Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii

Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii

4.

Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii

4. FAMILIA YA KIISLAMU

4.1. Ndoa Katika Uislamu

1. Maana ya Ndoa:

Kilugha: ni mkataba wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kufuata utaratibu uliowekwa na jamii.
Kisheria: ni mkataba wa hiari wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kuzingatia sharti na taratibu za Kiislamu.




2. Umuhimu wa ndoa katika Uislamu

Ni jambo lililokokotezwa sana kwani ni katika Sunnah za Mtume (s.a.w) yenye umuhimu ufuatao;
i. Kuhifadhi jamii na zinaa

- Ndoa hukinga wanandoa na jamii kwa ujumla na zinaa kwa kuhifadhi tupu zao na kukidhi matamanio baina yao.
Rejea Qurโ€™an (5:5), (4:24)



ii. Kuendeleza kizazi cha mwanaadamu kwa utaratibu mzuri

- Lengo la ndoa pia ni kuhifadhi, kutunza na kuendeleza kizazi cha mwanaadamu bila kuzaliana kiholela.
Rejea Qurโ€™an (4:1), (42:11)



iii. Kujenga mapenzi, huruma na ushirikiano katika familia

- Ndoa huleta utulivu katika moyo kati ya wanandoa na kupatikana huruma, mapenzi na ushirikiano baina yao
Rejea Qurโ€™an (30:21), (2:187)




iv. Kukuza uhusiano na udugu katika jamii

- Uhusiano na udugu kati ya wanafamilia walioana huimarika na kuongezeka zaidi kuwa ukoo, kabila, taifa, n.k
Rejea Qurโ€™an (25:54), (49:13)



v. Kukilea kizazi katika maadili

- Ndoa inakusudiwa kuwa kiungo cha kulea na kuelimisha kizazi katika tabia na maadili mema anayoyaridhia Allah (s.w).


vi. Kumuendeleza mwanaadamu kiuchumi

- Ndoa huchochea wanandoa na wanajamii kwa ujumla kujijenga kiuchumi ili kukidhi mahitaji muhimu ya kimaisha na kibinaadamu.
Rejea Qurโ€™an (6:151)



                   

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2836

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰5 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Nadharia ya uchumi wa kiislamu
Nadharia ya uchumi wa kiislamu

Dhana ya uchumi wa kiislamu imejegwa jui ya ukati na kati. Dhana hii imetofautiana sana na dhana nyinginezo kama ubepari na ujamaa.

Soma Zaidi...
Yaliyoharamishwa kwa mwenye kuwa katika ihram
Yaliyoharamishwa kwa mwenye kuwa katika ihram

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
namna ya kuswali 6
namna ya kuswali 6

Lugha ya Swala Lugha ya swala,kuanzia kwenye Takbira ya kuhirimia Swala mpaka kumalizia swala kwa Salaam, ni Kiarabu.

Soma Zaidi...
Zoezi la nne mada ya fiqh.
Zoezi la nne mada ya fiqh.

Maswali mbalimbali kuhusu fiqh.

Soma Zaidi...
sunnah za swala
sunnah za swala

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...