image

Ndoto ya mgonjwa, binti mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

NDOTO YA MGONJWA BINTI WA MFALME.

Nilipokuwa nimelala nilioa kana kwamba nipo katikati ya kundi kubwa la watu na wote ni wanume. Wote walikuwa wanagombania kuushika mkono wangu. Ila walishindwa kuupata kwa sababu nilipokuwa nipo nilizungukiwa na miba hivyo walishindwa kupita. Watu hawa walionekan kuminyana na miba ile bila mafanikio hata wakaanza kugombana na kulaumiana juu ya nani ameweka miba ile.

 

Wakiwa katika hali hiyo ghafla upepo mkubwa ulivuma ukiambatana na vumbi kubwa. Miti iliinama kwa upepo ule na wale watu wote wakatulia kwanza. Katika hali hiyo alitokea kijana mmoja mzuri aliyevaa mavazi meupe yenye kuvyovywa kwenye dahabu nyekundwu. Kwa hakika alinivutia sana. Kisha akawaambia wale watu kuwa wasigombane yeye ndiye aliyeweka ile miba, na hivyo hakuna hata mmoja ataweza kuivuka miba ile ila mpaka aitoe.

 

Mmoja kati ya wale watu akamuuliza ni kwa sababu gani ameamua kuweka miba ile. Akawajibu kuwa “kwa muda mrefu pacha wangu amekuwa akiulinda mkono wa huyu binti dhidi ya wabaya na mabaya. Lakini si muda mrefu amepoteza maisha kwa sababu ya huyu binti. Wale watu wakaanza kupiga makelele na kumwambia kuwa yeye ni muongo. Vipi itawezekana huyu binti asiyejuwa hata kushika silaha akamuuwa pacha wako. Kwakweli hatujasikia jambo kama hili.

 

Akawajibu kuwa huyu binti siku moja alipokuwa anachota maji kisimani sehemu ya mwili wake ilidondokea kisimani na kumkuta pacha wangu akiwa katika hali ya kupewa majikumu hivyo muda ule hakuwa na nguvu yoyote ya kujikinga. Hivyo aliungua mwili wake kwa sababu hiyo akapoteza maisha baada ya siku 9 toka tukio lile. Hivyo nikaweka miba hii na kuapa kuwa hakuna yeyote atakayeipita miba hii na kukuta mkono wa binti huyu muuaji wa pacha wangu.

 

Mtu mwingine kati ya wale watu akauliza “vipi sasa miba hii utaitowa lini, au ni lini utaweza kuushika mkono wake na kumtoa kizuizini”. akajibu kuwa mpaka sasa huyu binti alikuwa kwenye adhabu ya kumuua pacha wangu lakini kwa sasa adhabu imekwisha hivyo nitamtowa kwenye kizuizi hiki mbele ya macho yenu. Basi pale pale akazungumza maneno fulani kisha miba yote ikaondoka. Nilipokuwa nikitoka yule kijana akanishika mkono na kunitowa pale. Ila kabla ya kuondoka eneo lile ghafla akachomwa na mkuki na kufariki palepale.

 

Jambo hili liliwashangaza wale watu wengine na wakaanza kujiuliza nani amemuuwa. Mtu mmoja mwenye sura mbaya akatokea akiwa amepanda punda mweusi. Akazungumza kumwambia yul kijana “nilikuwa nakusubiri tu umtoe ili nimchukue mimi, wewe ni kijana mdogo lakini ulinishinda wa miba yako hii kwa hakika nilishindwa kupita ila sasa hakina wa kunizuia” basi palepale akanichukuwa na kunipeleka chini ya ardhi iliyopo nchi nisiyoijua. Ghafla nikasikia maumivu kwenye mgongo wangu na nikashituka kuoka usingizini. Hii ndiyo ndoto niliyoiota ewe mjuzi na muelewa wa hadithi za usiku.

 

Katika kuitafasiri ndoto ile akasema kuwa “umekuwa ukiposwa na watu wengi lakini hakuna alokubaliwa mpaka sasa, hii ni kutokana na jini aliyekuwa amekfunga usiolewe akisubiri apewe madaraka kwenye utawala wao ili akuchukuwe na akufanye mke wake. Jini huyu alikuwekea ulinzi mkubwa dhidi ya maradhi na wachawi katu usingeweza kudhuriwa hata. Alikuwekea kinga iliyofanana na kunga yake. Bila shaka ulipokwenda kuchota maji sehemu ya mwili wako iliyomdondokea ni nywele zako. Na kwa kuwa alikuwa akipokea amri hakuweza kudhibiti usito w nywele yako iliyojaa nguvu iliyotokana na kinga zake. Hivyo alipatwa na matatizo kama ndoto inavyo elezwa.

 

Utawala huu wa majini upo chini ya kisima hicho ulichokwenda kuchotea maji. Majini hawa walikuwa mapacha hivyo moacha wake kama ndoto zinavyoonesha kwa hasira na majonzi akakupa haya maradhi kama adhabu. Na bila shaka atakuja mwenyewe kukutibu kama ndoto inavyosema. Halikadalika pacha huyu unamfahamu na ulishawahi kukutana nae na anakupenda pia hivyo hataweza kukuua.

