- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke?
- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke?
Jibu ndio:
- Kama ndoa hiyo imekusudiwa kumfanya mwanamke nguvu kazi ya uchumi, kuwa mwangalizi wa himaya ya mumewe tu, n.k.
- Kumzalia watoto wengi kama nguvu kazi ya uchumi, ulinzi wa mali yake tu, na kukosekana malengo ya ndoa, n.k.
- Kukosekana uadilifu na haki zake za msingi za kuolewa na kutekeleza majukumu yake ya msingi ili kufikia lengo kuumbwa kwake.
- Kunyanyaswa kama kupigwa, kutohurumiwa, kutukanwa, kutothaminiwa au kutengwa katika mahitaji ya kimaisha na kukidhi haja za kimwili pia.
Jibu hapana
- Kama ndoa inakusudiwa kumhifadhi na kumsitiri mwanamke na kila aina ya uovu na uchafu wa matamanio ya kimwili.
- Ikiwa ni kwa ajili ya kuwahifadhi na kuwasitiri wajane walioachwa na waume wao bado wakihitaji malezi ya ndoa.
- Ikiwa ni kuwanusuru, kuwahifadhi na kuwasitiri wanawake wema waliokosa waume wa kuwaoa wasijejiingiza katika machafu.
Sababu ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja
Mafunzo ya Qurβan (57:25) na (4:3) yanatoa sababu zifuatazo;
i. Ukewenza ni ruhusa kutoka kwa Allah (s.w), hivyo wanaume hawana budi kuipokea kwa lengo la kumcha Allah (s.w).
ii. Ukewenza ni fursa pekee kwa wanaume waislamu wema, waadilifu kuwaoa wanawake hawa ili wasijekuolewa na wanaume waovu.
iii. Ukewenza hupelekea hifadhi kwa wajane, mayatima na wanawake wema wanaohitaji hifadhi, malezi, n.k.
iv. Ukewenza unaruhusika tu kwa kufanya uadilifu kwa wanawake wote katika kukidhi matamanio ya kimwili.
Hekima ya Ukewenza (kuoa mke zaidi ya mmoja)
Kuna sababu za kibinafsi, kimaadili, kiuchumi na kijamii kama ifuatavyo;
i. Kama mke ni tasa, hawezi kuzaa:
- Ikiwa mume anahitaji mtoto wa kumrithi kisheria na mkewe hawezi kuzaa hanabudi kuoa mke mwingine lakini akae kwa wema na wanawake wote.
ii. Kama mke ana maradhi ya kudumu:
- Kama mke ana ugonjwa wa kudumu na hawezi kumkidhia mahitaji ya kimwili, mume hanabudi kuoa mke mwingine na kuishi nao kwa wema.
iii. Kuwahifadhi Wanawake wajane na walioachika:
- Wanaume wanalazimika kuoa wake zaidi ya mmoja kama kuna wanawake wajane waliofiwa na waume zao au walioacha.
iv. Kuwapa hifadhi wanawake waliozidi idadi ya wanaume katika jamii:
- Kama wanawake watakuwa wengi katika jamii, italazimika wanaume kuoa wake zaidi ya mmoja ili kuepusha kuenea machafu na maovu.
v. Kuwapa hifadhi na malezi watoto yatima:
- Mwanamke akifiwa na mume na ana watoto, malezi kamili hukosekana kama wazazi, hivyo kuolewa kunaboresha malezi kwa watoto walioachwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Maana ya UchumiMfumo wa maisha wa Kiislamu humuelekeza binaadamu kujenga na kudumisha uhusiano wake na Al-lah (s.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi hafifu na najisi ndogo.
Soma Zaidi...Yajuwe mambo ambayo yanapendeza kuyafanya wakati ukiwa umefunga Ramadhani.
Soma Zaidi...Unaweza kijiuliza ni kwa nini hasa kimepelekea kufaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa.
Soma Zaidi...Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.
Soma Zaidi...Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu.
Soma Zaidi...