picha

Namna ya kumsaidia mtoto mwenye degedege

Degedege ni ugonjwa unaoshambulia sana watoto chini ya miaka mitano,na uwaletea matatizo mengi pamoja na kuwepo kwa ulemavu na vifo vingi vinavyosababishwa na ugonjwa huu.

Zifuatazo ni njia za kumsaidia mtoto kama amepatwa na degedege,

1. Mlaze mtoto kwenye sehemu ambayo itazuia kungata ulimi, kwa sababu mtoto akiachwa na degedege atasikia maumivu  kwenye ulimi na anaweza kushindwa kunyonya au kula

 

2. Kama Kuna makohozi yoyote yanayombana kifuani au kohoni inabidi yatolewe kwa sababu yanaweza kuingia kwenye mfumo wa hewa na kuleta matatizo mengine

 

3.mpatie mtoto dawa ambazo zinahitajika kwa ajili ya kuzuia degedege, dawa hizi ziwe zimeagizwa na daktari hizo dawa zipo hospitalini na uponyesha ugonjwa huu.

 

4. Hakikisha kwamba kiasi Cha sukari kwenye mwili ni Cha kawaida, kama sukari haiko kwenye kiwango chake jaribu kufanya iwe kwenye kiwango na pia angalia kiasi Cha madini kwenye mwili

 

5. Angalia kama joto la mwili liko kawaida, kama  haliko kawaida mpatie dawa za kushusha joto la mwili, angalia pia msukumo wa damu, pia upumuaji,mapigo ya moyo yanaendaje, hakikisha kila kitu kwenye mwili Kiko kawaida

 

6. Hakikisha mtoto Yuko sehemu nzuri ambayo hawezi kuanguka na hakikisha mtoto anaangaliwa mda wote Ili kuepuka madhara mbalimbali yanayoweza kutokea wakati anahudumiwa

 

7. Endelea kuangalia chanzo Cha degedege kama ni maambukizi kutokana na magonjwa nyemelezi au ni bakteria au ni virusi, kama ni ugonjwa wowote inabidi kutibiwa mara Moja.

Angalisho kama mtoto bado ana degedege usimpe kitu chochote Cha kula kwa kupitia mdomoni maana chakula kinaweza kuingia kwenye mfumo wa hewa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 4153

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 ai web app     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Mambo yanayopunguza nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo yanayopunguza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho.

Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa walio na majeraha ya macho kutokana na aina mbalimbali ya jeraha

Soma Zaidi...
Je, utamsaidia vipi mtu aliyeumwa na nyuki?

Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya.

Soma Zaidi...
Njia za kutumia Ili kuepuka tatizo la kupungua kwa damu

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa tatizo na kuishiwa damu, kuishiwa damu ni tatizo linolowakumba watu wengi na kusababisha matatizo mengi

Soma Zaidi...
Hatua za kufuata baada ya kuhisi kuwa umeambukizwa na virusi vya HIV

Posti hii inahusu zaidi hatua za kufuata unapohisi umeambukizwa na virus vya ukimwi. Kwa sababu watu wengi wanakuwa na kiwewe anapohisi ameambukizwa na virus vya ukimwi kwa hiyo wanapaswa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Zijue kazi za ini

Post hii inahusu zaidi kazi za ini, ni kiungo muhimu kwenye mwili ambacho Kina umuhimu sana, bila ini maisha ya mwanadamu yanaweza kuishia pabaya

Soma Zaidi...