picha

Namna ya kutunza nywele za mgonjwa

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza nywele za mgonjwa hasa kwa wagonjwa mahututi na wale wasiojiweza tunafanya hivyo ili tuweze kuwatoa kwenye hali ya usafi.

Namna ya kutunza nywele za mgonjwa ambaye hajiwezi.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mara nyingi tunakuwa na wagonjwa majumbani kwetu na tunashindwa kuwahudumia kwa sababu ya kutojua au pengine tunashindwa tuwahudumie namna gani kwa hiyo na nywele za mgonjwa zinapaswa kusafishwa kwa njia zifuatazo.

 

2.Kwanza kabisa unapaswa kumwambia mgonjwa nia na lengo la kumfanyia usafi kama mgonjwa anaweza kusikia na pia hakikisha kuwa hakuna Watu ambao hawahusiki ili mgonjwa aweze kujisikia huru  unaweza kuwa na msaidizi wako.

 

3.Ondoa nguo kwenye sehemu ya kichwa na weka nguo za kumwoshea Mgonjwa inaweza kuwa kanga au kitambaa chochote ambacho ukitoa unaweza kukiosha tena na weka mpira ili maji yasidondoke kwenye godoro na Mashuka mengine.

 

4.Msaidie mgonjwa aweze kusogeza kichwa chake juu ya kitanda ili kuweza kuwa karibu na beseni na hakikisha kichwa kipo kwenye beseni na wakati wa kumwosha nywele tumia maji ya moto .

 

5 Chukua maji kutoka kwenye beseni na mwekee mgonjwa na mwekee kwenye kichwa cha Mgonjwa na weka sabuni safisha nywele za mgonjwa na hakikisha kuwa zimetakata na pia chukua taulo safi upanguse nywele za mgonjwa na safisha sehemu ambapo mgonjwa alikuwepo na hakikisha mgonjwa nywele zake zimekuwa safi.

 

6.Mpake mafuta mgonjwa kwenye nywele zake na kama kuna mba unaweza kuweka dawa ili kuepuka hali ya kujikuna kama inawezekana unaweza kumsuka kama ni mwanamke.

 

7.Kwa hiyo baada ya kujua haya tuwafanyie usafi wa nywele wagonjwa na mtaweza kuona mabadiliko kwa sababu pengine hali ya mgonjwa uendelea kubwa mbaya kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kwa kumfanyia mgonjwa usafi anaweza kupata nafuu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1827

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Ukiwa unalima sana unaweza kukonda

Unadhanivkufanya kazi kunaweza kukusababishia maradhi ama mwili kudhoofu, ama kukonda. Umeshawahivkujiuliza wanao nenepa huwa hawafanyi kazi?

Soma Zaidi...
Huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri

Post hii inahusu zaidi tiba na huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu fati na mafuta na kazi zake mwilini

Hata kama mtu atakuambbia usile vyakula yenye mafuta bado itahitajika kula tu. Kuna mafuta na fati je unajuwa utofauti wao. Ni zipi kazi zao mwilini? Endelea na makala hii

Soma Zaidi...
Utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyeaha

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyesha

Soma Zaidi...
Kwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?

Swali languKwanini mtu alie ng'atwa na nyoka hairuhusiwi kumpa pombe?

Soma Zaidi...
Dalili za sumu ya pombe

hatari matokeo ya kunywa kiasi kikubwa cha pombe kwa muda mfupi. Kunywa pombe haraka kupita kiasi kunaweza kuathiri kupumua kwako, mapigo ya moyo, halijoto ya mwili na kunaweza kusababisha Coma na kifo.

Soma Zaidi...