image

Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu

Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu.

Ili uweze kutawadha kwanza unatakiwa uandae maji yaliyo safi.  Maji safi ni yale ambayo hayajachanganyika na najisi na yakawa yamenajisika. 

 

Baada ya kuandaa maji yako sasa ni wakati wa kutekeleza ibada ya udhu.  Vyemakuanza kupigamswaki.  Kwani kupiga mswaki ni sunnah ambazo zimesisiyizwa sana katika Uislamu. 

 

Hatuwa za kuchukuwa udhu:

1. Kutia nia:

Nia ni kukusudia kitendo. Hii ni hatuwa ya kwanza na muhimu kwani Mtume s.a.w amesema "kila jambo hulipwa kwa kuzinhatia nia" hadithi ni sahihi. 

 

2. Anza na kupiga bismillah kisha osha kiganja vya mikono.  Osha kwanza kabla hujatumbukiza mikono kwenye chombo. 

 

3. Kisha osha uso: 

Uso unatakiwa uoshwe kwa marefu hake na mapana.  Hakikisha unaziosha sehemu zote za uso kama kwenye kidevu na kufika hadi kwenye maoteo ha masikio.  Uoshaji wa uso unaambatana na kusukutuwa na kuingiza maji puani. 

 

Hivyo basi kwa mpanhilio utaanzakusukutuwa kisha utaingiza maji puani.  Utafanya hivi mara tatu kisha ndipo utaosha uso pia utaosha mafa tatu.  Pia utaosha na kwenye ndevu kuhakikisha kuwa ngozi ya kidefu imepata maji. 

 

4. Kuosha mikono. 

Baada ya kumalizakuosha uso utaosha mikonokwa utaratibu utaanza mkono wa kulia mara tatu kisha mkono wa kushoto mara tatu. Hakikisha kuwa mkono unauosha mpakakwenye kiwiko.  Vyema ukafika juu zaidi. 

 

Endapo mkonoutakuwa huna amaumekatwa utaosha kipande kilichopo.  Baa ya kumaliza mkono wa kulia utaosha wa kushoto. 

 

5. Kupaka maji kichwani: 

Hapa utafanya hivi mara moja kama alivyokuwa akifanya Mtume S.A.W. Hata hivyo hakuna ubaya ukizidisha.  Lengo hapa ni kuoaka maji kichwani na si kuosha nywele. 

 

Upakaji wa maji utaendana na kupaka maji kwenye masikio. Nje ya masikio nandani yake. Kidole cha cha shahada kiingie ndani yavsikio na gumba kipake juu ya sikio. 

 

Ni katika sunnah kutumia maji yaleyale yaliotumika kupakakichwa.  Yaani baada ya kupaka maji kichwani utaingiza kidole cha shahada ndani ya sikio,  kisha gumba wwka juu ya pindo za sikio kwa juu na kupaka maji. 

 

Unapopaka kichwa utaanzia mbele kuja nyuma kisha utatoa nyumana kuleta mbele,  kisha ndipp utamalizia masikioni .

 

6. Kuosha miguu

Kisha utaosha miguu miwili mara tatutatu.  Utaanza wa kulia na kumalizia wa kushoto.  Hakikisha maji yanaingia mpaka kwenye mipasuko ya miguu yaani magaga.  Hakikisha unaosha mpaka kwenye fundo zamiguu yaani kungu za miguu. Vyema ukizidisha mpaka kwenye ugoko. 

 

Baada ya hapo utakuwa umeshatia udhu. Usikose post inayofuata itazungumzia dua ya kumaliza kutia udhu. 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 912


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa
Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki. Soma Zaidi...

Njia za kuzuia na kupunguza zinaa katika jamii
(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii. Soma Zaidi...

Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii. Soma Zaidi...

Taratibu za mahari katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu. Soma Zaidi...

maana ya uchumi kiislamu
Maana ya UchumiMfumo wa maisha wa Kiislamu humuelekeza binaadamu kujenga na kudumisha uhusiano wake na Al-lah (s. Soma Zaidi...

Wanaowajibika kuhijji
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

hukumu ya ombaomba katika uchumi wa kiislamu
Suala la omba-ombaTukiliangalia suala la omba-omba kwa upana kidogo, ambalo hivi sasa linaongelewa katika vikao mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, tutaona kuwa ni Uislamu pekee unaotoa namna bora ya kulishughulikia suala hili. Soma Zaidi...

Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)
Soma Zaidi...

Nafasi ya serikali katika ugawaji
Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi. Soma Zaidi...

Wanaostahiki kupewa zakat
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sunnah za funga ya ramadhan
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ni zipi najisi katika uislamu
Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi. Soma Zaidi...