Namna ya kutunza nywele za mgonjwa

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza nywele za mgonjwa hasa kwa wagonjwa mahututi na wale wasiojiweza tunafanya hivyo ili tuweze kuwatoa kwenye hali ya usafi.

Namna ya kutunza nywele za mgonjwa ambaye hajiwezi.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mara nyingi tunakuwa na wagonjwa majumbani kwetu na tunashindwa kuwahudumia kwa sababu ya kutojua au pengine tunashindwa tuwahudumie namna gani kwa hiyo na nywele za mgonjwa zinapaswa kusafishwa kwa njia zifuatazo.

 

2.Kwanza kabisa unapaswa kumwambia mgonjwa nia na lengo la kumfanyia usafi kama mgonjwa anaweza kusikia na pia hakikisha kuwa hakuna Watu ambao hawahusiki ili mgonjwa aweze kujisikia huru  unaweza kuwa na msaidizi wako.

 

3.Ondoa nguo kwenye sehemu ya kichwa na weka nguo za kumwoshea Mgonjwa inaweza kuwa kanga au kitambaa chochote ambacho ukitoa unaweza kukiosha tena na weka mpira ili maji yasidondoke kwenye godoro na Mashuka mengine.

 

4.Msaidie mgonjwa aweze kusogeza kichwa chake juu ya kitanda ili kuweza kuwa karibu na beseni na hakikisha kichwa kipo kwenye beseni na wakati wa kumwosha nywele tumia maji ya moto .

 

5 Chukua maji kutoka kwenye beseni na mwekee mgonjwa na mwekee kwenye kichwa cha Mgonjwa na weka sabuni safisha nywele za mgonjwa na hakikisha kuwa zimetakata na pia chukua taulo safi upanguse nywele za mgonjwa na safisha sehemu ambapo mgonjwa alikuwepo na hakikisha mgonjwa nywele zake zimekuwa safi.

 

6.Mpake mafuta mgonjwa kwenye nywele zake na kama kuna mba unaweza kuweka dawa ili kuepuka hali ya kujikuna kama inawezekana unaweza kumsuka kama ni mwanamke.

 

7.Kwa hiyo baada ya kujua haya tuwafanyie usafi wa nywele wagonjwa na mtaweza kuona mabadiliko kwa sababu pengine hali ya mgonjwa uendelea kubwa mbaya kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kwa kumfanyia mgonjwa usafi anaweza kupata nafuu.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 1064

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Zijue sababu za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo,ni sababu mbalimbali hasa za kiafya kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...
Njia za kujikinga na kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari

Soma Zaidi...
Utaratibu wa lishe kwa wazee

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wazee

Soma Zaidi...
Yajue malengo ya kusafisha vidonda.

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kusafisha vidonda, kwa sababu Kuna watu wengine huwa wanajiuliza kwa nini nisafishe kidonda hospitalini au kwenye kituo chochote Cha afya, yafuatayo ni majibu ya kwa Nini nisafishe kidonda.

Soma Zaidi...
Zijue kazi za ovari

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa ovari kwenye mwili wa mwanamke. ovari ni sehemu ambapo mayai ya mwanamke hutunza, kwa hiyo kila mwanamke huwa na ovari ambayo husaidia kutunza mayai.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa aliyepatwa na presha ya kushuka

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na presha ya kushuka

Soma Zaidi...
Njia za kufuata unapohudumia watu waliopata ajali

Post hii inahusu zaidi namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa watu waliopata ajali. Ajali ni tukio lisilotarajiwa ambalo kinaweza kumkuta mtu yeyote, tunapotoa huduma ya kwanza tnazingatia rangi ambazo huwakilisha jinsi watu walivyoumia.

Soma Zaidi...
Kuboresha afya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mambo yanayosaidia kuboresha afya

Soma Zaidi...
Hatari ya uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi hatari zilizopo kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa na pia unene usio wa kawaida usababisha mtu kuwa na matatizo mbalimbali hasa saratani za kila sehemu kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Mzunguko wa mwezi kwa mwanamke

Posti hii inahusu zaidi mzunguko wa mwezi kwa mwanamke, ni mzunguko ambao huchukua siku ishilini na nane kwa kawaida Ila lla ubadilika kulingana na mtu, Ila ngoja tuangalie siku ishilini na nane tu.

Soma Zaidi...