 

Ila pindi atakapo kutibu tukio kubwa litampata litakalopelekea mauti yake na kwa upande wako pia hautakuwa salama kama ulivyoona kwenye ndoto. Alivyomaliza kusema hayo akamwambia baba kuwa hii ni tafasiri ya ndoto ya binti yako ewe mtukufu mafalme. Basi baba aliingiwa na majonzi kwa tafasiri ile ila hakuwa na jinsi. Kwa hakika nilikumbuka kuwa nilipokuwa mdogo sura ile niloiona kwenye ndoto niliiona. Niliona mtoto anazunguruka kwenye kisima na nili[omfuata akasema amepotea.

 

Basi siku ya ilofuata asubuhi akaja mganga mmoja na akasema anaweza kunitibu, lakini akataka mfalme aweke ahadi juu ya kumuozesha pindi atakaponitibu. Baba alikubali, basi nilipomuona tu nilimjuwa kuwa ni yule nilomuona kwenye ndoto. Kwa hakika alikuwa ni kijana mtanashati na ni mzuri pia, nilikubaliana na wazo la baba la kuniozesha kama ataitibu. Ila sikuweza kumueleza baba kuwa huyu mdiye yule nilomuona wenye ndoto kwa kuhofia kuvunja ahadi ya kuniozesha kuokana na tafsiri ya ile ndoto.

 

Basi ilichukua nywele kumbe ni ile nywele yangu na kuichoma na kuniambia nijifunike shuka ili mosho wote wa ile nywele unipate mimi. Basi haukupita muda nilipiga ukelele mkali sana hata baba alishangaa, kisima kiliporomoka madongo na maji yalijaa kwenye kisima, kuku walitawanyuka na punda wakawa wanapiga kelele ovyoovyo. Nilipoteza fahamu na nisijue kilichofata baada ya hapo. Nilipokuja kuzinduka mikajikuta nimepona kabisa. Basi ahadi ikaendelea na nikaolewa na yule kijana.

 

Tuliishi pale nyumbani kwa raha kwa muda wa siku tatu. Siku ya nne asubuhi nyoka mkubwa alitoka kisimani mchana na watu walimshuhudia a kuja ndani akamuua mume wangu na kunimeza mimi. Sikujua nini kiliendelea kuhusu mwili wa mume wangu au nini kiliendelea baada ya pale. Nilikujakushituka siku tatu baadae na kujikuta nipo humu ndani. Huyu jini ameniweka humu na amenifanya mkewe na anakuja kila baada ya siku 40. ila nikiwa na shida nae au nikipata matatizi huwa nabonyeza hii pete ya mkufu na hapohapo atakuja. Hii ndio stori yangu ewe Habil makata kuni.

 

Basi niliposikia habari hii nilistajabu sana na kuona kumbe kuna watu wamepta makubwa kuliko hata mimi. Basi na mimi nikamueleza stori yangu hata nikafika pale. Basi tulikunywa na kufurahia pae ndani. Nilikunywa pombe na nilipokuwa nimelewa nikaivuta ile pete ya mkufu na kuanguka chin. Yule binti alipiga kelele na kusema umeniua na maisha yako yapo hatarini pia. Toka nje na ukimbie.

 

Basi muda uleule pale ndani pakawa na kiza kinene nikajitahidi kutoka nje na kiakumbuka kuwa nimesahau kiatu kimoja ndani. Sikujuwa kilichoendelea huko ndani ila nilipofika nyumbani niliishia kitandani. Haikupita muda ilifika mchana na akaja mtu mmoja kutaka kuni. Nilipotka moyo wangu ulitetemeka kwani sikupata kumjua mtu yule akaniuliza “asubuhi ya leo ulikuwa wapi” nikamjibu nilikuwa hapahapa leo sijatoka. Akanionesha kiatu changu akasema “hiki sio chakwako?” nilionekana kubabaika basi akapiga guu lake chini na hapo hapo upepo mkali ukanibeba.

 

Alinituwa ufukweni mbele ya yule binti na kumuuliza kama ananijua. Yule binti akakana na kusema kuwa hanijui na mimi pia nikakana kusema kuwa namjua. Basi jini yule akamchinja ule mwanamke na kunuiambia “sasa ni zamu yako”. nikaanza uomba msamaha lakini hakuonekana ni mwenye kusamehe. Nika mwambi “naomba unihurumie kama khalid alivyomuhurumia Jlid”. basi jini akauliza “kwani jalid alimfanya ni ni Khalid”. nikaanza kumsimulia kisa cha Khalid na Jalid kwa upole kma ifuatavyo;-





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1005


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kitabu Cha Hadithi ya jini
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Alif lela u lela 1
Alif lela u lela ni hadithi zilizosheheni utamu na machungu pamoja na visa vya wachawi na majinim soma sasa. Soma Zaidi...

Binti wa ndotoni
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Safari ya tatu ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya waziri aliyeadhibiwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Kitabu Cha Hadithi ya mvuvi
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Hadithi ya mji uliogeuzwa mawe
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Kiapo cha sultani
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Safari ya nne ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Kitabu Cha hadithi ya wanawake watatu
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

MWANZO WA USALITI
Download kitabu Hiki Bofya hapa USALITI UNANZA HAPA Baada ya kukaa pale siku moja nahodha akaamrisha chombo kiondoke pale na kurudi nyumbani. Soma Zaidi...