanakuwa na kiwewe anapohisi ameambukizwa na virus vya ukimwi kwa hiyo wanapaswa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Yanayoathiri afya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mambo yanayoathiri afya

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kuharisha hii ni chanjo wanayopewa watoto wadogo chini ya miaka mitano kwa lengo la kuzuia kuharisha chanjo hiyo kwa kitaalamu huitwa Rotarix.

Soma Zaidi...
Mambo yanayoathiri Uponyaji was jeraha.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kuadhiri Uponyaji wa jeraha.jeraha huleta maumivu makali sana, vilevile Uvimbe, kutoa usaha. Pia jeraha hutofautiana katika kupona kwa mtu mzima na Mtoto.

Soma Zaidi...
Jifunze jinsi ya kumsaidia mwenye kifafa

Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaid

Soma Zaidi...
Namna ya kutoa huduma ya kwanza

Huduma ya kwanza ni huduma anayopewa mgonjwa au mtu yeyote aliyepata ajali kabla ya kumpeleka hospitalini

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa vitamini C mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za upungufu wa vitamini C mwilini

Soma Zaidi...
Zijue kazi za chanjo ya DTP au DPT (Donda Koo,Pepopunda, na kifaduro))

Posti hii inahusu zaidi kazi ya chanjo ya DTP au DPT ambayo Inazuia magonjwa ya Donda Koo, Pepopunda na kifaduro.

Soma Zaidi...
Njia za kutumia Ili kuepuka tatizo la kupungua kwa damu

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa tatizo na kuishiwa damu, kuishiwa damu ni tatizo linolowakumba watu wengi na kusababisha matatizo mengi

Soma Zaidi...
Njia za kushusha presha

Post hii inakwenda kukujulisha njia za kushusha presha iliyopanda.

Soma Zaidi...