Namna ya kutoa huduma kwa mgonjwa wa Dengue.
Posti hii inahusu zaidi huduma anayopaswa kupata mgonjwa wa ndengue, kwa sababu tunafahamu wazi Ugonjwa huu hauna dawa ila kuna huduma muhimu ambayo anaweza kupata na akaendelea vizuri.
Huduma kwa mgonjwa wa Dengue.
1.Kwa hali ya kawaida Ugonjwa ambao unasababishwa na virusi huwa hauna dawa lakini kuna huduma mbalimbali ambazo utolewa na mgonjwa anaweza kupona na kuendelea na hali yake ya kawaida na pengine huwa tiba inayotolewa kuendana na dalili iliyopo kama Mgonjwa anaumwa kichwa dawa ya maumivu utolewa au kama anaharisha dawa ya kuzuia kuharisha utolewa na mambo kama hayo hatimaye Mgonjwa anapata nafuu na kuendelea na shughuli zake kama kawaida.
2. Kwa sababu mgonjwa wa Dengue anakuwa na maumivu makali ya kichwa kwa kawaida anapewa dawa ya maumivu na kwa wakati mwingine anapewa maji ambayo yamependekezwa na wizara ya afya ni lingers na pengine Mgonjwa kama ana uwezo wa kunywa maji ya kawaida anaweza kunywa na pia kuna wakati mwingine hali ikiwa imefikia pabaya mgonjwa huwa anatoa damu kwa hiyo kuna hatari ya kupungukiwa damu kwa hiyo anaongezea damu na anapewa dawa ya kusaidia damu iache kutoka mara kwa mara.
3. Vile vile Tunapaswa kuzuia Ugonjwa huu kwa kwa kuwapatia watu elimu kuhusu kuwepo kwa ugonjwa huu na kuwapatia mbinu za kujikinga na ugonjwa huu kwa kutumia neti wakati wa usiku kukata vichaka na mazalia ya mbu na kwa wakati mwingine kutumia dawa za kujipaka ili kuweza kupunguza kiwango cha kuenea kwa mbu.
4. Kwa hiyo baada ya kujua Ugonjwa huu jamii pia inapaswa ielezwe wazi pale Ugonjwa huu unapotokea ili kuweza kuwafahamisha watu wajue namna ya kujikinga na hasa kuwakinga watoto wadogo na wazee ambao wapo kwenye hatari kubwa ya kupata matatizo zaidi, kwa hiyo na mila na desturi potovu zinapaswa kuepukwa wakati wa kipindi hiki cha Ugonjwa huu ili kuepuka madhara na matatizo yatokanayo na Ugonjwa ambao hauna dawa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Uchunguzi wa kuharisha damu na tiba yake
Posti hii inahusu zaidi uchunguzi wa kuharisha damu na Tiba yake, ni Ugonjwa ambao unaowashambulia sana watoto hasa wenye chini ya umri wa miaka mitano, kwa hiyo huoaugonjwa tunaweza kuutambua na kutibu kwa njia zifuatazo.
Soma Zaidi...Msaada kwa Mgonjwa aliyeshindwa kupitisha mkojo.
Posti hii utokea huduma ya kwanza kwa mtu aliye na shida ya kushindwa kupitisha mkojo kutoka kwenye kibofu Cha mkojo,
Soma Zaidi...TIBA YA MINYOO AU DAWA YA MINYOO: praziquantel (biltricide) mebendazole (vermox, emverm) na albendazole (albenza).
TIBA YA MINYOO Moja katika sifa za minyoo ni kuwa wanatibika kwa urahisi pindi mgonjwa akipewa dawa husika.
Soma Zaidi...Vimelea vya tumbo (Minyoo): Dalili za kuwepo mwilini na tiba.
Vimelea vya tumbo, maarufu kama minyoo, ni tatizo la kiafya linaloathiri watu wa rika zote, likichangia kwa kiasi kikubwa utapiamlo na upungufu wa damu. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu jinsi ya kutambua dalili za maambukizi, taratibu za utambuzi hospitalini, na mikakati madhubuti ya tiba na kinga ili kudumisha afya ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula.
Soma Zaidi...Matatizo ya tezi ya shingo (Thyroid disorders): Dalili zake.
Tezi ya shingo (Thyroid gland) ni kiungo kidogo chenye umbo la kipepeo kilichopo sehemu ya mbele ya shingo. Ingawa ni ndogo, ina kazi kubwa sana ya kuzalisha homoni zinazodhibiti kila kitu kuanzia kasi ya mapigo ya moyo, joto la mwili, hadi namna tunavyochoma kalori. Matatizo ya tezi hutokea pale tezi hii inapozalisha homoni nyingi sana (Hyperthyroidism) au kidogo sana (Hypothyroidism). Makala haya yanachambua dalili za hali hizi mbili ili kukusaidia kuelewa ishara za mwili wako.
Soma Zaidi...