image

Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

  1. Maiti awekwe juu ya kitanda chenye tobo katikati ili kupitisha uchafu unaotoka tumboni.
  2. Pawepo na shimo (ufuo) usawa wa tobo la kitanda, kama hakuna uwekano chombo kiwepo cha kukingia uchafu unaotoka kwa maiti.

        -  Pia maiti inaweza kuoshewa bafuni au kwenye karo liliotengenezwa

                     kwa kazi hiyo.

 

  1. Maiti afunikwe na nguo moja kubwa yenye kupenyeza maji wakati wa kuosha.

 

  1. Maiti akalishwe juu ya kitanda usawa wa tobo na shimo (ufuo) na ainamishwe nyuma kidogo, kama ni mzito ni vizuri msaidizi wa muoshaji amuegemeze kwenye magoti yake.

 

  1. Muoshaji apitishe mkono wa kushoto kwenye tumbo la maiti na kuliminyaminya taratibu ili kutoa uchafu ndani.

 

  1. Amlaze chali na kuminyaminya tumbo lake kama ilivyo mara ya kwanza.

 

  1. Aikalishe tena na apitishe mkono wa kushoto chini akiwa amevaa kitambaa au gloves na kusafisha tupu mbili kwa maji safi. 

-   Kama hapaja takata, basi na avae gloves safi na ile chafu aitupe kwenye  

                       ufuo na asafishe tena kama mara ya kwanza mpaka patakate.

 

  1. Baada ya hapo, muoshaji afunge kitambaa safi kwenye kidole chake shahada na akichovye kwenye maji na kumswakisha maiti meno yote na kisha akitupe ufuoni.

 

  1. Muoshaji azungushe kitambaa kingine safi kidole chake kidogo mkono wa kushoto na kumsafisha nacho maiti tundu za pua kisha akitupe ufuoni.

 

  1. Asafishe kucha za maiti kwa kijiti safi na laini iwapo ni ndefu na chafu.

 

  1. Kisha amkalishe maiti na amtawadhishe kwa kufuata taratibu za kawaida za kutia udhu (kutawadha).

 

  1. Maiti akiwa amekalishwa, ataanza kumuoshwa kichwa akiwa ameinamishwa mbele kidogo.

- Kama nywele au ndevu ni nyingi zichanwe na kuoshwa kwa sabuni na

   maji mpaka zitakate.

            - Mwanamke mwenye nywele nyingi zisukwe mikia, na zilizong’oka 

              ziambatanishwe na sanda.

 

  1. Baada ya kuoshwa kichwa, maiti italazwa kwa ubavu wa kushoto na kuanza kuoshwa ubavu wa kulia, mbele na nyuma kwa pamoja kwa sabuni na maji safi mpaka itakate.

 

  1. Kisha itaoshwa ubavu wa kushoto kama ilivyooshwa wa kulia.

 

  1. Baada ya makosho (maosho) haya mawili, la maji na sabuni na la kuondoa sabuni, kosho la tatu la maji liwekewe karafuu na marashi ili kulegeza viungo (maungo) vya maiti.

 

  1. Baada ya makosho matatu haya, muoshaji anyooshe viungo vya maiti na kumlaza kama alikuwa mara tu baada ya kufa.

 

  1. Kisha achukue nguo kavu na kumfuta maiti, na baada ya hapo maiti awekwe juu ya mkeka mkavu na kufunikwa kwa nguo kavu tayari kuvalishwa sanda (kukafiniwa). 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 917


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Ni zipi siku ambazo ni haramu kufunga? na ni kwa nini hairuhusiwi kufunga katika siku hizo
Soma Zaidi...

Ni kwa nini lengo la Funga na swaumu halifikiwi na wafungaji?
Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji Wengi? Soma Zaidi...

malezi ya mtoto mchanga baada ya talaka
Soma Zaidi...

Twahara
FIQH 1. Soma Zaidi...

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Soma Zaidi...

Swala za sunnah na faida zake
Soma Zaidi...

haki na wajibu kwa watumishi wa nyumbani (house boy and house girl)
Soma Zaidi...

Muundo wa Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...

Riba na Madhara Yake Katika Jamii
- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara. Soma Zaidi...

Namna lengo la zakat linavyofikiwa
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Aina za hijjah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kujitwaharisha Najisi ndogo
Soma Zaidi...