NDANI YA JUMBA LA ALADINI


image


Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu


NDANI YA JUMBA LA ALADINI

Hatimaye Aladini anaingia ndani, Loo! Alitamani kupiga kelele, huku ameziba mdomo wake kwa mshangao. Uzuri wa ndani ulikuwa mara dufu ya nje. Ukumbi kubwa ilio katika umbo la duara. Mlango mkuu wa kuingilia kwenye ukumbi ulukuwa na pazia la rangi ya kijivu. Maashindi ya kiarabu yaliyopangiliwa na kutengeneza umbo la uwa zuri lililoonekana kuchanua. Maandishi yalikuwa ya rangi za kuchanganyika huku rangi ya zambarau ikitawala vyema. “Marhaban bikum” yaani karibuni sana, yalikuwa ndio maneno yaliyoandikwa yalivyosomeka.

 

Zuria la rangi nyekundu lilitandikwa na kuenea ukumi mzima. Zuria lilikuwa na michirizi ya zambarau na kutengeneza madoa makubwa ya rangi ya buluu. Zuria lilichanganya rangi nyingine na kutengeneza mauwa majubwa yaliyo mazuri. Rangi za mauwa hayo zilifanana sana na rangi za magoya ya kanga. Yaani madoa meupe na meuzi. Madirisha makubwa yaliyongaa vyema na kuonyesha kwa ufasaha kilicho nje. Michirizi ya madirisha ilikuwa inavutia kama vile ni mikufu ya dhahabu iliyoning’inizwa kweye vipete vya madirisha.

 

Mapazia yaliyokunywa mafundo yalining’inia kwenye madirisha. Aladini aliliendea dirisha moja na kufungua pazia. Loo! Lilikuwa ni pazia zuri sana, lenye rangi ya kijivu kama lile pazia kubwa. Pazia lilikuwa na picha ya ndege yule aliyeunganisha roho mbili hizi. Alikuwa ni ndege mzuri sana kwa kumuangalia. Vipete kwa kuning’inizia pazia vilikuwa vya rangi ya ugoro iliyo wiva sana iliyochanganyika na michirizi ya rangi ya samawati na kutengeneza mabadilishano ya rangi kama pundamilia aliyenona. Pazia lilifunika diisha na kushuka kwa chini na kutengeneza sura ya kuvutia.

 

Meza kubwa iliyozungukwa na viti iliwekwa katikati ya chumba. Ibila shaka ni meza ya kulia chakula, kwani vitu vilivyoonekana kwenye meza vinasadivu yaliyomo. Masinia 6 yaliyofunikwa na makawa ya rangi ya samawati, yenye micirizi ya kahawiya kwa chini. Masinia yalingaa kama ni almazi iliyowekwa. Kabaesni kadogo kalikojaa vijiko, visahani na vitu vingine. Maji safi yalionekana kwenye jagi. Ni masafi sana kiasi cha kuonyesha kana kwamba jagi ni tupu. Aani anaonekana aliye upande wa pili kama ni kioo. Harufunzuri ilikuwa ikitokea kwnye meza kubwa.

 

Viti vikubw avyenye magodoro ya harir vilizunguka meza na kutengeneza duara lama kiota cha mayai ya kuku anayelalia. Viti vizuri vilivyokuwa vya rangi za kupendeza na kuwekwa vikuku nya lulu pembeni ya kila kimoja. Basi uzuri ulioje wa ndani ya jumba hili. Juu karabai mishumaa mikubwa ya rangi nyekundu na njano ilining’inizwa ikiwa kwenye matovu makubwa ya rangi ya zamabarau. Matovu yalionekana kuwa na vijiwe vya ranirangi vikining’inia hakuna aliyejuwa ni madini ya aina gani. Ila vijiwe hivi ifikapo usiku kuakisi mwanga kutoka kwenye mishumaa na kugeuka kama taa zinazowaka.

 

Mjakazi mkubwa aliyeandaliwa na mama Aladini akaanza kupanga kundi la wajakazi na wafanyakazi kila mmoja kwenda kwenye eneo lake la kazi. Mjakazi mwingine aliye mrefu zaidi na mzuri sana akamchukuwa Aladini na mke wake kuwapeleka kwenye chumba chao. Walikutana na mfululizo wa mapazia yasiyopungua 5 ynye rangi mbalimbali za kupendeza. Hatimaye wakakaribishwa na harufu nzuuri iliyotoka nyuma ya pazia lenye rangirangi kama uwa la waridi. Mjakazi akawakaribisha na kurudi nyuma, huku akimuashiria binti sultani sasa ni kazi kwake kuongoza njia.

 

Mjakazi akabakia pale pale, binti sultani akafungua pazia, Loo! Kitasa cha dhahabu kikawakaribisha. Aladini kwa mkono wake akafungua kitasa, mlango ukafunguka. Hatimaye wawili hawa wapo ndani, kinanukia sana chumba chao. Uzuri wa chumba na mapambo hakukuwa na tofauti sana ya kile chumba cha binti Sultani. Tofauti ni kuwa vitu vyake vilikuwa ni vya thamani sana. Hatimaye kwa uchovu wa safari wawili hawa wakaamuwa kupumzika na mlango ukafungwa.

 

Atimaye siku ikaenda hivyo na muda wa chakula ukafika, wakapata chakula kizuri. Mama Aladni aliendeela kuwa pale, ijapokuwa hakupendelea kuishi pale. Alitarajia baada ya ujio wa Sultani arudi nyumbani kwake. Mama Aladini ijapokuwa mambo yote alikuwa akiyashuhudia kwa macho yake lakini hakuwa akiamini hasa uhalisia na nini itakuwa hatima ya mambo yale. Hivyo hakutaka kulekeza maisha yake ya mwanzo kirahisi. Masi ambo yakawa hivyo na usiku ukaingia na hatimaye kukakucha.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    2 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    3 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    4 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    5 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya php    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image SAFARI YA MUUJIZA ( SEHEMU YA PILI)
Post hii ni mwendelezo wa hadithi ya safari yenye muujiza ,ni pale mtoto ya Mungu mengi anafika kwenye kituo Cha ntonga na kuona yake mazingira na kufahamu njia ya kwenda kule. Soma Zaidi...

image NIMLAUMU NANI ( sehemu ya tatu)
Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya kijana Frank na Amisa pia na wapenzi wawili ambao ni James na Amina. Soma Zaidi...

image Historia ya pango, aladini na kitabu
Soma Zaidi...

image Kwanini dirisha moja?
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Mtoto wa tajiri na maskini (sehemu ya pili)
Post hii inahusu zaidi watoto wa wawili ambapo mmoja ni mtoto wa tajiri na mwingine ni mtoto wa maskini. Soma Zaidi...

image Hadithi ya tabibu wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Kuelekea bonde la uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Hadithi iliyosimuliwa na mshona nguo
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Deni la mapenzi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Hadithi ya chongo watatu wa mfalme na wanawake wa Baghdad
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...