Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k
Nguzo za kuu za umama katika kipindi cha kujifungua na kulea watoto.
1.Mama akiwa katika kipindi cha kujifungua na kulea watoto katika kipindi hiki anapaswa kuwa na nguzo kuu muhimu zinazopaswa kumwongoza ili aweze kupata watoto wenye afya nzuri na makuzi mema pasipokuwa na magonjwa na vizuizi vyovyote wakati wa makuzi ya mtoto mpaka mtoto anafikia umri wa miaka mitano na kuzidi kwa hiyo zifuatazo ni nguzo kuu za umama.
2.Uzazi wa mpango.
Wazazi wote wawili wanapaswa kutumia uzazi wa mpango ambao wanaona unafaa kwao baada ya kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya, kwa kutumia uzazi wa mpango wazazi wanaweza kupata idadi ya watoto ambao wanawahitaji na watoto wanaweza kupata malezi muhimu na mapenzi kutoka kwa wazazi wao, kwa kutumia uzazi wa mpango uepusha kubwa na watoto wanaofuatana sana na kusababisha ukuaji wa watoto kubwa wa shida na kusababisha umaskini ambapo mama baada ya kufanya shughuli mbalimbali za kuongeza uchumi anatumia mda mwingi kulea watoto.
3.Kuhudhulia kliniki wakati wote wa ujauzito na baada ya kujifungua pale anampeleka mtoto.
Mama akibeba mimba tu anapaswa kwenda kliniki ili kuweza kuona maendeleo ya mimba na kupata elimu mbalimbali hasa kuhusu Dalili za hatari wakati wa ujauzito pia mama anapaswa kupima maambukizi ili aweze kumkinga mtoto na Maambukizi yoyote yale, kwa hiyo hata mama akijifungua anapaswa kupeleka mtoto wake kliniki ili apate chanjo mbalimbali za kumkinga na magonjwa kama vile kifua kikuu, kupooza na magonjwa mbalimbali, kwa hiyo akina Mama mnapaswa kuhudhuria kliniki kwa sababu kuna faida nyingi kwa Mama na mtoto pia.
4. Kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito.
Mama akiwa na mimba anapaswa kupima maambukizi yote kwa awamu mbili ya kwanza ni pale anapobeba mimba tu na wakati akiwa na miezi minane ya ujauzito hii ni kwa sababu ya kuepuka kumwambukiza mtoto akiwa kwenye tumbo la Mama, na wakati wa kujifungua kwa kumpatia mama dawa za kupunguza makali ya virus vya ukimwi na mtoto akizaliwa na Mama mwenye Maambukizi anapaswa kupewa dawa pindi anapozaliwa hata kama yeye hana Maambukizi kwa hiyo huwa kwenye uangalizi kwa kipindi cha miezi sita.
5.Uangalizi wa Mama na mtoto ndani ya masaa ishirini na manne.
Mama anapojifungua salamu huwa kwenye uangalizi ndani ya masaa ishirini na manne ili kuangalia kama kuna mabadiliko yoyote yanayoweza kujitokeza kwa mtoto na Mama pia kwa hiyo kama hakuna mabadiliko yoyote mama anaruhusiwa kutoka hospitalini na kama kuna mabadiliko yoyote Mama na mtoto watapaswa kutibiwa kufuatana na hali zao.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo zinaweza kujitokeza na zikaonesha kwamba mbegu za kiume ni dhaifu au ni chache.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kuhusu njia za uzazi wa mpango, uzazi wa mpango ni njia za kupanga uzazi Ili kupata idadi ya watoto unaohitaji
Soma Zaidi...Maumivu wakati wa tendo la ndoa kitaalamu huitwa dyspareunia.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.
Soma Zaidi...Kupungua kwa idadi ya mbegu za kiume kunamaanisha kuwa Majimaji (shahawa) unayotoa wakati wa kufika kileleni huwa na mbegu chache kuliko kawaida. Hesabu yako ya manii inachukuliwa kuwa chini kuliko kawaida ikiwa una chini ya mbegu milioni 15. Kuwa na idad
Soma Zaidi...Je na wewe ni moja kati ya wake ambao wanahitajivkujuwa siku za kupata mimba. Ama siku za competes mwanamke mimba. Post hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku 7 Hadi 14
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili.
Soma Zaidi...Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa
Soma Zaidi...