Namna ya kutekeleza swala ya maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Utaratibu wa kusimamisha swala ya maiti ni kama ifuatavyo;

  1. Maiti iwekwe mbele.
  2. Imamu asimame katikati ya mwili wa maiti ikiwa maiti ni ya kike, na usawa wa mabega kama maiti ni ya kiume.
  3. Maamuma watasimama kwenye mistari (safu) kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, n.k.
  4. Baada ya hapo swala itaanza na kuendelea kama ifuatavyo:
    1. Nia - ambayo ni kukusudia moyoni.
    2. Kuleta takbira ya kwanza; kwa kusema, “Allaah Akbar”
    3. Imamu na maamuma watasoma suratul-Faatiha – kimya kimya.
    4. Imamu ataleta Takbira ya Pili kisha maamuma – kimya kimya kwa maamuma na si lazima kuinua mikono wao. 
    5. Kumswalia Mtume (s.a.w) kama ilivyo katika Tahiyyatu, wote – kimya kimya.
    6. Imamu ataleta takbira ya Tatu kisha maamuma- kama walivyofanya awali.
    7. Wote kumuombea maiti dua kimya kimya, ikiwemo: 

“Allaahumma ghfir lihayyinaa wamaayyitinaa washaahidinaa waghaaibinaa waswaaghirinaa wakaabirinaa wadhakirnaa waunthaanaa. Allaahumma man ahyaytahuu minnaa faahyi ‘alal Islaam. Waman tawaffaytahuu minnaa tawaffahuu ‘alal Imaani. Allaahumma laa tahirimnaa ajirahuu walaa taftinaa ba’adahuu”

    Tafsiri:

“Ewe Allah tusamehe sisi, na maiti wetu, na mashahidi, na wasiokuwepo miongoni wetu, vijana wadogo miongoni mwetu na wakubwa miongoni mwetu, wanamume wetu, na wanawake wetu. Ewe Allah, yeyote yule miongoni mwetu utakayemewezesha kuishi, mjaalie aishi katika Kiislamu na yeyote miongoni mwetu utakayemfisha, mfishe katika Imani (ya Kiislamu). Ewe Allah, usitukatishe ujira kutoka kwake na wala usitufitinishe baada yake.” 

 

            -   Au kwa kifupi tuweza kumuombea maiti kama ifuatavyo;

                “Allaahumma ghfir lahuu warhamhuu wa-afihii wa-afu-anhu”

            Tafsiri:

                “Ewe Allah, Mghufirilie na Umrehemu”.

 

  1. Imamu ataleta Takbira ya nne na maamuma kufuatihia kama awali.
  2. Wote watawaombea waislamu dua – (pia si lazima kuleta dua hii).

Rejea Qur’an (59:10).

 

  1. Imamu kutoa salaam na maamuma kufuatishia bila kutoa sauti kama ilivyo kwenye swala ya kawaida kwa kusema; 

        “Assalaamu ‘alaykum Warahmatullaah (Wabarakaatuh)”

    Tafsiri:

        “Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake”.



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/01/02/Sunday - 02:58:48 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 899


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Saumu (funga)
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa
Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Zoezi
Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira. Soma Zaidi...

Kuhifadhiwa kwa Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Dalili na ishara za jeraha kwenye ngozi
Posti hii inaonyesha dalili,sababu na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyepata jeraha kwenye ngozi kwa kuingiliwa na kitu Kama mwiba,Pini,sindano n.k Soma Zaidi...

Aina za swala..
Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.
Posti hii inahusu zaidi Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji, tukumbuke kuwa mtu aliyefanyiwa upasuaji anakuwa kwenye riski sana ya kupata magonjwa na mambo mengine mbalimbali kwa hiyo kuna dalili zikijitokeza kwa mgonjwa aliyepasuliwa Zinapaswa kuf Soma Zaidi...

Waislamu wanaolazimika kufunga
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hoja juu ya kukubalika hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.
Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume. Soma Zaidi...