Nguo zinazovaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi nguo za kuvaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake, hizi ni nguo ambazo wahudumu wa afya wanapaswa kuzivaa wakati wa upasuaji kwa ajili ya kuwakinga na Maambukizi kati ya wahudumu wa afya na wagonjwa pia

Nguo zinazovaliwa kwenye chumba cha upasuaji.

1.Kofia

Hii ni mojawapo ya nguo inayokaliwa kwenye chumba cha upasuaji, kofia yenyewe huwa mara nyingi imeshinwa kwa nguo, kazi yake ni kuzuia nywele kutoka kwenye kichwa cha mhudumu kuingia kwa mgonjwa wakati wa upasuaji, kwa hiyo kila mhudumu anapaswa kuivaa hii kofia kwa kufanya hivyo Maambukizi yataweza kupungua na kuepuka kuwepo kwa magonjwa yadiyotegemewa.

 

2.Nguo nyingine ni Maski au kwa lugha nyingine tunaweza kuita Barakoa.

Mask au barakoa uvaliwa na kufunika sehemu za mdomo, pua kwa hiyo kazi yake ni kuzuia mate kudondoka wakati wa upasuaji au hewa kutoka mdomoni inaweza kuwa na wadudu kwa hiyo ikasababisha wadudu kuingia kwenye sehemu ambayo imefunguliwa na kuleta Maambukizi au pengine mhudumu anaweza kupiga chafya na kusababisha wadudu kusambaa, lakini kama kuna Maski hakuna kitu chochote kinachoweza kutokea mdomoni au puani.

 

3.Nguo nyingine ni apron.

Hivi ni nguo ambayo uvaliwa juu ya gauni, nguo hii kazi yake ni kuzuia damu au majimaji kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu, kwa sababu wakati mwingine mgonjwa anaweza kuwa na Maambukizi na yakifika kwa mhudumu moja kwa moja yanaweza kusababisha Maambukizi kwa mgonjwa kwa hiyo ni lazima mhudumu kuvaa hii apron ili kuepukana na Maambukizi.

 

4.Nguo nyingine ni gauni.

Hii nayo ni nguo inapaswa kuvaliwa wakati wa upasuaji kwa sababu ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu au kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa, kwa hiyo kila mhudumu ni lazima kuvaa hii nguo hili kuepukana na Maambukizi ya magonjwa mbalimbali yanayoweza kusambaa kwa damu au kwa maji maji kama vile Ukimwi, homa ya ini na magonjwa mengine mengi.

 

5.Nguo nyingine ni boot au viatu vilivyofunikwa.

Pia nazo zinapaswa kuvaliwa wakati wa upasuaji kwa sababu uzuia Maambukizi kwa mfano kama kuna sindano imedondoka chini kwa bahati mbaya isiweze kuingia moja kwa moja kwenye mwili bali Uchoma juu ya viatu kwa sababu pengine mgonjwa anaweza kuwa na magonjwa ya kuambukiza kama sindano ikichoma juu ya boot ni vizuri kuliko kuchoma moja kwa moja kwenye ngozi.

 

6.Nguo nyingine ni gloves.

Pia nazo uvaliwa wakati wa upasuaji kwa sababu uzuia maambukizi kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa na kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu, hizi gloves kama zikichafua inabidi zibadilishwe ili zivaliwe nyingine kwa kuepuka Maambukizi kwa hiyo nazo zinapaswa kuvaliwa kwa mda wake na kwa sheria zake.

 

 

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/02/07/Monday - 07:56:47 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 940


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Dondoo za afya 81-100
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dondoo za afya Soma Zaidi...

Nguo zinazovaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake
Posti hii inahusu zaidi nguo za kuvaliwa kwenye chumba cha upasuaji na kazi zake, hizi ni nguo ambazo wahudumu wa afya wanapaswa kuzivaa wakati wa upasuaji kwa ajili ya kuwakinga na Maambukizi kati ya wahudumu wa afya na wagonjwa pia Soma Zaidi...

Kauli za wataalamu wa afya
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu kauli mbalimbali za wataalamu wa afya Soma Zaidi...

Safari ya damu kwa Kila siku
Posti hii inakwenda kukuletea mfumo wa damu mwilini na safari zake za Kila siku Soma Zaidi...

Ijue timu ya upasuaji
Posti hii inahusu timu ya upasuaji hii ni timu ambayo inahusika katika chumba cha upasuaji, kwa sababu ya kutunza usafi na usalama chumba hiki kinapaswa juwa na timu ya watu wanne na walio na elimu kuhusu kazi hiyo. Soma Zaidi...

Zijue sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji
Post hii inahusu zaidi sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji kina sehemu kuu nne na sehemu hizo ufanya kazi tofauti tofauti kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Habari za uzima,nimesoma makala yako tumbo linaniuma upande wa kulia Ila sisikii Sana yenyewe Ila nikibonyeza na mkono ndio inauma yaani ni Kama nimegongwa sehem flani alafu Kuna maumivu lakini ni mpaka upaguse ndio una experience maumivu Kama Kuna namna
Kama unasumbuliwana tumbo upande wa kulia, kushoto, kitomvuni ama kuoande wa kuliavkwachini, basi muulizaji huyu atakupa uelewa. Soma Zaidi...

Umoja wa mataifa unazungumziaje afya
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo ya kiafya yanayozungumzwa na umoja wa mataifa Soma Zaidi...

Dondoo za afya 61-80
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dondoo za afya Soma Zaidi...

Mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji
Posti hii inahusu zaidi mambo yanayohitajika kabla ya kuanza upasuaji ni mambo muhimu ambayo yanapaswa kufanyika kwanza na baadaye upasuaji unaweza kuendelea. Soma Zaidi...

Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa Soma Zaidi...

ZIJUWE FIGO, KAZI ZA FIGO NA NAMNA YA KULINDA FIGO DHIDI YA MARADHI
Je unatambuwa namna fgo inavyofanya kazi, unazijuwa kazikuu za fogo mwilini, na je unajuwa namna ya kujilinda dhidi ya maradhi ya figo?. Basi makala hii itakujuza kuhusu masomo haya1 Soma Zaidi...