NAMNA YA KUTEKELEZA SWALA YA MAITI HATUA KWA HATUA


image


Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)


  • Namna ya kutekeleza swala ya Maiti hatua kwa hatua.

Utaratibu wa kusimamisha swala ya maiti ni kama ifuatavyo;

  1. Maiti iwekwe mbele.
  2. Imamu asimame katikati ya mwili wa maiti ikiwa maiti ni ya kike, na usawa wa mabega kama maiti ni ya kiume.
  3. Maamuma watasimama kwenye mistari (safu) kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, n.k.
  4. Baada ya hapo swala itaanza na kuendelea kama ifuatavyo:
    1. Nia - ambayo ni kukusudia moyoni.
    2. Kuleta takbira ya kwanza; kwa kusema, “Allaah Akbar”
    3. Imamu na maamuma watasoma suratul-Faatiha – kimya kimya.
    4. Imamu ataleta Takbira ya Pili kisha maamuma – kimya kimya kwa maamuma na si lazima kuinua mikono wao. 
    5. Kumswalia Mtume (s.a.w) kama ilivyo katika Tahiyyatu, wote – kimya kimya.
    6. Imamu ataleta takbira ya Tatu kisha maamuma- kama walivyofanya awali.
    7. Wote kumuombea maiti dua kimya kimya, ikiwemo: 

“Allaahumma ghfir lihayyinaa wamaayyitinaa washaahidinaa waghaaibinaa waswaaghirinaa wakaabirinaa wadhakirnaa waunthaanaa. Allaahumma man ahyaytahuu minnaa faahyi ‘alal Islaam. Waman tawaffaytahuu minnaa tawaffahuu ‘alal Imaani. Allaahumma laa tahirimnaa ajirahuu walaa taftinaa ba’adahuu”

    Tafsiri:

“Ewe Allah tusamehe sisi, na maiti wetu, na mashahidi, na wasiokuwepo miongoni wetu, vijana wadogo miongoni mwetu na wakubwa miongoni mwetu, wanamume wetu, na wanawake wetu. Ewe Allah, yeyote yule miongoni mwetu utakayemewezesha kuishi, mjaalie aishi katika Kiislamu na yeyote miongoni mwetu utakayemfisha, mfishe katika Imani (ya Kiislamu). Ewe Allah, usitukatishe ujira kutoka kwake na wala usitufitinishe baada yake.” 

 

            -   Au kwa kifupi tuweza kumuombea maiti kama ifuatavyo;

                “Allaahumma ghfir lahuu warhamhuu wa-afihii wa-afu-anhu”

            Tafsiri:

                “Ewe Allah, Mghufirilie na Umrehemu”.

 

  1. Imamu ataleta Takbira ya nne na maamuma kufuatihia kama awali.
  2. Wote watawaombea waislamu dua – (pia si lazima kuleta dua hii).

Rejea Qur’an (59:10).

 

  1. Imamu kutoa salaam na maamuma kufuatishia bila kutoa sauti kama ilivyo kwenye swala ya kawaida kwa kusema; 

        “Assalaamu ‘alaykum Warahmatullaah (Wabarakaatuh)”

    Tafsiri:

        “Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake”.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    6 Magonjwa na afya    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya muislamu.
Kwenye kipengele hichi tutajifunza ni nani muislamu. Soma Zaidi...

image Maswali kuhusu Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Wanaostahiki kupewa zakat
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya shahada
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kutoa vilivyo vizuri
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Msonge wa uongozi na siasa katika serikali ya kiislamu mafinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Aina kuu za dini
Katika kipengele hichi tutajifunza aina kuu mbili za dini. Soma Zaidi...

image Haki za raia katika dola ya kiislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Uandishi wa hadithi wakati wa mtume (s.a.w)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...